Saturday, May 18, 2024

MKUTANO WA 16 WA BARAZA LA KISEKTA LA MAWAZIRI WA FEDHA WA EAC WAFANYIKA ARUSHA

Mkutano wa 16 Wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Fedha na Uchumi (SCFEA) la Jumuiya ya Afrika Mashariki umefanyika Mei 17, 2024 jijini Arusha Tanzania. Mkutano huo ulitanguliwa na mikutano ya ngazi ya watalaam na Mkutano wa Makatibu Wakuu iliyofanyika kuanzia tarehe 13 hadi 16 Mei 2024.


Mkutano wa SCFCEA ulifanyika sambamba na mkutano wa Mashauriano ya Kibajeti wa Mawaziri wa Fedha na Uchumi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Arusha. Mwenyekiti wa Mkutano huo alikuwa Mhe. Mwigulu Nchemba (Mb.), Waziri wa Fedha wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

 

Ujumbe wa Tanzania uliongozwa na Mhe. Saadah Mkuya (Mb.), Waziri wa Nchi. Ofisi ya Rais Fedha na Mipango wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na kuhudhuriwa pia na Mhe. Stephen Byabato (Mb.), Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki.


Mkutano huo ulipokea na kujadili taarifa ya Utekelezaji wa maamuzi ya mkutano wa 15 wa (SCFEA) pamoja na masuala mbalimbali. Aidha, Nchi Wanachama ziliwasilisha Miongozo ya Bajeti kwa mwaka wa fedha 2024/2025, Kaulimbiu za bajeti kwa mwaka wa Fedha 2024/2025 ambapo Mkutano huo pia ulipitisha Kaulimbiu ya bajeti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa mwaka wa fedha 2024/2025 na kupitisha tarehe 13 Juni 2024 kuwa tarehe ya kusoma bajeti za nchi wanachama.


Vilevile, Mkutano huo ulipitisha Mkataba wa Kuondoa Utozaji Kodi Mara Mbili baina ya Nchi Wanachama na Mkataba Kifani wa Kuongoza Majadiliano baina ya Nchi za EAC na nchi nyingine



Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (katikati) akiongoza  Mkutano wa Mashauriano ya Kibajeti wa Mawaziri wa Fedha na Uchumi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki  uliofanyika sambasamba na  Mkutano wa 16 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Fedha na Uchumi (SCFEA) la Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika Mei 17, 2024 jijini Arusha. Ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa SCFEA uliongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango, Zanzibar, Mhe. Saada Mkuya na kumshirikisha pia Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Mhe. Stephen Byabato, Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu Mwamba, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango, Zanzibar, Dkt. Juma Malik Akil, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Alphayo Kidata na viongozi wengine waandamizi wa Serikali

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Mhe. Stephen Byabato (katikati) akichangia jambo wakati wa  Mkutano wa 16 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Fedha na Uchumi (SCFEA) la Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika Mei 17, 2024 jijini Arusha. Kushoto ni kiongozi wa ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano huo, Mhe. Waziri Mkuya na kulia ni Dkt. Mwamba

Mkutano ukiendelea

Viongozi wakiwa wamesimama wakati wa ufunguiz wa mkutano

Wajumbe wa mkutano wakifuatilia

Mkutano ukiendelea

Wajume wakifuatilia mkutano

Picha ya pamoja


 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.