Friday, May 31, 2024

MAWAZIRI WA BIASHARA ,VIWANDA, FEDHA NA UWEKEZAJI WA EAC WAAZMIA KUBORESHA MAZINGIRA YA BIASHARA

Picha ya pamoja kwenye Mkutano wa 44 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji (SCTIFI) la Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika katika Makao Makuu ya Jumuiya hiyo jijini Arusha.

Mawaziri wanaosimamia sekta ya Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji katika Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kwa pamoja wamekubaliana kuendelea kuboresha ya mazingira ya biashara katika Jumuiya, huku wakitilia mkazo katika kuondoa vikwazo visivyo vya kodi, kurahisisha uvushaji wa mizigo mipakani, na kuimarisha utendaji wa miundombinu ya kusaidia biashara ikiwemo Vituo vya kutoa Huduma Pamoja Mpakani (OSBP). 

Vilevile wamekubaliana mapendekezo ya viwango mbalimbali vya ushuru wa forodha vitakavyo tumika katika mwaka wa fedha 2024/25 ambavyo vitachochea ukuaji wa uchumi wa nchi wanachama.

Azma hiyo imefikiwa leo tarehe 31 Mei 2024 kwenye Mkutano wa 44 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji (SCTIFI) la Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika katika Makao Makuu ya Jumuiya hiyo jijini Arusha.

Akizungumzia kuhusu azma hiyo Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba ameeleza kuwa hatua hiyo imefikiwa ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo yaliyotolewa na Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, ya kuwataka Watendaji na Viongozi walipo chini yao kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara na kuondoa vikwazo vya kibiashara katika Jumuiya.

Waziri Nchemba aliongeza kutaja maeneo yaliyofanyiwa maboresho katika mkutano huo kuwa ni pamoja makubaliano kuhusu viwango vya tozo za barabara kwa Nchi Wanachama kutoka Dola za Marekani 16 hadi 10. 

Eneo jingine ni makubaliano ya utekelezaji wa mkakati wa Himaya Moja ya Forodha (Single Customs Territory) hasa kwa upande wa Tanzania na Kenya, ambapo Tanzania ilishaanza utelezaji wake. 

Jamhuri ya Kenya imeahidi kuanza kupitisha bidhaa za Tanzania katika mfumo wa himaya moja ya forodha mara moja na kufikia mwenzi Julai 2024, na kuleta wafanyakazi wake wa mamlaka ya forodha kwa ajili ya kuwezesha ukaguzi kabla mzigo haujaanza kuondoka ili mzigo usisimame mpakani. Hatua hiyo itasaidia kuondoa msongamano, usumbufu na upotevu wa mapato kwa Serikali na wasafirishaji wa bidhaa kati ya Tanzani na Kenya.

“Tanzania tumekuwa tukikabiliwa na tatizo la msongamano wa maroli katika mipaka yetu ikiwemo Namanga, Sirari, Holili na Hororo, hii imechangiwa na kuto kuwepo kwa maafisa wa KRA upande wa Tanzania ambao wangesaidia kufanyia kazi nyaraka za kupitisha mzigo mpakani kabla gari husika halijafika mpakani tofauti na ilivyo sasa, utelezaji wa ahadi hii itasaidia kutatua tatizo hili lililo tusumbua kwa muda mrefu” Alisema Nchemba. 

Katika hatua nyingine Waziri Nchemba kwenye mkutano huo amewa ongoza Mawaziri wenzake kuzindua mfumo mpya wa Kielektroniki wa masuala ya forodha unaolenga kuongeza ufanisi katika biashara kwa kuweka mazingira ya uwazi, uwajibikaji na hatimaye kuongeza mapato kwa Serikali za Nchi Wanachama wa Jumuiya.

Mkutano huo wa Mawaziri ulitanguliwa na mkutano ngazi ya Wataalam uliofanyika tarehe 27 hadi 29 Mei 2024 na ngazi ya Makatibu Wakuu uliofanyika tarehe 30 Mei 2024. 

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato akifuatilia mkutano

Ujumbe wa Tanzania katika Mkutano huo umejumuisha Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba ambaye pia aliongoza ujumbe wa Tanzania, Mhe. Shariff Ali Shariff, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais anayeshughulikia Kazi, Uchumi na Uwekezaji- Zanzibar, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Exaud S. Kigahe.
Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba akichangia jambo kwenye Mkutano wa 44 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji (SCTIFI) la Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika katika Makao Makuu ya Jumuiya jijini Arusha.
Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato wakishirikishana jambo kwenye Mkutano wa 44 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji (SCTIFI) la Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Arusha.
Mawaziri Sekta ya Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji wa Afrika Mashariki wakishuhudia uzinduzi wa mfumo mpya wa Kielektroniki wa masuala ya forodha unaolenga kuongeza ufanisi na mapato kwa Serikali za Nchi Wanachama wa Jumuiya

Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Exaud S. Kigahe wakifuatilia Mkutano wa 44 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji (SCTIFI) la Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Arusha.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Biashara, Uwekezaji na Sekta za Uzalishaji Bw. Benjamin Mwesiga wakifuatilia Mkutano wa 44 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji (SCTIFI) la Jumuiya ya Afrika Mashariki
Mkutano ukiendelea
Mkutano ukiendelea
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais anayeshughulikia Kazi, Uchumi na Uwekezaji Zanzibar Mhe. Shariff Ali Shariff (kushoto) akichangia jambo kwenye Mkutano wa 44 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji (SCTIFI) la Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika katika Makao Makuu ya Jumuiya jijini Arusha.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.