Wednesday, May 8, 2024

BALOZI YAKUBU, TIC KUSHIRIKIANA KUVUTIA WAWEKEZAJI COMORO

 

Balozi wa Tanzania nchini Comoro Mhe.Said Yakubu akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC) Bw. Gilead Teri  alipowasilia katika ofisi za  TIC jijini Dar es Salaam.


Balozi wa Tanzania nchini Comoro Mhe.Said Yakubu akizungumza kitu alipomtembelea Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC) Bw. Gilead Teri  (hayupo pichani) katika ofisi za  TIC jijini Dar es Salaam.

Balozi wa Tanzania nchini Comoro Mhe.Said Yakubu (kushoto) akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC) Bw. Gilead Teri  (kulia) katika ofisi za  TIC jijini Dar es Salaam.

Mazungumzo yakiendelea. 
 Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC) Bw. Gilead Teri  (kulia) akimkabidhi Balozi wa Tanzania nchini Comoro Mhe.Said Yakubu (kushoto) machapicho mbalimbali yanayoelezea fursa za uwekezaji zinazopatikana nchini alipotembelea Ofisi za TIC jijini Dar es Salaam.

 




Balozi wa Tanzania nchini Comoro Mhe.Said Yakubu amekutana na kuzungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC) Bw. Gilead Teri  katika ofisi za  TIC jijini Dar es Salaam.
 
Katika mazungumzo hay,  Mhe. Balozi na Bw. Teri wamejadili  namna ya kukuza uwekezaji kati ya Tanzania na Comoro ambako Balozi huyo anaenda kuiwakilisha Tanzania.
 
Kupitia mazungumzo hayo TIC imeahidi kupeleka ujumbe wa kwanza wa wawekezaji angalau 20 mwishoni mwa mwezi Juni 2024 na itashirikiana na Taasisi za sekta binafsi kuandaa ziara za wawekezaji kila mwezi kati ya Julai na Disemba 2024 kuangalia sekta mbalimbali ikiweka kipaumbele katika sekta ya  uchukuzi, fedha, afya, utalii na ujenzi.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.