Monday, August 27, 2018

Makamu wa Rais ashiriki sherehe za kuapishwa Majaji wapya wa Mahakama ya Afrika

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Majaji wapya wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu ambao wameapishwa jijini Arusha. Kutoka kushoto ni Mhe. Jaji Amani Aboud (Tanzania), Mhe.Jaji Blaise Tchikaye (Congo) na kulia ni Mhe. Jaji Stella Isibhakhonem Anukam (Nigeria) 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa hafla ya kuapishwa kwa majaji wapya watatu wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu jijini Arusha.


Viongozi Mablimbali wa Serikali akiwemo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (wa pili kulia) wakimsiliza  Mhe. Samia Suluhu Hassan alipokuwa akihutubia kwenye hafla ya kuapishwa majaji watatu wapya wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu jijini Arusha. 
Sehemu ya Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia hotuba ya Mhe. Samiha Suluhu Hassan 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea zawadi kutoka kwa  Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu Mhe. Jaji Sylvain Ore mara baada ya kuapishwa kwa Majaji wapya watatu wa mahakama hiyo jijini Arusha.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akimpongeza Mhe. Jaji Stella Isibhakhonem Anukam (Nigeria) mara baada ya kuapishwa
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bibi Caroline Chipeta akisalimiana na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk Adelardus Kilangi katikati ni Afisa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Wilbroad Kayombo
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samiha Suluhu Hassan na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga (Mb.), wakiwa kwenye picha ya pamoja na Majaji wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu jijini Arusha. 























No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.