Saturday, August 18, 2018

Tanzania yateuliwa rasmi kuwa Makamu Mwenyekiti wa SADC

Mkutano wa 38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), unaofanyika mjini Windhoek, Namibia, kuanzia tarehe 17 hadi 18 Agosti 2018, umemteua Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa Makamu Mwenyekiti wa SADC kwa kipindi cha Agosti 2018 mpaka Agosti 2019.

Kufuatia uteuzi huo, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atapewa rasmi jukumu la Uenyekiti wa SADC katika Mkutano mkuu ujao wa 39 utakaofanyika Tanzania mwezi Agosti 2019.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC unaofanyika mjini Windhoek, Namibia kuanzia tarehe 17 hadi 18 Agosti 2018.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akifuatilia ufunguzi wa mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali mjini Windhoek, Namibia. Kulia ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Jamhuri ya Afika Kusini, Mhe Lindiwe Sisuli.
Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof Adolf Mkenda akifuatilia hafla ya ufunguzi wa mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali mjini Windhoek, Namibia.
Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika, Dkt. Stergomena L. Tax akitoa hotua ya ufunguzi wa mkutano pamoja na taarifa ya mwaka ya utekelezaji wa Jumuiya ambapo alitumia fursa hiyo kuwashukuru viongozi waliomaliza muda na nchi wanachama kwa ushirikiano walioutoa katika utekelezaji wa malengo na mipango mbalimbali ya kanda.
Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini na Mwenyekiti wa SADC aliyemaliza muda, Mhe. Cyril Ramaphosa akikabidhi nafasi ya uenyekiti kwa mwenyekiti mpya na Rais wa Jamhuri ya Namibia, Mhe. Hage Geingob.

Mwenyekiti wa SADC na Rais wa Namibia, Mhe. Hage Geingob akihutubia mara baada ya kukabidhiwa nafasi ya uenyekiti wa SADC mjini Windhoek, Namibia ambapo aliishukuru Serikali ya Afrika kusini kwa uongozi mahiri kwa kipindi chote cha uongozi wake na aliahidi kushirikiana na wanachama wote katika kuiletea kanda maendeleo na kupunguza umasikini.
Wanafunzi walioshinda shindano la insha wakiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mtendaji wa SADC, Dkt. Stergomena Tax na Mwenyekiti wa SADC, Mhe. Cyril Ramaphosa njini Windhoek ,Namibia.

Sehemu nyingine ya Wanafunzi walioshinda shindano la insha wakiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mtendaji wa SADC, Dkt. Stergomena L. Tax na Mwenyekiti wa SADC, Mhe. Cyril Ramaphosa njini Windhoek ,Namibia.

Waandishi wa habari walioshinda shindano la mwandishi bora wa SADC katika radio, gazeti na televisheni wakiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mtendaji wa SADC, Dkt. Stergomena Tax na Mwenyekiti wa SADC, Mhe. Cyril Ramaphosa njini Windhoek ,Namibia.
Kutoka kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango (SMZ), Bw. Ali Juma Khamis  pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikaiano wa Afrika Mashariki , Balozi Innocent Shiyo wakifuatilia mkutano.
Kutoka Kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Joseph Nyamhanga pamoja na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Khatibu Kazungu wakifuatilia mkutano.
Wa pili kutoka kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Bw. Edwin Mhede pamoja na Afisa Mambo ya Nje Mwandamizi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Agness kayola (kulia) wakifuatilia mkutano.

Kutoka kustoto ni Balozi wa Tanzania nchini Namibia mwenye makazi yake nchini Afrika Kusini, Mhe. Sylisvester Ambokile na Naibu Mwanasheria Mkuu, Bw. Evaristo Longopa wakifuatilia hafla ya ufunguzi wa mkutano.


Ujumbe kutoka Serikali ya Tanzania ukufuatilia mkutano.

Sehemu nyingine ya ujumbe huo ukifuatilia mkutano.


Waasisi wa SADC wakiwa wamesimama wakati wimbo wa Tiafa wa Namibia  na wimbo wa SADC ukipigwa, kushoto ni Rais mstaafu wa kwanza  wa Jamhuri ya Namibia, Mhe. Sam Nujoma na kulia kwake ni Rais wa mstaafu wa kwanza wa Jamhuri ya Msumbiji, Mhe. Joaquim Chissano.

Wake za Waheshimiwa marais walifuatilia hafla ufunguzi wa Mkutano

Picha ya pamoja



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.