Friday, August 24, 2018

Waziri Mahiga amuaga Balozi wa Ubelgiji nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb.), akizungumza kwenye hafla ya kumuaga Balozi wa Ubelgiji aliyemaliza muda wa kuiwakilisha nchi yake hapa Tanzania Mhe. Paul Cartier (wa tatu kutoka kulia). Dkt. Mahiga alitumia fursa hiyo kumpongeza kwa kuiwakilisha nchi yake vyema hapa Tanzania. Hafla hiyo imehudhuriwa pia na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo,  Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (hayupo pichani), Kaimu Mkurugenzi Idara ya  Ulaya na Amerika, Bw.Jestas  Nyamanga na baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Hafla hiyo ilifanyika hivi karibuni katika Hoteli ya Hyatt Regency  jijini Dar es Salaam.
Balozi Paul Cartier naye alipata fursa ya kuishukuru Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, kwa ushirikiano aliokuwa akipata kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. 
Mhe. Mwakyembe akisikiliza hotuba zilizokuwa zikitolewa na Dkt, Mahiga pamoja na Mhe.Cartier
Dkt. Mahiga akimkabidhi Balozi Cartier zawadi yenye mchoro wa Hifadhi ya  Mlima Kilimanjaro kama ukumbusho wa moja ya vivutio vya utalii vilivyopo Tanzania
Waziri Mahiga (katikati), Balozi Cartier (wa nne kutoka kulia), Waziri Mwakyembe (wa tatu kutoka kulia), Bw. Nyamanga (wa tatu kutoka kushoto), Mke wa Balozi Cartier (wa nne kutoka kushoto) pamoja na watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa katika picha ya pamoja.

 





No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.