Monday, May 13, 2024

RAIS SAMIA AWASILI PARIS, UFARANSA KWA ZIARA YA KIKAZI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amewasili jijini Paris, Ufaransa tarehe 12 Mei, 2024 na kupokelewa na Viongozi Waandamizi wa Serikali, Watumishi wa Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Ufaransa na Watanzania wanaoishi nchini humo.


Rais Samia ataongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi kuhusu Nishati Safi ya kupikia barani Afrika utakaofanyika Makao Makuu ya UNESCO na kuhudhuriwa na Marais wengine wa Afrika akiwemo Rais wa Jamhuri ya Sierra Leone, Mhe. Julius Maada Bio na Rais wa Ghana, Mhe. Nana Akufo-Addo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea maua kutoka kwa mtoto Khaira Ali Jabiri mara baada ya kuwasili jijini Paris, Ufaransa kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia utakaofanyika tarehe 14 Mei, 2024

Mhe. Rais Samia akisalimiana na Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Mhe. Suleiman Jaffo (Mb.) mara baada ya kuwasili jijini Paris, Ufaransa tarehe 12 Mei, 2024.

Mhe, Rais Samia akisalimia na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga (Mb.) mara baada ya kuwasili jijini Paris, Ufaransa tarehe 12 Mei, 2024.

Sehemu ya watumishi wa ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Ufaransa wakisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan mara baada ya kuwasili jijini Paris, Ufaransa tarehe 12 Mei, 2024.






 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.