Friday, August 10, 2018

Balozi wa Saudi Arabia akutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa Wizara

Mhe. Balozi Dkt.Augustine Mahiga Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (kushoto), akisalimiana na Mhe. Mohamed Ben Mansour Al Malek Balozi wa Saudi Arabia nchini Tanzania (kulia) walipokutana kwa mazungumzo jijini Dar es Salaam. Mazungumzo baina ya Viongozi wa Wizara na Balozi Mohamed yalijikita katika kuendeleza na kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia baina ya Mataifa haya mawili (Tanzania na Saudi Arabia).

Aidha viongozi hao wamekubaliana kukamilisha maandalizi ya kongamano la biashara litakalo husisha wafanyabiashara na wadau wengine kutoka Saudi Arabia na Tanzania. Balozi Mohamed amebainisha kuwa ujumbe kutoka Saudi Arabia utakuwa na wafanyabiashara zaidi ya 40 wakiongozwa na Waziri wa Biashara wa Saudi Arabia.

 Aidha Balozi Mohamed ameonesha nia yakuanzisha  majadiliano kati ya Tanzania na Saudi Arabia ya kuanzisha safari za ndege za moja kwa moja kutoka Tanzania kwenda Saudi Arabia kwa lengo la kukuza biashara baina ya nchi hizi mbili.
Mhe. Balozi Dkt.Augustine Mahiga Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Balozi Mohamed Ben Mansour Al Malek Balozi wa Saudi Arabia nchini Tanzania, Bw. Suleiman Saleh, Kaimu Mkurugenzi Idara ya Mashariki ya Kati (wa kwanza kulia) na Bw. Hangi Mgaka Afisa Mambo ya Nje (wa kwanza kushoto)

Bw. Suleiman Saleh, Kaimu Mkurugenzi Idara ya Mashariki ya Kati, akisalimiana na Mhe. Balozi Mohamed Ben Mansour Al Malek Balozi wa Saudi Arabia nchini Tanzania walipokutana kwa mazungumzo jijini Dar es Salaam

Balozi Ramadhani Mwinyi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akisalimiana Balozi Mohamed Ben Mansour Al Malek Balozi wa Saudi Arabia nchini Tanzania, walipokutana kwa mazungumzo jijini Dar es Salaam

Balozi Ramadhani Mwinyi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (wa pili kushoto) akiwa katika mazungumzo na Ben Mansour Al Malek Balozi wa Saudi Arabia nchini Tanzania (wa pili kulia) 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.