Na Mwandishi wetu
Katika
kukuza Diplomasia ya Uchumi, kuimarisha na kushirikisha Jumuiya za Kimataifa Serikali
imekutana na Mabalozi, Wakuu na Wawakilishi wa Mashirika na Taasisi za Kimataifa
zilizopo hapa nchini kujadili Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha
2021/22 pamoja na mbinu za pamoja za kupambana na ugonjwa wa UVIKO 19.
Mkutano
huo umefanyika Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Wizara za Kisekta zikiwemo Fedha
na Mipango, Viwanda na Biashara, Afya, Maliasili na Utalii, Uwekezaji na Wizara
ya Fedha na Mipango – Zanzibar pamoja na Mabalozi na Wawakilishi wa mashirika
ya Kimataifa 54 kutoka nchi na taasisi mbalimbali.
Lengo
la Mkutano huo pamoja na mambo mengine, ni kuwapitisha Mabalozi na Wawakilishi
wa Mashirika ya Kimataifa kwenye Bajeti ya Serikali ya 2021/22, Mipango ya
Utekelezaji wake na Maeneo ya Ushirikiano.
Akiongoza
Mkutano huo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe.
Balozi Liberata Mulamula (Mb) ametaja sababu za Serikali kukutana na Mabalozi
pamoja na Wawakilishi wa Mashirika na Taasisi za Kimataifa ambao pia ni wadau
wa maendeleo ili kuwajengea uelewa katika mipango na utekelezaji wa Bajeti ya
Serikali ya 2021/22 pamoja na maeneo ya Ushirikiano.
“tumeona
tuweke utaratibu wa kukutana na wadau hawa wa maendeleo ili kujenga uelewa wa
pamoja katika maeneo muhimu yaliyoainishwa katika bajeti ya Serikali ili waweze
kupata picha halisi ya mipango na mikakati ya Serikali katika utekelezaji wa
Bajeti,” amesema Balozi Mulamula
Kwa
Upande wake Balozi wa nchi za Umoja wa Ulaya (EU) hapa Nchini, Mhe. Manfredo
Fanti amesema uamuzi wa Serikali wa kukutana na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika
na Taasisi za Kimataifa umekuwa mzuri sana umesaidia kufahamu mipango na
mikakati mbalimbali ya Serikali katika utekelezaji wa bajeti yake ya 2021/22.
“Kupitia
mkutano wa leo tumeweza kupata picha halisi ya ushirikiano wetu na Tanzania na umezidi
kuimarika lakini pia tumeweza kuona na kujadili baadhi ya vipaumbele vya bajeti
ya Serikali ya Tanzania, mipango ya maendeleo jambo ambalo sisi kama wadau wa
maendeleo limetuhamasisha kuendelea kushirikiana kwa ukaribu n a uwazi zaidi,” amesema
Balozi Fanti
Mkutano
huo umehudhuriwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Mwigula Nchema (Mb), Waziri
wa Viwanda na Biashara, Prof. Kitila Mkumbo (Mb), Waziri wa Maliasili na
Utalii, Dkt. Damas Ndumbaro (Mb), Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia,
Wazee na Watoto, Dkt. Dorothy Gwajima (Mb), Waziri wa Fedha na Mipango kutoka
Serikalini ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Jamal Kassim Ali, Pamoja na Naibu
Waziri Wizara ya Uwekezaji Mhe. William Tate Olenasha (Mb).
Pamoja
na Mambo mengine, Mawaziri hao wamepata fursa ya kutoa ufafanuzi katika maeneo
yanayohusu wizara zao ikiwa ni pamoja na mipango ya Serikali katika kukuza
uchumi, kukusanya mapato, kukuza Viwanda, kuboresha mazingira ya Biashara na
Uwekezaji, kukuza utalii na jinsi Serikali inavyojipanga kuboresha sekta ya
afya nchini hasa katika kupambana na janga la UVIKO 19.
 |
Baadhi
ya Mawaziri walioshiriki katika Mkutano wa Mabalozi, Wakuu na Wawakilishi wa
Mashirika na Taasisi za Kimataifa zilizopo hapa nchini kujadili Mapato na
Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2021/22 pamoja na mbinu za pamoja za
kupambana na ugonjwa wa UVIKO 19. Aliyevaa kitenge katikati ni Waziri wa Mambo ya
Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiongoza
Mkutano huo.  | Waziri
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb)
akichangia jambo wakati wa Mkutano wa Mabalozi, Wakuu na Wawakilishi wa
Mashirika na Taasisi za Kimataifa zilizopo hapa nchini kujadili Mapato na
Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2021/22  | Sehemu
ya Mabalozi, Wakuu na Wawakilishi wa Mashirika na Taasisi za Kimataifa zilizopo
hapa nchini wakifuatilia Mkutano |
|
 | Balozi
wa Canada hapa nchini, Mhe. Pamela O'Donnell akichangia jambo katika Mkutano wa
Mabalozi, Wakuu na Wawakilishi wa Mashirika na Taasisi za Kimataifa zilizopo
hapa nchini kujadili Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2021/22 |
 | Balozi
wa Kenya hapa nchini, Mhe. Dan Kazungu akichangia jambo katika Mkutano wa
Mabalozi, Wakuu na Wawakilishi wa Mashirika na Taasisi za Kimataifa zilizopo
hapa nchini kujadili Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2021/22
 | Mwakilishi
Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Mhe. Christine Musisi akichangia
jambo katika Mkutano wa Mabalozi, Wakuu na Wawakilishi wa Mashirika na Taasisi
za Kimataifa zilizopo hapa nchini | |
 | Balozi
wa Ufaransa hapa nchini, Mhe. Frederic Clavier akichangia jambo katika Mkutano wa
Mabalozi, Wakuu na Wawakilishi wa Mashirika na Taasisi za Kimataifa zilizopo
hapa nchini |
 | Balozi
wa Rwanda hapa nchini, Meja Jenerali Charles Karamba akichangia jambo katika Mkutano
wa Mabalozi, Wakuu na Wawakilishi wa Mashirika na Taasisi za Kimataifa zilizopo
hapa nchini |
 | Waziri
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb)
akiongea na waandishi wa habari leo Dar es Salaam mara baada ya kumalizika kwa
Mkutano wa Mabalozi, Wakuu na Wawakilishi wa Mashirika na Taasisi za Kimataifa
zilizopo hapa nchini |
 | Balozi
wa nchi za Umoja wa Ulaya (EU) hapa Nchini, Mhe. Manfredo Fanti akiongea na
waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa Mkutano wa Mabalozi, Wakuu na
Wawakilishi wa Mashirika na Taasisi za Kimataifa zilizopo hapa nchini |
|