Sunday, May 12, 2024

WAZIRI MAKAMBA AONGOZA KIKAO CHA MAANDALIZI YA MKUTANO WA WAKUU WA NCHI KUHUSU NISHATI SAFI YA KUPIKIA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba akiongoza kikao cha maandalizi cha ujumbe wa Tanzania uliopo jijini Paris, Ufaransa kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi kuhusu Nishati Safi ya Kupikia utakaofanyika tarehe 14 Mei, 2024 katika Makao Makuu ya UNESCO.

Lengo la mkutano huo ni kulifanya suala zima la nishati safi ya kupikia kuwa la kipaumbele katika agenda ya kimataifa; kuanisha hatua madhubuti za kisera zitakazoharakisha matumizi ya nisahti safi ya kupikia na kutoa fursa ya washirika kutoa ahadi za kifedha, sera na ubia ili kufikia azma ya kukuza matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Kikao hicho cha maandalizi kimefanyika katika ofisi za ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Ufaransa tarehe 12 Mei, 2024.

Kutoka kushoto ni Mshauri wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania- Diplomasia, Balozi Maulida Hassan, Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Noel Kaganda na Mkuu wa Utawala na Fedha katika Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Ufaransa, Bw. Amos Tengu wakifatilia kikao kilichofanyika katika ofisi za ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Ufaransa tarehe 12 Mei, 2024. 


Wajumbe wa kikao hicho wakifatilia majadiliano.
Kikao kikiendelea. 

Kikao kikiendelea.
 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.