Saturday, November 28, 2020

UBALOZI WA TANZANIA AFRIKA KUSINI WAPEWA CHANGAMOTO YA KUTEKELEZA DIPLOMASIA YA UCHUMI, SIASA

Na Nelson Kessy, Pretoria

Ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini wapewa changamoto ya kuhakikisha kuwa unatekeleza Diplomasia ya Uchumi pamoja na Diplomasia ya Siasa iliyopo ndani ya Ilani ya Chama Cha Mapinduzi CCM (2020-2025).

Changamoto hiyo imetolewa na Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge wakati alipotembelea Ubalozi huo jijini Pretoria nchini Afrika Kusini kwa ajili ya kujionea utendaji kazi wa Ubalozi na mali za Serikali nchini humo. 

Balozi Ibuge ameutaka Ubalozi huo kuhakikisha kuwa unatekeleza diplomasia ya uchumi pamoja na diplomasia ya siasa kwa weledi ili kuleta manufaa ya Taifa.

"Nawapongeza kwa utendaji kazi wenu na nawasihi muendelee kujituma katika kazi (proactive) katika kuwapata wawekezaji na kutengeneza kuwa ni sehemu ya mfumo wa kuleta mabadiliko ambayo Serikali imeyapanga kupitia Ilani ya CCM ya 2020-2025," Amesema Balozi Ibuge.

Balozi Ibuge pia alipongeza utendaji wa Ubalozi huo ambao pamoja na Afrika Kusini unaiwakilisha Tanzania katika Ufalme wa Lesotho, Jamhuri ya Botswana, Jamhuri ya Namibia na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC). Kadhalika Balozi Ibuge alipokea changamoto mbalimbali zinazoikumba Ubalozi huo na Kuahidi kuzifanyia kazi ili kuongeza tija na ufanisi wa Ubalozi.

Kwa upande wake Balozi wa Tanzania Nchini Afrika Kusini, Meja Jenerali Gaudence Milanzi amemueleza Balozi Ibuge mafaniko mbalimbali ya Ubalozi katika kutekeleza diplomasia ya uchumi na siasa nchini Afrika Kusini.

Moja kati ya mafanikio hayo ni pamoja na kuenezwa kwa lugha ya Kiswahili ambapo Serikali ya Tanzania na ya Afrika Kusini zinatarajia kusaini mkataba wa kutumika lugha ya Kiswahili kama katika shule za Afrika Kusini mwezi wa Machi 2021.

"Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Serikali ya Afrika Kusini tutasaini mkataba wa kutumika kwa lugha ya Kiswahili katika shule za Afrika Kusini mwezi wa Machi 2021," Amesema Balozi Milanzi.

Pamoja na mambo mengine Balozi Milanzi ameahidi kusimamia sera ya Diplomasia ya uchumi pamoja na Diplomasia ya siasa kwa kuhakikisha kuwa ubalozi utaendelea kuwasiliana na wawekezaji mbalimbali wa kuwekeza nchini Tanzania katika sekta za Biashara, Madini na Mawasiliano.


Balozi wa Tanzania Nchini Afrika Kusini, Meja Jenerali Gaudence Milanzi akiwatambulisha baadhi ya wafanyakazi kwa Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ibuge wakati alipowasili Ubalozini leo tarehe 27 Novemba 2020


Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge akisaini kitabu cha wageni katika Ubalozi wa Tanzania Nchini Afrika Kusini leo tarehe 27 Novemba 2020


Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akisisitiza jambo kwa watumishi (hawapo pichani) wakati wa mkutano  


Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge akiendesha kikao na wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini  


Balozi wa Tanzania Nchini Afrika Kusini, Meja Jenerali Gaudence Milanzi akimuonesha baadhi ya mali Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi wakati alipokuwa anakagua mali za Serikali Ubalozini



 

 

 

 

 


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.