Wednesday, May 22, 2024

BALOZI KAGANDA AKUTANA NA MKURUGENZI WA UHUSIANO WA KIMATAIFA WA DJIBOUTI

Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa (DMC) Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Noel Kaganda akizungumza na Mkurugenzi wa Uhusiano wa Kimataifa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ya Djibouti Balozi Guelleh Idriss Omar aliyemtembelea katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam



Mkurugenzi wa Uhusiano wa Kimataifa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ya Djibouti Balozi Guelleh Idriss Omar akizungumza alipokutana na Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa (DMC) Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Noel Kaganda katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam


Kikao kikiendelea

kikao kikiendelea

Kikao kikiendelea

Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa (DMC) Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Noel Kaganda akizungumza na Mkurugenzi wa Uhusiano wa Kimataifa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ya Djibouti Balozi Guelleh Idriss Omar aliyemtembelea katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam


Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa (DMC) Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Noel Kaganda katika picha  na Mkurugenzi wa Uhusiano wa Kimataifa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ya Djibouti Balozi Guelleh Idriss Omar alipomtembelea katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam


Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa (DMC) Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Noel Kaganda katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Uhusiano wa Kimataifa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ya Djibouti Balozi Guelleh Idriss Omar na timu yake walipomtembelea katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam


 

 

 

 

Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa (DMC) Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Noel Kaganda amekutana na Mkurugenzi wa Uhusiano wa Kimataifa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ya Djibouti Balozi Guelleh Idriss Omar katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam

 

Balozi Guelleh Idriss Omar yuko nchini na Ofisi ya Uratibu wa Kitaifa ya Djibouti kuhusu Uhamiaji (BCNM) kwa ziara ya kubadilishana uzoefu na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusu masuala ya uhamiaji kwa ushirikiano na Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM)

 

Ziara hiyo inalenga kuimarisha uwezo wa wawakilishi wa Serikali ya Djibouti katika usimamizi wa uhamiaji, kubadilishana na wadau muhimu kuhusu mbinu bora za usimamizi wa uhamiaji, kuendeleza ushirikiano kati ya nchi za Afrika Mashariki, hasa Tanzania, na kubadilishana uzoefu wa kivitendo katika usimamizi wa uhamiaji kati ya Djibouti na mamlaka za Tanzania.

Katika kikao hicho Balozi Kaganda aliithibitishia Djibouti dhamira ya Serikali ya Tanzania ya kudumisha uhusiano wa karibu wa kikazi na Serikali ya Djibouti, kwa lengo la kuimarisha zaidi ushirikiano na ubia kati yan chi hizo mbili.

Naye Balozi Guelleh Idriss Omar ameshukuru nafasi ya kujifunza juu ya namna Tanzania inavyooendesha shughuli za uhamiaji wa kimataifa na uhusiano na nchi nyingine  na kuahidi kuendelea kushirikiana na Tanzania kwa manufaa ya pande zote mbili.

 

Wajumbe wengine katika ziara hiyo ni pamoja na Bi. Ifrah Ali Ahmed, Mshauri Mkuu wa Waziri wa Mambo ya Ndani, Bw. Mohamed Houmed Abasse, Mkuu wa Wilaya ya Tadjourah, Bw. Hassan Abdi Robleh, Mkuu wa Mkoa wa Dikhil, Bi. Amana Awaleh Oumar, anayehusika na ulinzi katika BCNM, Bi. Hasna Omara Farah, anayehusika na maendeleo katika BCNM, na Bw. Abdallah Mohamed Bourhan, Afisa Mradi wa Kitaifa (BMM) - IOM Djibouti.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.