Wednesday, May 15, 2024

WAZIRI MAKAMBA AONGOZA MJADALA KUHUSU "NISHATI SAFI YA KUPIKIA KUWA SERA YA KIPAUMBELE BARANI AFRIKA"

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb.) ameongoza majadiliano kuhusu "Nishati Safi ya Kupikia kuwa Suala la Kipaumbele barani Afrika" uliofanyika katika Makao Makuu ya UNESCO jijini Paris, Ufaransa leo tarehe 14 Mei, 2024.

Aliongoza majadiliano hayo na mwenyekiti mwenza Mhe. Mary Robinson, Mwenyekiti wa Wazee na Rais Mstaafu wa Ireland.

Mjadala huo pamoja na masuala mengine ulijadili kwa kina umuhimu wa kila Nchi kuweka mikakati ya kisera ili kuhakikisha nishati safi ya kupikia inapatikana kwa uhakika na kwa gharama nafuu ili kuwafikia wananchi wote.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb.) akiongoza majadililiano kuhusu "Nishati Safi ya Kupikia kuwa Suala ya Kipaumbele Barani Afrika" uliofanyika jijini Paris, Ufarasa tarehe 14 Mei, 2024.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Januari Makamba pamoja na Mwenyekiti mwenza na Rais Mstaafu wa Ireland Mhe. Mary Robinson wakifatilia majadiliano.

Wakipongezana kwa kuongoza mjadala.

Majadiliano yakiendelea.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.