Friday, January 8, 2021

HABARI KTK PICHA WANG Yi AKUTANA, KUFANYA MAZUNGUMZO NA JPM

Mjumbe wa Baraza la Taifa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamuhuri ya Watu wa China, mhe. Wangi Yi ameendelea na ziara yake leo kwa kutembelea eneo la Mwalo wa Chato na kukutana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli pamoja na kuongea na vyombo vya Habari vya nchini akiwa yeye na mwenyeji wake, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi, (Mb).

Awali, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametoa wito kwa Watanzania kutumia uwepo wa soko la China katika kupeleka mazao ya kilimo yaliyoongezwa thamani.

Ametoa wito huo wilayani Chato wakati akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa China Wang Yi aliyepo nchini kwa ziara ya kikazi ambapo Rais Magufuli ameiomba serikali ya China kutumia ushirikiano na Tanzania kununua mazao ya kilimo hapa nchini.


Mjumbe wa Baraza la Taifa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamuhuri ya Watu wa China, mhe. Wangi Yi akiangalia jinsi bondo la samaki linavyotolewa na mmoja kati ya wavuvi wanaojishughulisha na shughuli za uvuvi katika Mwalo wa Chato mkoani Geita

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza Mjumbe wa Baraza la Taifa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamuhuri ya Watu wa China, mhe. Wangi Yi  wakati alipokuwa anaongea na waandishi wa Habari - Chato mkoani Geita

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi moja kati ya zawadi Mjumbe wa Baraza la Taifa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamuhuri ya Watu wa China, mhe. Wangi Yi 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Mjumbe wa Baraza la Taifa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamuhuri ya Watu wa China, mhe. Wangi Yi, Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi pamoja na baadhi ya Mawaziri wakiongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Mjumbe wa Baraza la Taifa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamuhuri ya Watu wa China, mhe. Wangi Yi, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Kabudi, Balozi wa China Nchini Tanzania, Mhe. Wang Ke pamoja na Makatibu Wakuu wa Wizara mbalimbali

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Kabudi, (Mb) akiongea na Waandishi wa Habari (hawapo pichani)- Chato mkoani Geita 

Mjumbe wa Baraza la Taifa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamuhuri ya Watu wa China, mhe. Wangi Yi akiongea na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) - Chato mkoani Geita 

 

Mjumbe wa Baraza la Taifa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamuhuri ya Watu wa China, mhe. Wangi Yi akiwaaga viongozi mbalimbali katika uwanja wa ndege wa Geita - Chato muda mfupi kabla ya kuondoka kwake



Mawaziri wakiongozwa na Prof. Kabudi wakimuaga Mjumbe wa Baraza la Taifa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamuhuri ya Watu wa China, mhe. Wangi Yi katika uwanja wa ndege wa Geita - Chato   


Ndege aliyokuja nayo Mjumbe wa Baraza la Taifa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamuhuri ya Watu wa China, mhe. Wangi Yi ikiondoka 



















No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.