Tuesday, August 8, 2023

MKUTANO WA WAKUU WA NCHI NA SERIKALI WA SADC NGAZI YA WATAALAMU WAANZA NCHINI ANGOLA

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Bi. Amina Shaban (mwenye mtandio) akiwa na ujumbe wa Tanzania unaoshiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ulioanza leo katika ngazi ya maafisa waandamizi jijini Luanda, Angola.
Mwenyekiti wa ngazi ya maafisa waandamizi aliyemaliza muda wake ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Ushirikiano wa Kikanda wa DRC, Balozi Songhu Kayumba (kulia) akikabidhi uenyekiti kwa Mwenyekiti mpya wa maafisa waandamizi kutoka Angola, Balozi Nazare Salvador ambaye ni Mkurugenzi wa Ofisi ya SADC nchini Angola katika Wizara ya Uhusiano wa Nje ya nchi hiyo.


Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ngazi ya maafisa waandamizi ukiendelea jijini Luanda, Angola.



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.