Friday, August 17, 2018

Tamasha la kwanza la Michezo la Afrika Mashariki lazinduliwa Bujumbura, Burundi.

Brigadia  Generali Mary Hiki akizungumza na wanamichezo kutoka (Tanzania hawapo pichani) washiriki wa Tamasha la Kwanza la Michezo la Afrika Mashariki linaloendelea jijini Bujumbura, Burundi. Brigadia Generali Hiki ambaye anahudumu katika Ubalozi wa Tanzania nchini Burundi alizungumza na wanamichezo hao kwaniaba Kaimu ya Balozi.
Tamasha hili linalofanyika kwa mara ya kwanza nchi Burundi limetokana na maagizo ya Mkutano wa 35 wa Baraza la Mawaziri la Afrika Mashariki.

Tamasha hili lenye kauli mbiu "kujenga Jumuiya ya Afrika Mashariki na amani kupitia michezo" linafanyika kuanzia terehe 16 hadi 30 Agosti, 2018. Washiriki zaidi 1000 kutoka nchi wananchama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki watashiriki kwenye michezo mbalimbali ya tamasha hili.

Tanzania imewakilishwa na jumla ya wanamichezo 58 ambao watashiriki katika michezo ya mpira wa pete, mpira wa miguu, riadha na karatee.

Tamasha hili limefunguliwa tarehe 16 Agosti 2018 na Mhe. Dkt. Joseph Butore Makamu wa Pili wa Rais wa Jamhuri ya Burundi, katika viwanja vya Sekondari vya SOS jijini Burundi na kuhudhuriwa na viongozi na watendaji waserikali kutoka nchi wanachama. 

Meza kuu ni Mhe. Dkt. Joseph Butore Makamu wa Pili wa Rais wa Jamhuri ya Burundi (wa pili kulia) Bw.Liberatus Mfumukeko (wapili kushoto)  Katibu Mkuu Seretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Ali Kirunda Kivenjija Naibu wa Pili wa Waziri Mkuu na Waziri wa Masuala ya Afrika Mashariki kutoka Uganda (wa kwanza kulia) na Mhe. Jacques Enyenimigabo Waziri wa Vijana na Michezo wa Burundi (wa kwanza kushoto) wakiwa wamesimama wakati wimbo wa Taifa wa Burundi ukipigwa kwenye hafla ya ufunguzi wa Tamasha la Kwanza la Michezo la Afrika Mashariki

Sehemu ya watendaji na viongozi wa Serikali wa nchi Wanachama wakiwa wamesimama wakati wimbo wa Taifa wa Burundi ukipigwa kwenye ufunguzi wa Tamasha la Michezo

Wanamichezo kutoka Tanzania wakipita kwa furaha mbele ya jukwaa kuu kwenye hafla ya ufunguzi wa Tamasha la Kwanza la Michezo la Afrika Mashariki

Makamu wa Rais, Mhe Samia Suluhu Hassan aongoza ujumbe wa Tanzania katika mkutano wa Wakuu wa Nchi na Seriikali wa SADC wanaounda Utatu wa Asasi ya Ushirikiano wa Siasa, ulinzi na Usalama.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa katika mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) wanaounda Utatu wa Asasi ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama uliofanyika mjini Windhoek, Namibia tarehe 16 Agosti 2018. 
Kutoka kushoto ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda wakifuatilia mkutano.

Mhe. Samia Suluhu Hassan amemuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli katika mkutano huu pamoja  na Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC utakaofanyika tarehe 17 na 18 Agosti 2018.

Mkutano huu umehusisha Wakuu wa Nchi na Serikali wanaounda Utatu huo ambao ni Mheshimiwa João Manuel Gonçalves Lourenço, Rais wa Angola  na Mwenyekiti wa sasa wa SADC organ; Mheshimiwa Edgar Chagwa Lungu, Rais wa Jamhuri ya Zambia  na Makamu Mwenyekiti wa SADC Organ na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akimuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ambaye ni Mwenyekiti wa SADC Organ aliyemaliza muda wake.

 Mkutano huu umejadili taarifa ya hali ya siasa, ulinzi na usalama katika kanda kwa kipindi cha mwaka mmoja uliopita wa Agosti 2017 hadi Agosti 2018.

Agenda nyingine zilizojadiliwa katika mkutano huo ni pamoja na; taarifa ya utekelezaji wa maazimio ya SADC kuhusu kuimarisha hali ya siasa, ulinzi na usalama katika falme ya lesotho, hali ya siasa na usalama katika jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC),hali ya siasa na usalama nchini Madagasca,hali ya kidemokrasia katika kanda na taarifa ya uchaguzi mkuu kwa nchi wanachama ambao ni Madagasca, DRC na Eswatini.

vilevile mkutano huu umejadili kuhusiana na ujenzi wa sanamu ya Mwalimu Julius Nyerere iliyopendekezwa kujengwa katika jengo la Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika mjini Addis Ababa Ethiopia pamoja na majukumu ambayo serikali ya Tanzania imepewa katika kusimamia zoezi hilo linakamailika kwa wakati.

Makamu wa Rais. Mhe. Samia Suluhu Hassan akijadili jambo na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Innocent Shiyo wakati wa hafla ya ufunguzi wa mkutano huo.

Wajumbe wa Serikali ya Tanzania na Zambia wakifuatitilia hafla ya ufunguzi wa mkutano. Kulia kwa Makamu wa Rais ni Rais wa Jamhuri ya Zambia, Mhe. Edgar Chagwa Lungu


Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika, Dkt. Stergomena L.Tax (kulia) akitoa hotuba ya ufunguzi wa mkutano. Kushoto ni Rais wa Jamhuri ya Namibia na Mwenyekiti wa Asasi ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama.

Mhe. Waziri Mahiga (kati) akijadili jambo na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda (kulia) na Balozi Shiyo (kushoto) 

Mhe. Makamu wa Rais akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Mhe. Joseph Kabila kabla ya kuanza kwa mkutano huo. 

Thursday, August 16, 2018

CLARIFICATION ON MISLEADING RUMOURS ON THE ON-GOING VOLUNTARY REPATRIATION EXERCISE OF BURUNDIAN REFUGEES FROM TANZANIA


PRESS RELEASE

CLARIFICATION ON SOME MISLEADING RUMOURS BEING SPREAD REGARDING THE ON-GOING VOLUNTARY REPATRIATION EXERCISE OF BURUNDIAN REFUGEES FROM TANZANIA

1.0      INTRODUCTION

For more than five decades, The United Republic of Tanzania has been receiving and hosting refugees from different countries. Tanzania remains committed in finding durable solutions for these refugees, which have included naturalizing more than 250,000, of whom 162,156 were Burundians who entered Tanzania in 1972. In the same vein, Tanzania has assisted repatriation of refugees to their countries of origin whenever peace, security and stability were restored. Tanzania has also been in the forefront in facilitating resettlement of refugees to third countries, including the United States (25,094), Canada (2,278) and Australia (1,969).

In fulfilling its international obligation of providing safe haven to refugees, Tanzania has been doing the following:
    i.    Receiving asylum seekers;
  ii.    Providing sanctuary - places to live and protection; and
iii.    Finding durable solutions for refugees.

All these responsibilities are undertaken in line with the natinal laws and international instruments.

From April 2015, Tanzania started to receive an influx of refugees from Burundi due to political instability following the general elections. The influx led to the creation of two new refugee camps in Western Tanzania at Nduta and Mtendeli. As of 1 August 2018, the number of Burundian refugees hosted at Nduta, Mtendeli and Nyarugusu camps totaled 213,562.

2.0      PEACE, SECURITY AND STABILITY IN BURUNDI AND THE COMMENCEMENT OF VOLUNTARY REPATRIATION OF REFUGEES

Between May 2016 and July 2017, a substantial number of Burundian refugees started returning to their country of origin and many requested to be registered and assisted to voluntarily repatriate. When H.E. Dr. John Pombe Joseph Magufuli, President of the United Republic of Tanzania, and H.E. Pierre Nkurunzinza, President of the Republic of Burundi met in July 2017, already 6,000 Burundian refugees had registered for voluntary repatriation.

Following the delays in assisting the repatriation of the registered refugees, some of the refugees in Nduta camp rioted and, as a result, various properties, including vehicles and infrastructure, were destroyed.

Subsequent to many Burundian refugees starting to return to their country, and more than 12,000 to have registered for voluntary repatriation, the Government of Tanzania convened the first tripartite meeting (Tripartite Commission Meeting) involving Tanzania, Burundi and UNHCR, which took place in Dar es Salaam on 31 August 2017. The meeting agreed, among other things, to repatriate the 12,000 refugees by 31 December 2017. However, by the set date, a total of 13,102 refugees who had voluntarily registered were repatriated safely and in dignity.

Following the great successes of the outcomes of the first Tripartite Commission Meeting, the Government of Burundi convened the second Tripartite Commission Meeting in Bujumbura, Burundi on 28 March 2018. The meeting resolved to repatriate 72,000 voluntarily registered Burundian refugees by 31 December 2018.

The exercise of voluntary repatriation of refugees has continued to be conducted with due regard of safety, dignity and human rights. All the repatriated refugees are well received by the authorities in Burundi, in collaboration with UNHCR, IOM, WFP and other relevant stakeholders, and they are taken up to their places of domicile.

3.0      POSITIVE RESPONSE OF THE VOLUNTARY REPATRIATION EXERCISE

Up until 9 August 2018, a total of 42,463 Burundian refugees were already assisted to repatriate, while 30,401 refugees had been voluntarily registered, and were eagerly waiting to be assisted to repatriate.

So far, there are no records of any Burundian refugee returning to Tanzania after their repatriation. This, among others, bears testimony to the presence of peace, security and political stability in Burundi.

The involvement of relevant stakeholders is evidence that the exercise is being carried out transparently, and in compliance with international standards of human rights. All the required steps involved in voluntary repatriation are appropriately adhered to.

Furthermore, during the Bujumbura Tripartite Commission Meeting in March 2018, the Government of Burundi informed that they have protected and reserved all the properties that were left behind by the refugees, and that the same are given back to the owners upon their return. It is in this regard that, all refugees who have returned home have found and repossessed their properties, including farms and houses.

From 27 to 29 June 2018, the Ambassadors representing European countries in Tanzania visited Kigoma. The visit took them also to Nduta refugee camp, where they witnessed the voluntary repatriation exercise, and also had an opportunity to talk to refugees, and other stakeholders, regarding the exercise and they witnessed the urge of refugees to return to their home country.

Refugees who voluntarily repatriate are assisted to do so in busses and their belongings are transported in trucks. In addition, they are provided with three-months food ration upon arrival in Burundi.

On 18 May 2018, Burundians held a referendum for constitutional amendment. The exercise was conducted peacefully, and no group has contested the results. This is an indication of the strengthened national unity, and restoration of peace and stability in Burundi.

4.0      APPEAL OF THE GOVERNMENT OF TANZANIA TO THE INTERNATIONAL COMMUNITY

Through Tanzania Missions Abroad, particularly some of those in Western Europe, the Government of Tanzania has been informed of existence of some groups of people resident in those countries that are spreading preposterous rumors, that Tanzania is forcefully repatriating Burundian refugees. This is contrary to the truth, and we see this to be designed to undermine the successes of the on-going voluntary repatriation exercise.

The Government of Tanzania calls upon the international community to ignore the rumors, and instead support the on-going voluntary repatriation exercise, which is being conducted with due respect to human dignity. The Government urges the international community to continue providing the much-needed financial resources for the on-going voluntary repatriation exercise.

The Government of Tanzania calls on all the Burundian refugees to continue to register for voluntary repatriation so that they can go and participate in building their country, where peace and security have now returned.


Issued by: Government Communication Unit
Ministry of Foreign Affairs and East African
Cooperation, Dodoma
16th August, 2018

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan awasili mjini Windhoek, Namibia kushiriki mkutano wa 38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amewasili leo tarehe 15 Agosti 2018 katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Hosea Kutako mjini Windhoek, Namibia ambapo atamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) utakaofanyika tarehe 17 na 18 Agosti 2018. 
Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na mawaziri wa Serikali ya Namibia waliowasili kumpokea katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Hosea Kutako mjini Windhoek, Namibia. wa kwanza kulia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Christine !!Hoebes na wa kwanza kushoto ni Waziri wa Elimu ya juu, Mafunzo na Ubunifu, Mhe. Dkt Itah Kandjii-Murangi.

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako mjini Windhoek,Namibia.

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako mjini Windhoek,Namibia.

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango wa Serkali ya Mapinduzi Zanzibar, Bw. Ali Khamis Juma mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako mjini Windhoek,Namibia.

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Namibia mwenye makazi yake nchini Afrika Kusini, Mhe. Sylivester Ambokile mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako mjini Windhoek,Namibia.
Makamu wa Rais , Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana Naibu Mwanasheria Mkuu, Dkt. Evaristo Longopa mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako mjini Windhoek, Namibia.

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Balozi wa Namibia nchini Tanzania, Mhe. Theresia Samaria mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako mjini Windhoek,Namibia.
Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Bw. Edwin Mhede mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataiafa wa Hosea wa Kutako mjini Windhoek, Namibia.
Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Khatibu Kazungu mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako mjini Windhoek,Namibia.

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na   Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Innocent Shiyo mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako mjini Windhoek,Namibia.
Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Afisa Mambo ya Nje Mwandamizi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Agness Kayola mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako mjini Windhoek,Namibia.
Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Afisa Mambo ya Nje, Bi. Zulekha Fundi mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Hosea Kutako mjini Windhoek,Namibia.

Wednesday, August 15, 2018

Ubalozi wa Tanzania nchini Korea waandaa kongamano kuhamasisha wawekezaji sekta ya afya

Mgeni Rasmi katika Kongamano la kuhamasisha uwekezaji katika viwanda vya madawa na vifaa tiba nchini Bw. Geoffrey Mwambe, Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji (TIC) akitoa hotuba ya ufunguzi, kwa niaba ya Mhe. Ummy Ally Mwalimu (Mb), Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto, wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.   

Picha ya pamoja meza kuu: Kutoka kushoto: Makamu Mwenyekiti wa Korea-Africa Foundation (KAF), Mkurugenzi Mtendaji wa TIC, Bw. Geoffrey Mwambe, Balozi wa Tanzania Korea Mhe. Matilda Swilla Masuka, “Congressman” KIM Gyu-hwan, Rais wa KAF, Balozi Yeon-ho CHOI, na mwisho kulia ni Katibu Mtendaji wa Chama cha watengenezaji madawa (TAPI), Bw. Abbasi S. Mohamed.

Balozi wa Tanzania nchini Korea Kusini, Mhe. Matilda Swilla Masuka akitoa neno la ukaribisho katika Kongamano hilo.


Rais wa “Korea-Africa Foundation” waandaaji wenza wa Kongamano hilo, Balozi CHOI, Yeon-ho, akitoa neno katika hafla ya ufunguzi.


“Congressman” na Katibu wa “National Assembly Forum for Africa’s New Era” katika Bunge la Jamhuri ya Korea, Mhe. KIM, Gyu-hwan akitoa salamu za pongezi katika Kongamano hilo.  

 
Picha ya Pamoja ikijumuisha meza kuu na watoa mada kutoka: TIC, TFDA, MSD, Korea Health Industry Development Institute (KHIDI) na “Korea Medical Devices Industrial Association”.

Add caption

Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa TIC Bw. Geoffrey Mwambe ulipokutana na Kampuni ya LS watengenezaji wakubwa wa Matrekta na vifaa vya kilimo nchini Korea Kusini wenye lengo la kupanua wigo wa biashara kwa kuwa na uwakilishi na pia kuwekeza kwenye kiwanda “Assembly Plant”. 

Sehemu ya ujumbe kutoka Tanzania wakiwa na mwenyeji wao Balozi Matilda Swilla Masuka, baada ya kufanikisha Kongamano hilo la aina yake na lililovutia makampuni ya madawa na vifaa tiba zaidi ya 100.

Ujumbe kutoka Tanzania ukiwa katika picha ya pamoja na Wana Diaspora ambao walishiriki kikamilifu katika Kongamano hilo la kuhamasisha wawekezaji katika viwanda vya madawa na vifaa tiba.

Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa TIC, Bw. Geoffrey Mwambe, ulipotembelea Kampuni ya kutengeneza Madawa ya Celltrion, na kujionea shughuli mbalimbali za kampuni hiyo. Celltrion ni kampuni maarufu na inashika Na.1 nchini Korea katika “ sekta ya Bio-pharmacy”. Wakati za ziara hiyo ujumbe wa Tanzania uliambatana na Balozi wa Tanzania Korea, Mhe. Matilda Swilla Masuka, na Rais wa “Korea-Afrika Foundation”, Balozi Yeon-ho CHOI

===================================================================
KONGAMANO LA BIASHARA NA UWEKEZAJI
KUHAMASISHA WADAU WA MADAWA NA VIFAA TIBA KUWEKEZA NCHINI TANZANIA LAFANYIKA SEOUL, KOREA

Ubalozi wa Tanzania uliopo Seoul nchini Korea kwa kushirikiana na “Korea-Africa Foundation” na “Korea Chamber of Commerce and Industry” uliandaa Kongamano la Biashara na Uwekezaji kwa wadau wa sekta ya Afya lililofanyika Seoul, Jamhuri ya Korea.  Kongamano hilo la aina yake, liliandaliwa ili kuunga mkono juhudi za Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuboresha sekta ya Afya.

Kongamano hilo lililenga kuhamasisha uanzishwaji wa viwanda vya madawa na vifaa tiba nchini Tanzania, lilihudhuriwa na makampuni zaidi ya 100, kutoka pande zote mbili ikijumuisha: Makampuni ya utengenezaji madawa na vifaa tiba; Vyuo Vikuu; Taasisi za utafiti; Hospitali; Vyama vya watengenezaji wa madawa na vifaa tiba; Makampuni kutoka katika sekta binafsi; na Diaspora wa Tanzania waliopo Seoul.


Wakati wa Kongamano hilo, mada mbalimbali ziliwasilishwa zikijumuisha: Fursa zilizopo Tanzania katika sekta ya utengenezaji wa madawa na vifaa tiba; Mazingira ya ufanyaji biashara na vivutio “incentives” vinavyotolewa na Serikali; Hali ya soko na uhitaji (Market Potentiality); Taratibu za kufuatwa katika uingizwaji wa bidhaa za madawa na uanzishwaji wa viwanda husika; na Utayari wa sekta binafsi katika kushirikiana na wenzao wa Korea katika biashara na ubia katika viwanda vya madawa na vifaa tiba.

Kongamano hilo lilijumuisha wadau kutoka Wizara na Taasisi za kuitendaji za hapa nchini ikiwa ni pamoja na  Wizara ya Afya; Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki; Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji; Kituo cha Uwekezaji (TIC); MSD; TFDA, na Chama cha wenye Viwanda vya Dawa Tanzania (Tanzania Association Pharmaceutical Industries-TAPI).


Kwa upande wa Korea wawakilishi walitoka  Vyama vya watengenezaji wa madawa na vifaa tiba walitoa mada iliyokuwa na lengo la kubadilishana uzoefu na upande wa Tanzania. Kongamano lilihitimishwa kwa B2B, ambapo makampuni na Taasisi zilikutana kujadiliana zaidi fursa, maeneo ya ushirikiano, na kupata ufafanuzi wa kina katika maeneo mbalimbali; na baadaye kutembelea Makampuni ya Madawa.       





Ziara ya Kikazi ya Chuo cha Diplomasia nchini India.


Chuo cha Diplomasia Tanzania (Center for Foreign Relation -CFR) wamefanya ziara ya kikazi nchini India kuanzia tarehe 13-15 Agosti 2018. Ziara hiyo imekuja kufuatia mwaliko wa Taasisi ya Mafunzo ya Kidiplomasia ya India (Foreign Service Institute-FSI), na ililenga kujua shughuli za FSI na taasisi zinazoshirikiana nazo, pamoja na kujadiliana juu ya uwezekano wa kuingia katika makubaliano ya ushirikiano. 
Wajumbe wa CFR waliongozwa na Balozi Ombeni Sefue, Katibu Mkuu Kiongozi (Mst.), ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya CFR. Wajumbe wengine walikuwa ni pamoja na Kaimu Mkuu wa cha  Diplomasia (CFR), Dr Bernard Achiula, Dr Lucy Shule wa CFR, Dr Richard Mbunda kutoka UDSM, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia (DAA), Bibi Justa Nyange. Kutoka ubalozi wa Tanzania nchini India, alikuwepo Balozi Baraka Luvanda na Bibi Natihaika Msuya, Afisa Mambo ya Nje.

 Aidha, wajumbe hao walipata fursa ya kutoa mihadhara katika Kituo cha Stadi za Masuala ya Afrika katika Chuo Kikuu cha Nehru, Taasisi ya Stadi za Masuala ya Ulinzi na Usalama (IDSA) pamoja na Taasisi ya Tafiti Mahususi kuhusu ushirikiano baina ya Nchi za Kusini (South Cooperation Research Information System-RIS).
Kwa ujumla, ziara hiyo imekuwa ya mafanikio makubwa ambapo taasisi wenyeji zimeonesha dhamira ya dhati ya kushirikiana na CFR katika kujenga uwezo wa wanadiplomasia wa Tanzania.
Balozi Ombeni Sefue akimkabidhi  Mkuu wa Taasisi ya Stadi za Masuala ya Afrika, Profesa Ajay Dubey zawadi ya Kinyago.


Newly elected Member of Parliament in Pakistan with African Origin.



Tanzeela Qambrani, an African- Pakistanis woman whose ancestors originate from Tanzania has been elected as a Member of Parliament in Pakistan. She was nominated by the Pakistan People Party (PPP).  Qambrani has been elected to a special seat for women in the provincial parliament in Sindh. She aims at eliminating the stigma attached to her community, known as the Habashi, Sibbi or Sheedi who are the descendants of the Bantu people from Africa.

Tuesday, August 14, 2018

Wajumbe wa Mauritius wa wasili nchini kuangalia maeneo ya Uwekezaji wa viwanda vya sukari.



Ujumbe wa Serikali ya Mauritius ukiongozwa na Balozi wao mwenye Makazi yake Mjini Maputo, Msumbiji Mhe. Jean Pierre Jhumun umewasili nchini kwa ajili ya kukamilisha taratibu za uwekezaji wa viwanda vya sukari.

Ukiwa nchini, ujumbe huo umepanga kukutana na Viongozi mbalimbali wakiwemo;  Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Waziri wa Kilimo, Waziri wa Mazingira (Ofisi ya Makamu wa Rais), Uongozi wa kituo cha Uwekezaji (TIC), Bodi ya Sukari pamoja na kuonana na Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Pichani, ni Balozi Jhumun (kushoto) na Bwana Gansam Boodram (kulia) , CEO wa Mauritius Sugar Board, pamoja Mhe. Balozi Ramadhan Mwinyi (kati) ambaye ni Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushikiano wa Afrika Mashariki

Aidha, Ujumbe huo unategemea kutembelea maeneo mbalimbali, ikiwemo mkoa wa Pwani, Wilaya ya Rufiji kwa ajili ya kuangalia maeneo ambayo wanategemea kuanza awamu ya kwanza ya uanzishaji wa kiwanda kikubwa cha kuzalisha sukari ambacho kinategemea zaidi ya wananchi 6000. 
Awamu ya pili ya Mradi huo (baada ya miaka mitano) inategemewa kufanyika Mkoani Kigoma ambapo sukari itakayozalishwa pia itasafirishwa na kuuzwa katika nchi za jirani.

Ziara hii inafuatia ombi la Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli alilotoa (mwezi Marchi, 2017) kwa Mhe. Balozi Jhumun kumtaka kusaidia kuleta wawekezaji watakaoanzisha Viwanda vya sukari hapa nchini, wakati Balozi huyo akiwasilisha Hati za Utambulisho, Ikulu Dar es Salaam.
Kaimu Katibu Mkuu Mhe Balozi. Ramadhan Mwinyi akikaribisha wageni hao.


Pichani ni Wajumbe wa Kituo cha Uwekezaji (TIC), pamoja na Balozi Jhumun akiwa na Bw. Boodram kutoka Mauritius (kulia, mwisho).