Monday, July 8, 2024

MAANDALIZI YA MKUTANO WA 26 WA KAMATI YA MAWAZIRI WA ASASI YA SIASA, ULINZI NA USALAMA YA SADC YAANZA JIJINI LUSAKA

Mkutano wa 26 wa Kawaida wa Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Ushirikiano katika masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC-MCO) unatarajiwa kufanyika tarehe 11 na 12 Julai 2024 jijini Lusaka, Zambia. 

 

Mkutano huo umetanguliwa na Mkutano wa Kamati ya Makatibu Wakuu unaofanyika tarehe 08 na 09 Julai 2024 jijini hapa ambapo ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano huu unaongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo.

 

Mkutano wa 26 unalenga pamoja na mambo mengine kujadili agenda mbalimbali zenye lengo la kukuza na kuimarisha hali ya siasa, ulinzi na usalama katika Kanda ya SADC.

 

Akizungumza wakati wa ufunguzi rasmi wa Mkutano wa Makatibu Wakuu uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mulungushi jijini Lusaka, Mwenyekiti ambaye pia ni Katibu Mkuu anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ya Zambia, Bi. Etambuyu Gundersen amewakaribisha wajumbe wa mkutano huo na kuwataka kujadili kikamilifu agenda mbalimbali zilizopo mbele yao kabla ya kuziwasilisha kwa Mawaziri.

 

Aidha, kuhusu hali ya usalama na amani katika Kanda ya SADC, Bi. Etambuyu amesema kuwa, hali ni shwari huku akisisitiza kuendelea na jitihada za pamoja ili kuhakikisha amani ya kudumu inapatikana katika maeneo machache yenye changamoto za kiusalama katika kanda ikiwemo eneo la Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

 

Kadhalika ametumia fursa hiyo kuzipongeza Jamhuri ya Afrika Kusini na Jamhuri ya Madagascar kwa kuendesha kwa amani na utulivu zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge lililofanyika katika nchi hizo hivi karibuni.

 

Mbali na Balozi Shelukindo, viongozi wengine kutoka Tanzania wanaoshiriki Mkutano wa Makatibu Wakuu ni pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Faraji Mnyepe,  Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Jacob Mkunda,  Balozi wa Tanzania nchini Zambia, Mhe. Lt. Jen. Mathew Mkingule, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na  Kupambana na Rushwa,  Kamishna wa Polisi Salum  Hamduni, Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Talha Waziri na Maafisa Waandamizi wa Wizara na Vyombo vya ulinzi na Usalama.

Mwenyekiti wa Mkutano wa Kamati ya Makatibu Wakuu wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ambaye pia ni Katibu Mkuu anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ya Zambia, Bi. Etambuyu Gundersen akifungua rasmi mkutano huo uliofanyika tarehe 8 Julai 2024 jijini Lusaka, Zambia. Mkutano huo ni maandalizi ya Mkutano wa 26 wa Kawaida wa Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Ushirikiano katika masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa SADC unaotarajiwa kufanyika tarehe 11 na 12 Julai 2024
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo akiongoza ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa Kamati ya Makatibu Wakuu wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC unaofanyika jijini Lusaka, Zambia tarehe 8 na 9 Julai 2024

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Faraji Mnyepe (kushoto) akiwa na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Jacob Mkunda (katikati) pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na  Kupambana na Rushwa,  Kamishna wa Polisi Salum  Hamduni (kulia) wakishiriki hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Kamati ya Makatibu Wakuu wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) unaofanyika Lusaka, Zambia
Balozi Shelukindo akimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Talha Waziri wakati akifafanua jambo kwake kuhusu agenda za mkutano
Ujumbe wa Zambia ambao ni wenyeji wa Mkutano huo wakishiriki hafla ya ufunguzi

Ujumbe wa  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) wakishiriki hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Kamati ya Makatibu Wakuu

Ujumbe wa  Madagascar wakishiriki hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Kamati ya Makatibu Wakuu

Ujumbe wa Malawi wakishiriki hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Kamati ya Makatibu Wakuu
Ujumbe wa Angola wakishiriki hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Kamati ya Makatibu Wakuu
Ujumbe wa  Lesotho wakishiriki hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Kamati ya Makatibu Wakuu
Ujumbe wa  Botswana wakishiriki hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Kamati ya Makatibu Wakuu
Ujumbe wa  Msumbiji wakishiriki hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Kamati ya Makatibu Wakuu
Ujumbe wa Shelisheli wakishiriki hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Kamati ya Makatibu Wakuu

Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bibi. Talha Waziri akifuatilia hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Kamati ya Makatibu Wakuu wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC

Mkutano ukiendelea






 

Saturday, July 6, 2024

WAZIRI MAKAMBA AONGOZA KIKAO CHA MAWAZIRI 15 WA EAC

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akiongoza kikao cha Mawaziri wa Mambo ya Nje na Mawaziri wanaoshugulikia masuala ya Afrika Mashariki katika Jumuiya ya Afrika Mashariki unaofanyika Zanzibar.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba (katikati) akiongoza Mkutno wa Faragha wa Mawaziri wa Mambo ya Nje na Mawaziri wanaoshugulikia masuala ya Afrika Mashariki katika Jumuiya ya Afrika Mashariki unaofanyika Zanzibar.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akiongoza Mkutano wa Faragha wa Mawaziri wa Mambo ya Nje na Mawaziri wanaoshugulikia masuala ya Afrika Mashariki katika Jumuiya ya Afrika Mashariki unaofanyika Zanzibar.


Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk  (wa kwanza kushoto)  akishiriki Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje na Mawaziri wanaoshugulikia masuala ya Afrika Mashariki katika Jumuiya ya Afrika Mashariki unaofanyika Zanzibar.

Wajumbe kutoka nchi za Rwanda, Burundi na Kenya wakishirikia Mkutano wa faragha wa Mawaziri wa Mambo ya Nje na Mawaziri wanaoshugulikia masuala ya Afrika Mashariki katika Jumuiya ya Afrika Mashariki unaofanyika Zanzibar.

Mawaziri na Makatibu Wakuu walishiriki Mkutano wa faragha wa Mawaziri wa Mambo ya Nje na Mawaziri wanaoshugulikia masuala ya Afrika Mashariki katika Jumuiya ya Afrika Mashariki unaofanyika Zanzibar.



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba ameongoza kikao cha Mawaziri wa Mambo ya Nje na Mawaziri wanaoshugulikia masuala ya Afrika Mashariki katika Jumuiya ya Afrika Mashariki unaofanyika Zanzibar.

Akizungumza katika Mkutano wa faragha wa siku tatu ambacho yeye ni mwenyekiti  Mhe. Makamba amesema Tanzania imejidhatiti kuhakikisha Jumuiya ya Afrika Mashariki inakuwa imara, yenye umoja na inayofikia malengo yake.

“Madhumuni ya mkutano huu ni kuifanya familia yetu inakuwa imara, kuifanya Jumuiya ya Afrika Mashariki kutekeleza majukumu yake vizuri, Tanzania kama moja ya waanzilishi wa Jumuiya hii tumejidhatiti kuona jumuiya ikiwa na umoja, imara na yenye kufanikiwa” alisema Mhe. Makamba

Akiungumza katika kikao hicho Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Mhe. Musalia Mudavadi ameipongeza Tanzania kwa kukubali kuwa mwenyeji wa mkutano huo na kuongeza kuwa ni wakati muafaka kwa nchi wanachama kuhakikisha wanatumia fursa mbalimbali ndani ya jumuiya kwa manufaa ya wananchi.

Naye Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Afrika Mashariki wa Uganda Mhe. Rebecca Kadaga ameishukuru Serikali ya Tanzania kwa kuwa mwenyeji wa mkutano huo na kupongeza juhudi za kuimarisha jumuiya.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri Mhe. Dend Alor Kuol amesema kufanyika kwa kikao hicho ni jambo jema hasa ikizingatiwa kuwa kitaangalia masuala ya amani na usalama na mtangamano wa jumuiya ikiwa ni hatua za kuifanya jumuiya kusonga mbele.


Wakizungumza katika mkutano huo Mawaziri kutoka nchi wanachama wa EAC wanaohudhuria mkutano huo wameipongeza Tanzania kwa kukubali kuwa mwenyeji wa mkutano huo wa kwanza na wa kihistoria kufanyika ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Mkutano huo wa faragha unajadili taarifa ya Mwenyekiti wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya; hali ya amani, usalama, siasa na uhusiano kati ya nchi wanachama;  kutathmini na kujadili mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na masuala yanayokwamisha ufikiwaji wa malengo ya programu na miradi inayopangwa.

Mkutano kazi huo umeandaliwa kwa ushirikiano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika kwa njia ya mtandao tarehe 07 Mei, 2024.

Mawaziri kutoka nchi Nane Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki za Burundi, DRC, Kenya, Rwanda, Somalia, Sudan Kusini, Uganda, na Mwenyeji Tanzania wanahudhuria mkutano huo. Mkutano huo pia unahudhuriwa na Makatibu Wakuu wa Wizara hizo, maafisa waandamizi wa Wizara hizo na Wajumbe wa Secretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki wakiongozwa na Katibu Mkuu wa Jumuiya Bibi. Veronica Ndungu.

 

BALOZI MBAROUK ASHIRIKI MKUTANO WA MAANDALIZI WA KONGAMANO LA TISA LA DIASPORA AFRIKA

 

 


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb) akishiriki Mkutano wa Maandalizi wa Kongamano la Tisa la Diaspora baranı Afrika uliofanyika kwa njia ya mtandao.

Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb) akifuatilia mkutano huo wa Maandalizi wa Kongamano la Tisa la Diaspora baranı Afrika uliofanyika kwa njia ya mtandao.

Balozi Mbarouk  akifuatilia  Mkutano wa Maandalizi wa Kongamano la Tisa la Diaspora baranı Afrika uliofanyika kwa njia ya mtandao.


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb) ameshiriki Mkutano wa Maandalizi wa Kongamano la Tisa la Diaspora baranı Afrika uliofanyika kwa njia ya mtandao. 

Mkutano huo wa Umoja wa Afrika wa maandalizi kwa ajili ya Kongamano la Tisa kuhusu Diaspora wa Afrika na wenye Asili ya Afrika litakalofanyika nchini Togo baadaye mwaka huu. 

Akizungumza katika mkutano huo Balozi Mbarouk, aliuthibitishia mkutano huo kuwa Tanzania inaunga mkono Kongamano hilo na malengo yake lililopangwa kufanyika nchini Togo. 

Amesema Umoja wa Afrika na Mashirika ya Kikanda yamechukua hatua kadhaa kukuza na kuimarisha matumizi ya lugha za Kiafrika na tamaduni zake ikiwa ni pamoja na kutumia lugha ya Kiswahili katika ngazi za kitaifa, kikanda na kimataifa. 

Amesema jitihada hizo zililiwezesha Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO)  kuitangaza tarehe 7 Julai ya kila mwaka kuwa Siku ya Kiswahili Duniani. 

“Haya ni mafanikio makubwa kwa Afrika, Kiswahili kimekuwa moja ya lugha zinazotumika sana kutoka familia ya lugha za Kiafrika duniani ikiwa na zaidi ya wazumgumzaji milioni 230, na kuwa miongoni mwa lugha 10 zinazozungumzwa zaidi duniani, alisema Balozi Mbarouk.

Thursday, July 4, 2024

RAIS SAMIA AMUAGA RAIS NYUSI ZANZIBAR

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amemuaga Rais wa Msumbiji Mheshimiwa Filipe Nyusi katika uwanja wa ndege wa Abeid Amani Karume Zanzibar.


Mheshimiwa  Nyusi ameondoka nchini baada ya kumaliza ziara ya Kitaifa ya siku nne nchini.

Katika Uwanja wa Ndege wa Kimaraifa wa Abeid Amani Karume Mheshimiwa Nyusi ameagwa na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan.

Mheshimiwa Nyusi pia alisindikizwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba na viongozi wengine wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Akiwa nchini Mhe. Nyusi pamoja na kuzungumza na mwenyeji wake kwa lengo la kuendelea kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na wa kibiashara kati ya Tanzania na Msumbiji pia alifungua rasmi Maonesho ya Kimataifa ya 48 ya Dar es Salaam maarufu kama SabaSaba.

Kufuatia ziara hiyo Tanzania na Msumbiji zimekubaliana kuendelea kuimarisha uhusiano na zimesaini Hati mbili za Makubaliano ya ushirikiano katika sekta za afya na biashara ikiwa ni alama ya mafanikio ya ziara ya kitaifa ya siku nne ya Mhe. Filipe Nyusi, Rais wa Msumbiji.

Pia zimekubaliana pamoja na mambo mengine kuongeza ushirikiano katika sekta ya biashara na uwekezaji ikiwa ni pamoja na kuanzisha kituo cha pamoja cha biashara mipakani ili kurahisisha ufanyaji biashara kati ya wananchi wa nchi hizi mbili.

 

 Rais wa Msumbiji Mheshimiwa Filipe Nyusi akipunga mkono kuaga katika uwanja wa ndege wa Abeid Amani Karume Zanzibar alipoondoka nchini baada ya kumaliza ziara ya kitaifa nchini .

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiwa na  Rais wa Msumbiji Mheshimiwa Filipe Nyusi wakipokea salamu za heshima  katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar alipoondoka nchini baada ya kumaliza ziara ya kitaifa nchini

 

 

 


 

 










 

RAIS NYUSI AKUTANA NA DKT. MWINYI ZANZÄ°BAR

Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Mheshimiwa Filipe Nyusi amekutana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi Ikulu Zanzibar

Akizungumza na Dkt. Mwinyi Mheshimiwa Nyusi alitumia nafasi hiyo kumuaga kwa kuwa amemaliza kipindi chake cha uongozi nchini Msumbiji na kumshukuru kwa Ushirikiano aliompatia alipokuwa Waziri wa Ulinzi wa Tanzania.

Amemuahidi kuwa Msumbiji itaendelea kudumisha uhusiano na ushirikiano wake na Tanzania haÅŸa ikizingatiwa historia ya uhusiano uliopo kati ya Tanzania na Msumbiji

Naye Mhe. Dkt. Mwinyi amemshukuru Mhe. Nyusi kwa kumtembelea Zanzibar na kumkaribisha kutembelea Zanzibar wakati mwingine.

Mheshimiwa Nyusi alikuwa nchini kwa ziara ya kitaifa kuanzia tarehe Mosi Julai 2024

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi akimpokea Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Mheshimiwa Filipe Nyusi alipowasili Ikulu Zanzibar

 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Mheshimiwa Filipe Nyusi alipowasili Ikulu Zanzibar

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi akiwa na Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Mheshimiwa Filipe Nyusi alipowasili Ikulu Zanzibar

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi akiwa na Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Mheshimiwa Filipe Nyusi alipomtembelea Ikulu Zanzibar

 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi na ujumbe wake akizungumza na Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Mheshimiwa Filipe Nyusi alipomtembelea  Ikulu Zanzibar
Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Mheshimiwa Filipe Nyusi akizungumza alipomtembelea Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani)  Ikulu Zanzibar

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi akimkabidhi zawadi ya Picha   Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Mheshimiwa Filipe Nyusi   alipomtembelea  Ikulu Zanzibar
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi akiwa na Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Mheshimiwa Filipe Nyusi katika picha ya pamoja  alipomtembelea  Ikulu Zanzibar