Monday, August 21, 2023

RAIS WA INDONESIA AWASILI NCHINI

Rais wa Jamhuri ya Indonesia, Mheshimiwa Joko Widodo amewasili nchini kwa ziara ya Kitaifa ya siku mbili kuanzia tarehe 21 – 22 Agosti, 2023.

Ni majira ya saa 4:40 alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam na kupokelewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb).

Viongozi wengine walioshiriki mapokezi ya Mheshimiwa Widodo ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Albert Chalamila, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo, Balozi wa Tanzania nchini Indonesia, Mhe. Macocha Tembele, Balozi wa Indonesia nchini, Mhe. Tri Yogo Jatmiko pamoja na viongozi wengine waandamizi wa Serikali.



Rais wa Jamhuri ya Indonesia, Mheshimiwa Joko Widodo akipokelewa na Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam baada ya kuwasili nchini kwa ziara ya Kitaifa ya siku mbili tarehe 21 - 22 Agosti, 2023






No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.