Tuesday, August 20, 2019

MAAZIMIO YA MKUTANO WA 39 WA WAKUU WA NCHI WA SADAC


COMMUNIQUE OF THE 
39TH SADC SUMMIT OF HEADS OF STATE AND GOVERNMENT 
JULIUS NYERERE INTERNATIONAL CONVENTION CENTRE 
DAR ES SALAAM, UNITED REPUBLIC OF TANZANIA 
17 – 18 AUGUST 2019 
1. The 39th Ordinary Summit of the Heads of State and Government of the Southern African Development Community (SADC) was held at Julius Nyerere International Convention Centre in Dar es Salaam, United Republic of Tanzania, on the 17th and 18th August 2019. 

2. Summit was attended by the following Heads of State and Government and/or their representatives: 

Angola:                                      H.E. President João Manuel Gonçalves Lourenço 
Comoros:                                   H. E. President Colonel Azali Assoumani 
DRC:                                          H.E. President Félix Antoine Tshisekedi Tshilombo 
Madagascar:                              H.E. President Andry Rajoelina 
Mozambique:                             H.E President Felipe Jacinto Nyusi 
Namibia:                                    H.E. President Dr Hage G. Geingob 
Seychelles:                                H.E. President Danny Faure 
South Africa:                              H.E. President Cyril Ramaphosa 
United Republic of Tanzania:     H.E. President Dr. John Pombe Joseph Magufuli 
Zambia:                                      H.E. President Edgar Chagwa Lungu 
Zimbabwe:                                 H.E. President Emmerson Dambudzo Mnangagwa. 
Lesotho:                                    Right Hon Prime Minister Dr. Motsoahae Thomas Thabane 
Malawi:                                      Rt. Hon. Everton Herbet Chimulirenji – Vice President 
Eswatini:                                   H.E. The Right Hon. Prime Minister Mandvulo Dlamini 
Botswana:                                 Hon. Dr. Unity Dow – Minister of International Affairs and Cooperation 
Mauritius:                                 Hon. Nandcoomar Bodha – Minister of Foreign Affairs, Regional Integration and International Trade.

Monday, August 19, 2019

MABALOZI WA TANZANIA WATEMBELEA MIRADI YA MAENDELEO ZANZIBAR

Balozi Ramadhani Mwinyi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, (katikati; ambaye pia aliongoza ujumbe wa mabalozi katika ziara) akitoa maelezo kwa Mabalozi waliopotembelea mradi wa ujenzi wa jengo la makazi na biashara (Shopping mall) unaotekelezwa  na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Jumla ya mabalozi 42 wanaoiwakilisha Tanzania maeneo mbalimbali Duniani wapo nchini, ambapo pamoja na mambo mengine wametembelea miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali.

Wakiwa Zanzibar Mambalozi wametembelea mradi wa ujenzi wa jengo la biashara na makazi (shopping mall), uwanja mpya wa ndege (terminal 3), ujenzi wa mradi wa nyumba za makazi Fumba, ujenzi wa mradi wa barabara ya kilomita 31 (Kitope hadi Mkokotoni) na ujenzi wa bandari ya mafuta iliyopo eneo la Mnangapwani.

Mabalozi wamendelea kuridhishwa na kufahishwa na namna Serikali zote mbili (Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Muungano) zilivyo jidhatiti kutekeleza miradi mikubwa ambayo itachagiza kasi ya ukuaji wa uchumi na kuboresha maisha ya wananchi. 
Mabalozi wakisikiliza maelezo kuhusu mradi wa ujenzi wa jengo la makazi na biashara (Shopping mall) lililopo eneo la Mapinduzi square, Michenzani  kutoka kwa mtaalam na msimamizi wa mradi huo
Mabalozi wakitembelea maeneo mbalimbali yanayouzunguka maradi kuona shughuli zinazondelea katika eneo hilo
Mabalozi wakiwasili katika jengo la Makubusho ya Kumbukumbu ya Mapinduzi ya Zanzibar lililopo eneo la Michenzani, ambapo walipata fursa ya kufahamu kwa undani historia na taarifa mbalimbali kuhusu  Mapinduzi ya Zanzibar
Mabalozi wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watendaji wa Jengo la Makumbusho ya Kumbukumbu ya Mapinduzi na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki walipotembelea jengo hilo Agosti 19, 2019. 
Balozi Ramadhani Mwinyi Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akisalimiana na wafanyakazi wa mradi wa ujenzi wa uwanja mpya wa ndege wa Zanzibar, alipoongoza ujumbe wa mabalozi katika ziara ya mradi huo Agosti 19, 2019.
Mabalozi wakisiliza maelezo kuhusu ujenzi wa uwanja mpya wa ndege Zanzibar (Tereminal 3), kutoka kwa Mratibu wa Mradi huo Bw. Yasiri Costa.


Mabalozi wakiwasili eneo la mradi wa ujenzi wa barabara ya Kitope hadi Mkokotoni katika kiwango cha lami yenye urefu wa kilomita 31. Barabara hiyo hadi kukamilika kwake itagharimu jumla ya shilingi za Bilioni 58.6
Mabalozi wakiwa Wameambatana na watumishi wa Wizara wakitembelea eneo la mradi wa ujenzi wa barabara
Ujenzi wa daraja ukiendelea katika barabara ya Kitope-Mkokotoni
Mabalozi wakiwa eneo la ujenzi wa bandari ya mafuta iliyopo Mnangapwani walipotembele eneo la mradi huo Agosti 19, 2019.

Sunday, August 18, 2019

Naibu Waziri akutana na kufanya Mazungumzo na Balozi wa Umoja wa Ulaya, nchini Botswana


Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akisalimiana na Mhe.Jan SADEK Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini Botswana walipokutana kwa mazungumzo jijini Dar es Salaam.

Mazungumzo baina yao yalijikita kwenye masuala mbalimbali yaliyojadiliwa kwenye Mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).

Sambamba na hayo katika mazungumzo hayo Dkt. Ndumbaro aliendelea kumueleza Balozi Jan, juu ya umuhimu wa Umoja wa Ulaya kutekeleka wito alioutoa Mhe. Rais Magufuli wakati wa Mkutano wa SADC  kuhusu  kuiondolea nchi ya Zimbabwe vikwazo vya kiuchumi. Balozi Jan alikuwa nchini kuhudhuria Mkutano wa SADC
Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akizungumza alipokutana kwa mazungumzo na Balozi  Jan.
Mazungumzo yakiendelea
Mhe. Dkt. Ndumbaro akimsikiliza Balozi Jan walipokuna kwa mazungumzo jijini Dar es Salaam
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Ndumbaro akisisitiza jambo alipokutana kwa mazungumzo na Balozi Jan.

Saturday, August 17, 2019

MKUTANO WA 39 WA WAKUU WA NCHI NA SERIKALI WA JUMUIYA YA MAENDELEO KUSINI MWA AFRIKA (SADC)


Baadhi ya Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) wakiwa Katika Mkutano wa 39 wa Jumuiya hiyo unaofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JINCC) Dar es Salaam,Tanzania. 

Marais Wastaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakiwa waafuatilia Mkutano wa 9 wa Jumuiya hiyo unaofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JINCC) Dar es Salaam,Tanzania.
Kutoka kulia ni Rais Mstaafu wa awamu ya Pili Alhaji Ali Hassani Mwinyi,akifuatiwa na Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Mhe. Benjamini William Mkapa akifuatiwa na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete.

Marais Wastaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi,Zanzibar wakiwa wakifuatilia Mkutano wa 9 wa Jumuiya hiyo unaofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JINCC) Dar es Salaam,Tanzania. 
Kutoka kulia ni Rais Mstaafu wa awamu ya Pili Alhaji Ali Hassani Mwinyi,akifuatiwa na Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Mhe. Benjamini William Mkapa akifuatiwa na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Mstaafu wa awamu ya sita wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Aman Abeid Karume

Marais Wastaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi,Zanzibar pamoja na viongozi mbalimbali wa serikali wakifuatilia Mkutano wa 9 wa Jumuiya hiyo unaofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JINCC) Dar es Salaam,Tanzania. 
Kutoka kulia ni Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Mhe. Benjamini William Mkapa akifuatiwa na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akifuatiwa na  Rais Mstaafu wa awamu ya sita wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Aman Abeid Karume,akifuatiwa na Makamu wa Rais mstaafu wa awamu ya tatu Dkt Mohamed Gharib Bilali,akifuatiwa na Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi John Kijazi na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungao wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan,akiwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaji Dkt. Ali Mohamed Shein (katikati) na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa,wakiwa wanafuatilia Mkutano wa 39 wa wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) unaoendelea jijini Dar Es Salaam,Katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere(JNICC)

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungao wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan,akiwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaji Dkt. Ali Mohamed Shein (katikati) akifuatiwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi wakiwa wanafuatilia Mkutano wa 39 wa wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) unaoendelea jijini Dar Es Salaam,Katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere(JNICC)

Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. David Cleopa Msuya (wa kwanza kushoto) akifuatiwa na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. John Samuel Malecela (katikati) na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. faraji Kassidi Mnyepe wakifuatilia Mkutano wa 39 wa wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) unaoendelea jijini Dar Es Salaam,Katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere(JNICC)

Sehemu ya wahudhuriaji wa Mkutano wa 39 Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika wakifuatilia Mkutano wa 39 wa wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) unaoendelea jijini Dar Es Salaam,Katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere(JNICC)
Sehemu ya wahudhuriaji wa Mkutano wa 39 Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika wakiwa wamesimama kuimba wimbo wa Taifa wa Tanzania wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 39 wa wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) unaoendelea jijini Dar Es Salaam,Katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere(JNICC)

Mkutano wa 39 wa Wakuu wa nchi na Serikali wa nchi za SADC wafunguliwa rasmi

Wakuu wa nchi na Serikali wa nchi wanachama wa  Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) pamoja wa wajumbe mbalimbali waliohudhuria ufunguzi wa Mkutano wa 39 wa Kilele wa Wakuu hao wakiwa wamesimama wakati wimbo wa Taifa na Jumuiya ukipigwa. Mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.

Pamoja na mambo mengine yaliyojiri katika mkutano huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amekabidhiwa nafasi ya uenyekiti wa Jumuiya hiyo ambapo atahudumu kwa kipindi cha mwaka mmoja 2019/ 2020

Mkutano huu unaofanyika kwa siku mbili utafikia tamati kesho tarehe 17 Agosti, 2019
Wakuu wa nchi na Serikali wa nchi wanachama wa SADC wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya Mkutano wa ufunguzi uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaa 
Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akikabidhiwa uenyekiti na mwenyekiti anayemaliza muda wake Mhe. Hage Geingob Rais wa Namibia, wakati ufunguzi wa Mkutano wa kilele wakawaida wa Wakuu wa nchi na Serikali wa nchi za SADC uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akifuatilia tukio hilo.
Dkt. Stregomena Tax Katibu Mtendaji wa SADC, akihutubia wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa nchi za SADC 
Wakuu wa nchi na Serikali wa nchi wanachama wa SADC wakiwa wamesimama wakati wimbo wa Taifa na SADC ukiwa unapigwa kabla ya kuanza kwa Mkutano
Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akifuatilia Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa nchi wanachama za SADC uliokuwa ukiendelea
Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akifuatilia Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa nchi wanachama za SADC uliokuwa ukiendelea
Baadhi ya Mambalozi wa Tanzania wanaoiwakilisha nchi sehemu mbalimbali  wakifurahia jambo wakati wa Mkutano uliokuwa ukiendelea wa Wakuu wa nchi na Serikali wa nchi wanachama za SADC
Sehemu nyingine ya Mabalozi wa Tanzania wakifuatilia Mkutano

Mabalozi wa Tanzania wahitimisha ziara ya miradi maendeleo


Mabalozi wa Tanzania wanaoiwakilisha nchi sehemu mbalimbali duniani wakiwa Makao Makuu  ya Kampuni ya Taifa Gas iliyopo Kigamboni, Dar es Salaam  walipoitembelea kampuni hiyo kwa lengo la kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na Kampuni hiyo.

Maeneo mengine ambayo Mabalozi  wametembelea ni pamoja na Uwanja mpya ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (Teminal 3) mradi wa ujenzi wa barabara za juu za Ubungo (Ubungo interchange), Mamlaka ya Usimamizi wa Mawasiliano Tanzania (TCRA)  na Ujenzi wa mradi wa dajara jipya la surrender.
Mabalozi wakisikiliza ufanunuzi wa masuala mbalimbali kutoka kwa watendaji wa Kampuni ya Taifa Gas walipoitembela Makao Makuu ya Kampuni hiyo. 
Mhe. Baraka Luvanda Balozi wa Tanzania nchini India (Wakwanza kulia) na Mhe. Matilda Masuka Balozi wa Tanzania Jamhuri ya Korea wakifuatilia hotuba fupi ya ukaribisho.
Tokea kulia: Mhe. Asharose Migiro Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mhe. Dkt. Wilbroad Slaa Balozi Tanzania nchini Sweden, Mhe. Dkt. Pindi Chana Balozi wa Tanzania nchini Kenya, na Mhe. Wilson Masilingi Balozi wa Tanzania Washngton DC wakifuatila hotuba ya ukaribisho ya Taifa Gas, Dar es Salaam 
Mabalozi wakiwa Uwanja Mpya wa Ndege wa Julius Nyerere (Terminal 3) walipotembelea kuona ufanisi wa uwanja huo.  
Mabalozi wakisikiliza ufafanuzi kutoka kwa mtaalam walipotembelea eneo la ujenzi wa barabara za juu eneo la Ubungo, Dar es Salaam
Balozi Ramadhani Mwinyi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki  akisalimiana na Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano alipowasili Makao Makuu ya TCRA akiwa ameambatana na ujumbe wa Mabalozi
Mabalozi wakiwa katika picha ya pamoja na watendaji wa TCRA walipotembelea Makao makuu ya Ofisi hiyo

Friday, August 16, 2019

Rais Ramaphosa aitembelea kambi ya Wapigania uhuru wa Afrika Kusini iliyopo Mazimbu, Morogoro

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa ameongozana na Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini, Mhe. Cyril Ramaphosa pamoja na mkewe mara baada ya kuwapokea walipotembelea iliyokuwa Kambi ya Wapigania uhuru dhidi ya ubaguzi wa rangi kutoka Afrika Kusini iliyopo Mazimbu mkoani Morogoro. Kambi hiyo ni maarufu kwa jina la Solomon Mahlangu mmoja wa wapigaia uhuru aliyewahi kuishi kwenye kambi hiyo. Ziara ya Mhe. Rais Ramaphosa imefanyika tarehe 16 Agosti 2019
Mhe. Rais Ramaphosa akizungumza wakati alipotembelea kambi za wapigaia uhuru kutoka Afrika Kusini zilizopo Mazimbu mkoani Morogoro. Katika hotuba yake alitoa shukrani kwa Watanzania hususan wakazi wa eneo hilo kwa mchango mkubwa walioutoa ikiwemo kutoa eneo na kuwahifadhi wapigania uhuru wa nchi hiyo ambapo alisema amefarijika kukanyaga ardhi hiyo yenye historia kubwa ya ushirikiano wa kindugu kati ya Tanzania na Afrika Kusini. Pia aliahidi kuhakikisha nchi yake inaimarisha soko la mazao mbalimbali kutoka Morogoro na pia kuifanya kambi hiyo kuwa kituo kikubwa cha utalii.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza wakati wa ziara ya Mhe. Rais Ramaphosa iliyofanyika kwenye kambi ya wapigania uhuru wa Afrika Kusini iliyopo Mazimbu mkoani Morogoro. Mhe. Waziri Mkuu alisistiza nchi hizo kuimarisha ushirikiano  wa kihistoria uliopo kati ya Tanzania na Afrika Kusini
Mhe. Prof. Kabudi naye akizungumza wakati wa ziara ya Rais wa Afrika Kusini mkoani Morogoro
Sehemu ya wadau mbalimbali wakifuatilia hotuba za viongozi

Sehemu nyingine ya wananchi waliojitokeza kwenye ziara ya Mhe. Rais Ramaphosa mkoani Morogoro

Msemaji wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi akiwa na Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiabo wa Afrika Mashariki, Bw. Emmanuel Buhohela wakati wa ziara ya Rais wa Afrika Kusini kwenye kambi za wapigania uhuru kutoka Afrika Kusini zilizopo Mazimbu mkoani Morogoro

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika  Mashariki, Bw. Wilbroad Kayombo (katikati) akishiriki na wadau wengine ziara ya Rais wa Afrika Kusini alipotembelea mkoani Morogoro
Wageni waalikwa

Mhe. Waziri Mkuu akimkabidhi zawadi Mhe. Rais Ramaphosa
Mhe. Rais Ramaphosa akiwa ameongozana na Mhe. Waziri Mkuu wakipita kwenye makaburi ya wapigania uhuru kutoka Afrika Kusini yaliyopo Mazimbu, Morogoro
Mhe. Rais Ramaphosa akimsikiliza mmoja wa watoto wa wapigania uhuru aliyezikwa kwenye eneo hilo

Mhe. Rais Ramaphosa akipanda mti wa kumbukumbu mara baada ya kumaliza ziara yake kwenye kambi ya wapigania uhuru kutoka nchini kwake iliyopo Mazimbu, Morogoro

Mhe. Rais Ramaphosa aliumwagia maji mti huo mara baada ya kuupanda

Mhe. Rais Ramaphosa akiweka shada la maua kuwakumbuka wapigania uhuru wa Afrika Kusini waliokufa wakiwa kwenye harakati za kuiokomboa nchi hiyo dhidi ya ubaguzi wa rangi 

Mhe. Rais Ramaphosa akiwaaga wananchi waliojitokeza kwenye ziara yake alipotembelea kambi ya wapigania uhuru wa Afrika Kusini iliyopo Mazimbu, Morogoro