Friday, August 10, 2018

Kaimu Balozi wa Kuwait nchini Tanzania awasilisha ujumbe Wizarani

Bw. Suleiman Saleh Kaimu Mkurugenzi Idara Mashariki ya Kati, akisalimiana na Bw. Nasser Bader Al Ramzi Kaimu Balozi wa Kuwait nchini Tanzania walipokutana kwa mazungumzo jijini Dar es Salaam.

Katika mazungumzo hayo Bw. Nasser ameeleza kuwa Ubalozi unaandaa uataraibu wa kutembelea na kukagua maendelea ya miradi mbalimbali inayofadhiliwa Kuwait nchini Tanzania. Kaimu Mkurugenzi amemuhakikishia kuwa Wizara na Serikali kwa ujumla watampa ushirikiano wa hali ya juu wakati wote wa utelezaji wa majukumu yake nchi.

Aidha Bw.Nasser amewasilisha ujumbe maalumu kutoka nchini Kuwait kwa Serikali ya Tanzania 

Bw. Suleiman Saleh Kaimu Mkurugenzi Idara Mashariki ya Kati (katika) akimsikiliza Bw. Nasser Bader Al Ramzi Kaimu Balozi wa Kuwait nchini Tanzania  (kulia) walipokutana kwa mazungumzo jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kulia ni Bw. Hangi Mgaka Afisa Mambo ya Nje akifuatilia  mazungumzo

Bw. Suleiman Saleh Kaimu Mkurugenzi Idara Mashariki ya Kati akipokea ujumbe maalum kutoka kwa Bw. Nasser Kaimu Balozi wa Kuwait nchini Tanzania kushoto ni Bw. Hangi Mgaka Afisa Mambo ya Nje

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.