Wednesday, August 9, 2023

DKT. TAX ATEMBELEA AICC ARUSHA AZUNGUMZA NA BODI NA WATUMISHI , NA KUZURU CHUMBA CHA ICTR

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax akipokea shada la maua alipowasili katika Ofisi za Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC) jijini Arusha

Watumishi wa AICC wakiongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya AICC Balozi Ole Njolay na Mkurugenzi Mtendaji wa AICC wakimpokea Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax alipowasili katika Ofisi zao jijini Arusha kuwatembelea.

 Mkurugenzi Mtendaji wa AICC Bw. Emphraim Mafuru ( wa pili kulia) akitoa maelezo kwa  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax alipowasili katika Hospitali za AICC jijini Arusha


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax amembeba Mtoto wa kiume aliyezaliwa leo (tarehe 09 Agosti  2023)  katika Hospitali ya AICC alipotembelea hospitali hiyo ikiwa ni sehemu ya ziara yake katika Kituo cha AICC   jijini Arusha


 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax akisaini kitabu cha wageni  kwenye Chumba cha iliyokuwa Mahakama ya Kimatifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR) iliyokuwa ikiendesha shughuli zake katika jengo la AICC  jijini Arushaalipozuru chumba hicho



 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax katika picha ya pamoja na Bodi ya Wakurugenzi ya Kituo cha AICC alipotembelea eneo ambalo kitajengwa Kituo kipya cha Mikutano cha Kimatifa cha Mlima Kilimanjari (MKICC) alipotembelea Ofisi AICC  jijini Arusha


Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya AICC Balozi Daniel Ole Njolay na Mkurugenzi Mtendaji wa AICC Bw. Ephraim Mafuru wakiwa na  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax aliangalia kumbi mpya za mikutano zilizoongezwa katika Kituo hicho




Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax akizungumza na wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kituo cha AICC alipotembelea kituo hicho jijini Arusha


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax akizungumza na watumishi wa AICC jijini Arusha alipotembelea Ofisi za kituo hicho jijini Arusha

Watumishi wa AICC wakimsikiliza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax alipozungumza nao katika ofisi zao jijini Arusha

Watumishi wa AICC wakimsikiliza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax alipozungumza nao katika ofisi zao jijini Arusha

Watumishi wa AICC wakimsikiliza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax alipozungumza nao katika ofisi zao jijini Arusha

mwakilishi wa Watumishi wa AICC Bi. Catherine Kilinda akimkabidhi zawadi Mkurugenzi wa AICC tayari kumkabidhi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax alipotembelea ofisi za AICC na kuzungumza nao katika ofisi zao jijini Arusha


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax akionesha zawadi aliyopewa na watumishi wa AICC alipotembelea ofisi za AICC na kuzungumza na watumishi wa AICC katika ofisi zao jijini Arusha




Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax katika picha ya pamoja na watumishi wa AICC alipotembelea ofisi za AICC jijini Arusha


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb) atembelea ofisi za Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC) kujionea utendaji kazi wa taasisi hiyo na kupanga kwa pamoja jinsi ya kutekeleza majukumu ya AICC kwa mwaka huu wa fedha na kuleta tija kwa Taifa.

 

Mhe Waziri katika ziara hiyo amezuru Chumba cha iliyokuwa Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR) iliyokuwa ikiendesha shughuli zake katika jingo la AICC , hospitali ya AICC, eneo litakalojengwa Kituo kipya cha Mikutano cha Kimataifa cha Mlima Kilimanjaro (MKICC)  na kuzungumza na wajumbe wa bodi, menejimenti na watumishi wa AICC.

 

Akizungumza na watumishi hao Mhe. Dkt. Tax amewataka kuhakikisha huduma wanazotoa zinaendana na mahitaji ya wakati uliopo ili kuhimili ushindani wa soko la biashara ya utalii wa mikutano na kuiwezesha taasisi yao kupata mikutano mingi zaidi.

 

Mhe. Waziri pia amewapongeza watumishi hao kwa kazi nzuri wanayofanya ya kuitangaza nchi pale wanapotokea kuandaa mikutano ya Kimataifa kama ilivyotokea kwa mkutano uliofanyika nchini hivi karibuni wa Wakuu wa Nchi za Afrika uliojadili rasilimali watu.

Katika ziara hiyo Dkt. Tax aliambatana na Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa AICC walioongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Balozi Daniel Ole Njolay na Mkurugenzi Mtendaji wa AICC, Bw. Ephraim Mafuru. 

Mhe. Dkt. Tax amefanya ziara ya siku moja ya kutembelea AICC kwa ajili ya kujadiliana nao na kuona ni jinsi gani wanaendana na mikakatiitakyoiwezesha AICC kuendelea kuwa Kituo bora cha Mkitano katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Ziara hii ni ya kwanza kwa Mhe Waziri tangu ateuliwa kushika wadhifa wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki mwezi Oktoba 2022

Kituo cha AICC ni moja ya taasisi zilizo chini ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Taasisi nyingine ni Chuo cha Diplomasia Dar es Salaam (CFR) pamoja na Mpango wa Hiari wa Kujitathmini wa Afrika (APRM).

DKT. SHELUKINDO AKUTANA KWA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA VIETNAM

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo amekutana kwa mazungumzo na Balozi wa Vietnam, nchini Mhe. Nguyen Nam Tien katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Viongozi hao wamejadili masuala mbalimbali ya ushirikiano ikiwemo maandalizi ya Mkutano wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kwa lengo la kuimarisha ushirikiano katika sekta za kipaumbele hususan utalii, kilimo, afya, TEHAMA, biashara na uwekezaji, uchumi wa buluu na maeneo mengine.

“Vietnam itaendelea kushirikiana na wafanyabiashara wa Tanzania katika kuhakikisha wanapata fursa ya kujifunza na kubadilishana uzoefu wa kibiashara nchini Vietnam ili kukuza ushirikiano wa biashara na uwekezaji,” amesema Balozi Tien. 

Pamoja na mambo mengine, Balozi Tien amesifu uhusiano mzuri na wa muda mrefu uliopo kati ya Tanzania na Viet Nam. Pia, ameeleza kuwa Vietnam inafurahishwa na Uongozi imara wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Shelukindo amesema kwamba Tanzania inajivunia kuwa na uhusiano imara na Vietnam uliodumu kwa zaidi ya miaka 60. 

Dkt. Shelukindo amezialika kampuni kutoka Vietnam kuja kuwekeza nchini katika miradi ya kimkakati kwa maslahi ya pande zote mbili. “Nawaalika wafanyabiashara na wewekezaji wa Vietnam kuja kuwekeza Tanzania kwa kuwa Serikali imeboresha mazingira ya biashara na uwekezaji.” amesema Dkt. Shelukindo.

Dkt. Shelukindo ameongeza kuwa Vietnam imechangia vyema katika kukuza sekta ya mawasiliano kupitia Kampuni ya Halotel ambayo imetoa ajira kwa Watanzania. 

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo akisalimiana na Balozi wa Vietnam, nchini Mhe. Nguyen Nam Tien katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Balozi wa Vietnam, nchini Mhe. Nguyen Nam Tien akifafanua jambo kwa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo walipokutana kwa mazungumzo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam 

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo akizungumza na Balozi wa Vietnam, nchini Mhe. Nguyen Nam Tien katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam 







Tuesday, August 8, 2023

MKUTANO WA WAKUU WA NCHI NA SERIKALI WA SADC NGAZI YA WATAALAMU WAANZA NCHINI ANGOLA

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Bi. Amina Shaban (mwenye mtandio) akiwa na ujumbe wa Tanzania unaoshiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ulioanza leo katika ngazi ya maafisa waandamizi jijini Luanda, Angola.
Mwenyekiti wa ngazi ya maafisa waandamizi aliyemaliza muda wake ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Ushirikiano wa Kikanda wa DRC, Balozi Songhu Kayumba (kulia) akikabidhi uenyekiti kwa Mwenyekiti mpya wa maafisa waandamizi kutoka Angola, Balozi Nazare Salvador ambaye ni Mkurugenzi wa Ofisi ya SADC nchini Angola katika Wizara ya Uhusiano wa Nje ya nchi hiyo.


Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ngazi ya maafisa waandamizi ukiendelea jijini Luanda, Angola.



Monday, August 7, 2023

WAZIRI TAX APOKEA HATI ZA UTAMBULISHO ZA MWAKILISHI MKAZI WA UNICEF, AMUAGA MWAKILISHI MKAZI UNDP

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) amepokea Hati za Utambulisho za Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto (UNICEF) nchini Tanzania, Bi. Elke Wisch katika ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Waziri Tax amemweleza Bi. Elke Wisch kuwa UNICEF imekuwa na mchango mkubwa kuiunga mkono Serikali kwa kukuza, kulinda na kutimiza haki za watoto. 

“UNICEF ni wadau wakubwa na wamekuwa wakishirikiana na Serikali katika maeneno mengi………..na madhumuni yake ni kulinda haki ya mtoto na katika hili ni wadau wetu katika sekta za afya na elimu pamoja kuangalia maendeleo ya watoto,” amesema Dkt. Tax.

Waziri Tax ameongeza kuwa UNICEF wamekuwa pia wakisaidia katika kuhakikisha vifo vya watoto wadogo nchini vinapungua na wamekuwa na msaada mkubwa katika hilo.

Kwa upande wake Mwakilishi Mkazi UNICEF nchini, Bi. Elke Wisch amesema kuwa UNICEF itaendelea kutekeleza majukumu yake kwa kushirikiana na Serikali ili kuhakikisha kuwa haki za watoto zinalindwa na kuimarishwa kuanzia katika ngazi ya jamii na Tanzania nzima kwa ujumla.

 “UNICEF tunaahidi kuendelea kushirikiana na Serikali kuhakikisha kuwa haki za watoto zinalindwa na kuimarishwa kuanzia katika ngazi ya jamii na Tanzania nzima kwa ujumla.” amesema Bi. Wisch

Aidha, Bi Wisch ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa kufanikisha vizuri Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Rasilimali watu (Africa Heads of States Human Capital Summit) ulifanyika mwezi Julai. Ambapo amesema mkutano huo ulikuwa njia sahihi ya kujadili misingi ya ushirikiano pamoja na masuala mbalilmbali ya Watoto na vijana ambao ndiyo rasimali za kukuza na kuendeleza maendelea ya nchi.

 Katika tukio jingine, Waziri Tax amemuaga Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP), Bi. Christine Musisi baada ya kumaliza muda wake wa uwakilishi nchini.

Bi. Musisi amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa ambayo amekuwa akiifanya tangu alipoinga madarakani licha ya kuingia madarakani katika kipindi kigumu cha janga la Uviko 19.

“Nimekuwa na wakati mzuri kuona nchi ikikuwa, ikiwa na ustahimilivu hata katika kipindi cha janga la Uviko 19, nimeona pia maendeleo ya watu yakiwa imara kutokana na uongozi thabiti wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuhakikisha kuwa wananchi wa Tanzania wanalindwa,” alisema Bi. Musisi

Bi. Musisi ameongeza kuwa ilikuwa faraja kubwa kufanya kazi Tanzania kama mwakilishi mkazi wa UNDP ambapo alishirikiana vyema na Serikali katika kuhakikisha kuwa mpango wa maendeleo wa miaka mitano na malengo ya milenia yanatekelezwa na kutimia kama ilivyopangwa.



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akipokea Hati za Utambulisho za Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto (UNICEF) nchini Tanzania, Bi. Elke Wisch katika ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akizungumza na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP), Bi. Christine Musisi katika ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam. Bi Musisi amemuaga Dkt. Tax baada ya kumaliza muda wake wa uwakilishi nchini.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akimkabidhi zawadi ya picha Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP), Bi. Christine Musisi katika ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaamb baada ya kumaliza muda wake wa uwakilishi nchini






Thursday, August 3, 2023

WAZIRI TAX AFANYA MAZUNGUMZO NA SPIKA WA BUNGE LA ALGERIA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax amefanya mazungumzo na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Algeria, Mhe. Brahim Boughali alipomtembelea katika Ofisi za Bunge tarehe 2 Agosti 2023 jijini Algiers, Algeria.

Katika mazungumzo yao Waziri Tax alieleza kuwa uhusiano kati ya Tanzania  na Algeria ni wa kirafiki na kindugu tangu enzi za kupigania ukombozi wa bara la Afrika. 

Pia kupitia ziara yake ya kikazi nchini humo pamoja na kuhuishwa kwa maeneo ya ushirikiano katika Mkutano wa Tano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Algeria ni wazi kwamba nchi zetu zimejidhatiti kupiga hatua za kimaendeleo katika ushirikiano uliopo.

 ‘’Kuhitimishwa kwa mkutano  wa JPC kwa mafanikio ni hatua muhimu katika kuendelea kuimarisha ushirikiano wetu kwenye sekta za kiuchumi kwa maslahi ya pande zote’’ alisema Dkt. Tax.

Naye Spika wa Bunge la Algeria, Mhe. Brahim Boughali ameeleza kuwa Serikali ya Algeria ipo tayari kushirikiana katika masuala mbalimbali ya kibunge ili kwa pamoja tuweza kutatua changamoto mbalimbali zinazoendelea duniani.

‘’ Ni vema Bunge la Tanzania na la Algeria tukajenga mfumo rasmi wa ushirikiano ili kuweka utaratibu rasmi wa kushirikishana katika masuala mbalimbali ya kitaifa, kikanda na dunia kwa ujumla,’’ alisema Mhe. Boughali.

Aidha, Mhe. Spika Boughali amemhakikishia Mhe. Waziri Tax kuwa kwenye Kikao cha Bunge la Algeria la mwezi Septemba, suala la ushirikiano na Tanzania litakuwa ni moja ya eneo la  Kipaumbele katika mijadala ya Bunge hilo.

===================================


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax amefanya mazungumzo na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Algeria, Mhe. Brahim Boughali alipomtembelea katika ofisi za Bunge jijini Algiers, Algeria tarehe 2 Agosti 2023

Mazungumzo yakiendelea.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Stergomena Tax akiwasili katika Ofisi za Bunge la Algeria jijini Algiers.

Picha ya pamoja


TANZANIA YAFANYA UFUNGUZI RASMI WA UBALOZI JIJINI ALGIERS, ALGERIA

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imefanya ufunguzi rasmi wa Ubalozi wake jijini Algiers, Algeria tarehe 2 Agosti 2023.

Ufunguzi huo umefanywa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb) na kuhudhuriwa na mwenyeji wake Waziri wa Mambo ya Nje na Diaspora wa Algeria, Mhe. Ahmed Attaf,  Balozi wa kwanza wa Algeria kuhudumu nchini Tanzania, Balozi Noureddine Djoudi na Jumuiya ya Wanadiplomasia nchini Algeria.

Viongozi wengine waliohudhuria ufunguzi huo ni Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo, Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Dkt. Seif Shekalaghe, Naibu Makatibu Wakuu kutoka Wizara za Elimu, Sayansi na Teknolojia, Nishati na Mambo ya Ndani ya Nchi.

Akihutubia kwenye ufunguzi wa Ubalozi huo Waziri Tax ameeleza kuwa Tanzania na Algeria zimejidhatiti kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia kwa lengo la kukuza ushirikiano wenye maslahi kupitia sekta za kipaumbele.

‘’Ni imani yangu kuwa Ubalozi huu utaendelea kuwa kiunganishi kati ya serikali zetu kwa kutoa huduma za kidiplomasia, kuhudumia Watanzania” alisema Dkt. Tax

Naye Mhe. Attaf ameeleza kuwa ziara ya Waziri Tax imekuwa na mafanikio makubwa kwa kuwa wamepata fursa ya kuzungumza masuala ya ushirikiano katika sekta za biashara, uwekezaji na sekta nyingine muhimu kwa maendeleo ya mataifa hayo mawili.

‘’Balozi zetu zitaendelea kutekeleza majukumu yake ya msingi ili nia ya dhati ya kuimarisha na kukuza uhusiano iweze kuleta tija zaidi na kuziwezesha nchi zetu kunufaika kiuchumi,’’ alisema Mhe. Attaf.

Ufunguzi wa Ubalozi umefanyika pembezoni mwa Mkutano wa Tano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Algeria ambao umemalizika kwa mafanikio na kuwezesha kusainiwa kwa Hati 8 za Makubaliano ya Ushirikiano katika sekta za nishati, mafuta na gesi, elimu na teknolojia, mafunzo ya diplomasia, kumbukumbu na nyaraka, ulinzi na usalama, ushirikiano wa kidiplomasia, kilimo na afya. 

Uhusiano kati ya Algeria na Tanzania uliasisiwa mwaka 1963 mara baada ya uhuru wa Tanganyika. Tangu wakati huo nchi hizi zimeendelea kushirikiana katika maeneo mbalimbali kwa maslahi ya pande zote. Vilevile katika kuimarisha ushirikiano huo Tanzania imefanya ufunguzi wa Ubalozi wake nchini Algeria ambao ulianza kutekeleza majukumu yake tangu mwaka 2017.

=====================================

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akikata utepe kuashiria ufunguzi wa ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Algeria tarehe 2 Agosti 2023 jijini Algiers. Kushoto ni Waziri wa Mambo ya Nje na Diaspora wa Algeria, Mhe. Ahmed Attaf na kulia ni Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Mej. Jen. (Mst) Jacob Kingu wakishuhudia ufunguzi huo.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax na Waziri wa Mambo ya Nje na Diaspora wa Algeria, Mhe. Ahmed Attaf wakiwa katika ufunguzi wa Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Algeria tarehe 2 Agosti 2023.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akipongezwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Diaspora wa Algeria, Mhe. Ahmed Attaf baada ya kukamilisha taratibu za ufunguzi wa Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Algeria tarehe 2 Agosti 2023.


Waziri wa Mambo ya Nje na Diaspora wa Algeria, Mhe. Ahmed Attaf akihutubia wakati wa hafla ya ufunguzi wa Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Algeria tarehe 2 Agosti 2023.

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo (mwenye tai ya bluu) akifatilia hotuba zilizowasilishwa na Mawaziri wa Mambo ya Nje, Mhe. Dkt. Tax na na Mhe. Attaf.


Kutoka Kushoto ni Mkurugenzi Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Naimi Aziz, Mkurugenzi Mkuu Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Diaspora ya Algeria, Balozi Selma Malika na Balozi Djoudi wakifatilia hafla ya ufunguzi huo.

Picha ya pamoja, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax na Waziri wa Mambo ya Nje na Diaspora wa Algeria, Mhe. Ahmed Attaf.

Picha ya Pamoja, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax, Waziri wa Mambo ya Nje na Diaspora wa Algeria, Mhe. Ahmed Attaf na Watumishi wa Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Algeria na ujumbe wa Tanzania katika mkutano wa Tano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Algeria.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akimkabidhi zawadi Balozi wa kwanza wa Algeria kuhudumu nchini Tanzania, Balozi Noureddine Djoudi wakati wa hafla ya ufunguzi wa Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Algeria.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akihutubia wakati wa hafla ya ufunguzi wa Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Algeria tarehe 2 Agosti 2023.

Wednesday, August 2, 2023

RAIS WA ALGERIA AKUTANA KWA MAZUNGUMZO NA WAZIRI TAX

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Algeria, Mhe. Abdelmadjid Tebboune amekutana Kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) alipomtembelea Ikulu Jijini Algiers, Algeria tarehe 1 Agosti 2023.

Mazungumzo hayo yamefanyika pembezoni mwa Mkutano wa Tano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Algeria unaofanyika kuanzia tarehe 30 Julai 2023 hadi 1 Agosti 2023. 

Mazungumzo ya viongozi hao yalijikita katika kuendelea kuimarisha ushirikiano wa kirafiki na kidiplomasia ili kuweza kutekeleza diplomasia ya uchumi kwa maslahi mapana ya nchi zao.

Aidha, katika kuendelea kuimarisha ushirikiano Waziri Tax pamoja na majukumu mengine, atazindua Ofisi za Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 2 Agosti 2023 Jijini Algiers.

Uzinduzi wa ubalozi huo, ni hatua muhimu hasa wakati huu ambapo viongozi hao wamekubaliana kuinua sekta za uchumi ambazo ni pamoja na biashara, uwekezaji, nishati, madini, elimu, sayansi na teknolojia, afya na utalii.

======================================

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Algeria, Mhe. Abdelmadjid Tebboune akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) alipomtembelea ofisini kwake Ikulu Jijini Algiers, Algeria tarehe 1 Agosti 2023.

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Algeria, Mhe. Abdelmadjid Tebboune akisalimiana na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Mej. Jen. (Mst) Jacob Kingu ambaye alifuatana na Waziri Tax Ikulu ya Algiers, Algeria tarehe 1 Agosti 2023.

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Algeria, Mhe. Abdelmadjid Tebboune akisalimiana na Balozi wa Algeria nchini Tanzania, Mhe. Ahmed Djellal baada ya kuwasili Ikulu Algiers, Algeria tarehe 1 Agosti 2023.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) akiongea mbele ya waandishi wa Habari katika Ikulu ya Algiers baada ya kumalizika kwa mazungumzo yake na Mheshimiwa Rais Abdelmadjid Tebboune Ikulu  Algiers, Algeria tarehe 1 Agosti 2023

Baada ya Kuwasili katika Ikulu ya Algiers, Algeria.


TANZANIA NA ALGERIA ZASAINI HATI 8 ZA MAKUBALIANO NA MIKATABA YA USHIRIKIANO

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Algeria zimesaini Hati 8 za Makubaliano ya Ushirikiano katika sekta za umeme, gesi, biashara, viwanda na kilimo, utamaduni na sanaa, kumbukumbu na nyaraka, mafunzo katika vyuo vya diplomasia na ushirikiano katika taaluma na teknolojia.

Utiaji saini wa makubaliano hayo umeshuhudia na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) na Waziri wa Mambo ya Nje na Diaspora wa Algeria wakati wa Mkutano wa Tano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Algeria.

Mkutano wa Mawaziri ulitanguliwa na Mkutano Ngazi ya Maafisa Waandamizi uliofanyika tarehe 30 hadi 31 Julai 2023.

Ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano huu umeongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax. Viongozi wengine waliohudhuria ni pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo, Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Dkt. Seif Shekalaghe na Naibu Makatibu Wakuu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mambo ya Ndani ya Nchi, na Nishati

Madhumuni ya mkutano huo ni kutathmini hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa masuala mbalimbali ya ushirikiano yaliyokubaliwa kwenye Mkutano wa Nne uliofanyika mwaka 2010 jijini Dar es Salaam.

Akihutubia wakati wa ufunguzi wa mkutano huo Waziri Tax ameleza kuwa mkutano huu ni kielezo cha dhamira ya dhati kati ya Tanzania na Algeria kuendelea kuimarisha ushirikiano uliopo na kuweka mfumo rasmi wa kujitathimini katika masuala mbalimbali yaliyokubalika.

‘’ Ni imani yangu kuwa wataalam wetu wamefanya kazi kubwa katika majadiliano kwa kuangalia maeneo muhimu na ya kipaumbele ili kuendelea kukuza ushirikiano kwa maslahi ya nchi zote mbili" alisema Dkt. Tax.

Naye Waziri wa Mambo ya Nje na Diaspora wa Algeria, Mhe. Ahmed Attaf katika hotuba yake ameeleza kuwa  mkutano huo umetoa fursa ya kujadili na kukubaliana maeneo ya kipaumbele kwa maslahi ya pande mbili. 

Pia ameeleza kuwa kusainiwa kwa makubaliano ni ishara ya wazi kuwa nchi hizi zitaendelea kudumisha uhusiano mzuri uliopo sanjari na kukuza ushirikiano kwenye maeneo mapya yenye tija. 

‘’Serikali ya Algeria itaendelea kushirikiana kwa karibu na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kufanya kazi pamoja ili kufikia malengo tuliyojiwekea katika sekta mahsusi za ushirikiano,’’ alisema Mhe. Attaf.


Mhe. Dkt. Tax na Mhe. Attaf wamewashukuru Wakuu wa Nchi wa pande zote mbili kwa utayari na jitihada zao wanazozifanya katika kuhakikisha ushirikiano uliopo unaimarishwa zaidi kwa maslahi mapana ya nchi mbili.

Mkutano huo umejadili na kutathimini utekelezaji wa maeneo ya ushirikiano katika Siasa na Diplomasia, Ulinzi na Usalama, Fedha na Uchumi, Nishati, Habari na Mawasiliano, Kilimo, Elimu na Mafunzo, Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Utalii, Kilimo na Uvuvi na Afya, na Sanaa na Utamaduni.

Katika kuendelea kuhakikisha kwamba Tanzania na Algeria  zinatekeleza maazimio ya mkutano husika, nchi hizi mbili zimekubaliana kuitisha mkutano wa sita utakaofanyika nchini Tanzania mwaka 2025.

====================================

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) akihutubia wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Tano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Algeria uliofanyika tarehe 30 Julai 2023 hadi 1 Agosti 2023 jijini Algiers, Algeria. Pembeni yake ni Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo. 

Waziri wa Mambo ya Nje na Diaspora wa Algeria, Mhe. Ahmed Attaf akihutubia wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Tano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Algeria uliofanyika tarehe 30 Julai 2023 hadi 1 Agosti 2023 jijini Algiers, Algeria.

Kulia ni Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Mej. Jen. (Mst) Jacob Kingu na Mkurugenzi Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Naimi Aziz wakifuatilia Mkutano wa Tano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Algeria uliofanyika tarehe 30 Julai 2023 hadi 1 Agosti 2023 jijini Algiers, Algeria.

Kutoka kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Dkt. Maduhu Kazi na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Bw. Athumani Mbuttuka wakifuatilia Mkutano wa Tano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Algeria uliofanyika tarehe 30 Julai 2023 hadi 1 Agosti 2023 jijini Algiers, Algeria.

Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. James Mdoe pamoja na viongozi wengine Waandamizi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakifuatilia Mkutano wa Tano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Algeria uliofanyika tarehe 30 Julai 2023 hadi 1 Agosti 2023 jijini Algiers, Algeria.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax na Waziri wa Mambo ya Nje na Diaspora wa Algeria, Mhe. Ahmed Attaf wakisaini Hati ya Makubaliano ya Ushirikiano katika mafunzo ya diplomasia kati ya Chuo cha Diplomasia cha Tanzania (CFR) na Chuo cha Diplomasia cha Algeria wakati wa Mkutano wa Tano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Algeria uliofanyika tarehe 30 Julai 2023 hadi 1 Agosti 2023 jijini Algiers, Algeria.
===========================

Matukio katika picha viongozi kutoka sekta za ushirikiano kati ya  Tanzania na Algeria wakisaini Hati za Makubaliano na Mikataba ya Ushirikiano wakati Mkutano
 wa Tano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Algeria uliofanyika tarehe 30 Julai 2023 hadi 1 Agosti 2023 jijini Algiers, Algeria.