Tuesday, August 21, 2018

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Wanawake amewasili Nchini leo.

Mhe. Bi Phumzile Mlambo-Ngcuka akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga alipowasili Ofisini kwake kwa ajili ya mazungumzo kuhusu ushirikiano kati ya Tanzania na Shirika hilo.
Mhe. Balozi. Dkt Augustine Mahiga akiwa katika mazungumzo na Mhe Bi. Phumzile Mlango.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia wanawake, Mhe. Bi Phumzile Mlambo-Ngcuka akiwa ameongozana na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Katika Wizara ya mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,  Balozi Celestine Mushy mara baada ya kumpokea kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kwa ajili ya zaira ya kikazi Nchini kuanzia tarehe 21 hadi 24 Agosti, 2018


Mhe. Bi Phumzile Mlambo-Ngcuka  akimweleza jambo Balozi Mushy wakati wa mazungumzo yao mara baada ya kuwasili nchini


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.