Tuesday, February 19, 2013

Mhe. Mahadhi akutana na Msajili wa Mahakama ya ICTR

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) akizungumza na Msajili Mpya wa Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR) ya Jijini Arusha, Mhe. Bongani Majola (hayupo pichani) wakati Msajili huyo alipofika Wizarani kwa mazungumzo na Mhe. Mahadhi  juu ya masuala mbalimbali kuhusu Mahakama hiyo.

Mhe. Mahadhi (kulia) akiendelea na mazungumzo na Mhe. Bongani Majola, Msajili Mpya wa Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR) alipofika Ofisini kwa Mhe. Mahadhi kwa mazungumzo.

Mhe. Mahadhi akifafanua jambo kwa Mhe. Majola wakati wa mazungumzo yao. Wengine katika picha ni wajumbe waliofuatana na Mhe. Majola. Kulia ni Bw. Roland Konassi Amoussouga ambaye ni Mshauri Mwandamizi wa Sheria na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mipango wa ICTR na kushoto ni Bw. Jerry Mburi, Afisa Sheria na Utawala wa ICTR.

Mhe. Majola akiendelea na mazungumzo na Mhe. Mahadhi.
Mhe. Mahadhi na Wajumbe wengine wa ICTR wakimsikiliza Mhe. Majola.

Mhe. Mahadhi akimsikiliza Bw. Amoussouga alipokuwa akifafanua jambo.

Mhe. Majola (kulia) na Bw. Mburi wakimsikiliza mwenzao Bw. Amoussouga (hayupo pichani) alipokuwa anafafanua jambo kwa Mhe. Mahadhi (naye hayupo pichani)

Bw. Benedict Msuya (kulia), Afisa kutoka Kitengo cha Sheria, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akinukuu mazungumzo kati ya Mhe. Mahadhi na ujumbe kutoka ICTR. Mwingine katika picha ni Bw. Amoussouga mmoja wa wajumbe kutoka ICTR.

Mhe. Mahadhi akiagana na Mhe. Majola mara baada ya mazungumzo yao.

Mhe. Mahadhi akifurahia jambo na Bw. Amoussouga wakati wa kuagana.

UTEUZI WA BODI YA CHUO CHA DIPLOMASIA




TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Balozi Mwanaidi Sinare Maajar kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Diplomasia (CFR) kilichopo Kurasini Jijini Dar es Salaam.

Aidha, kufuatia uteuzi huo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Kamillius Membe (Mb.) amewateua Wajumbe wa Bodi hiyo kuwa ni:-

1.           Bw. Dushhood M. K. Mndeme
2.           Mhe. Balozi Abdi Mshangama
3.           Mhe. Dkt. Leonidas Mushokolwa
4.           Mhe. Dkt. Harold Utouh
5.           Mhe. Saidi Mtanda (Mb.)
6.           Mhe. Betty Machangu (Mb.)
7.           Bw. Affan Othman Maalim
8.           Bw. Abdurahaman Abdallah

Uteuzi wa Mwenyekiti na Wajumbe hao ni kwa kipindi cha miaka mitatu (3) kuanzia tarehe 22 Januari, 2013 hadi tarehe 21 Januari, 2016.

   
IMETOLEWA NA: WIZARA YA MAMBO YA NJE NA

USHIRIKIANO WA KIMATAIFA, DAR ES SALAAM


15 FEBRUARI, 2013

Saturday, February 16, 2013

Nchi za EAC zasaini Itifaki ya Amani na Usalama





Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), akiweka saini Itifaki ya Amani na Usalama ya Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC). Uwekaji saini huo ulifanyika katika Hoteli ya New Africa, jijini Dar es Salaam.


Mhe. Membe (wa pili kushoto) akiwa na viongozi wenzake wa nchi za EAC wakiwa wameshikilia Itifaki hiyo mara baada ya kusainiwa

Mhe. Membe akipitia Itifaki hiyo kabla ya kusainiwa huku Bw. John M. Haule, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akishuhudia.
Mhe. Membe akijadiliana jambo na Katibu Mkuu wake Bw. Haule. Mwingine katika picha ni Mhe. Pereira Ame Silima (Mb.), Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi.

Picha nyingine ya Mhe. Membe na Katibu Mkuu wake Bw. Haule na wajumbe wengine waliohudhuria mkutano huo.

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dkt. Richard Sezibera (kulia) akijadiliana jambo na Waziri wa Ulinzi wa Uganda.

Mhe. Membe akifanya mahojiano na Waandishi wa Habari baada ya shughuli ya utiaji saini kukamilika.

Picha zaidi za mahojiano kati ya Mhe. Membe na Waandishi wa Habari.














Friday, February 15, 2013

Waziri Membe akutana na Uongozi wa APRM Tanzania

Mhe Waziri leo amekutana na uongozi wa APRM Tanzania. Ujumbe huo chini ya Mwenyekiti Prof. Hassa Mlawa, umetumia fursa hiyo kumshukuru Mhe. Waziri Membe kwa ushirikiano alioutoa yeye kama Focal Point wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wizara kwa ujumla, ikiwemo kulipwa kwa deni la muda mrefu la mchango wa Tanzania katika Sekretariati ya APRM na kuliondolea taifa aibu. Aidha, Ujumbe huo ulitumia fursa hiyo kumueleza Mhe. Waziri juu ya hatua zinazofuata katika utekelezaji wa yatokanayo na Ripoti ya Tathmini ya Tanzania.
Mhe. Membe alipongeza Uongozi wa APRM kwa kazi nzuri waliyoifanya kwa uadilifu mkubwa na kuiletea Tanzania heshima. Ametumia fursa hiyo kuwahakikishia ushirikiano wa Wizara yake katika kuratibu utekelezaji wa yatokanayo na Ripoti hiyo.
Amewataka APRM kusambaza taarifa hiyo kwa wananchi na wadau wote kwa kuwa taarifa hiyo ni ya umma.


Wednesday, February 13, 2013

Courtesy visit of Indonesian Ambassador to Tanzania


Ambassador Mbelwa Kairuki (right), Director of the Department of Asia and Australasia in a discussion with H.E. Zakaria Anshar, the new Ambassador of the Republic of Indonesia to the United Republic of Tanzania.  

H.E. Ambassador Anshar paid a courtesy visit earlier today, with the purpose to explain his Country's desire to increase technical cooperation in various sectors in the coming years.  For a long time now, Indonesia has been actively involved in developing agriculture sector and providing training programs for farmers in Tanzania. 

Ambassador Kairuki explains how Tanzania has benefited from Indonesia's support in its training programs especially in agricultural field and expressed the Government's commitment to continue economic cooperation with Indonesia.

Ambassador Kairuki (center) in a discussion with Ambassador Anshar of Indonesia earlier today in his office.  Also in the photo is Mr. Charles Faini, Foreign Service Officer in the Ministry of Foreign Affairs.

Ambassador Kairuki, Director of the Department of Asia and Australasia and H.E. Ambassador Anshar of the Republic of Indonesia to Tanzania shake hands at the end of their discussion, solidifying the lasting, friendly relation that exist between the two countries.


Photos by Tagie Daisy Mwakawago 




Kikao cha wadau cha maandalizi ya mkutano wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Oman chafanyika

Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya (katikati) akipitia kumbukumbu wakati akiongoza kikao cha Wadau cha maandalizi ya Mkutano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Oman unaotarajiwa kufanyika Jijini Dar es Salaam tarehe 24 na 25 Februari, 2013. Wengine katika picha ni Balozi Bertha Semu-Somi (kulia), Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Bw. Elibariki Maleko, Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Mashariki ya Kati.
Baadhi ya wadau waliohudhuria kikao hicho wakimsikiliza mwenyekiti (hayupo pichani)
Wadau wengine wakati wa kikao hicho.

Hon. Membe in talks with the Director of the Word Food Programme


Hon. Bernard K. Membe (MP), Minister for Foreign Affairs and International Co-operation welcomes Ms. Ertharin Cousin, Executive Director of the United Nations World Food Programme (WFP) today in his office in Dar es Salaam.  Ms Cousin is in the country to visit and review areas of cooperation, particularly the operation status of the school feeding program.

 
Ambassador Mushy greets and welcomes Ms. Ertharin Cousin, Executive Director of the United Nations World Food Programme.  Also in the photo is Mr. Richard Ragan, Representative and Country Director of the UN's WFP in the United Republic of Tanzania.

Hon. Membe listens to Ms. Cousins explanation about the WFP and its food preservation and school feeding programs.

Other Representatives from the WFP that included Ms Shannon Howard (left), Programme Officer, Ms. Sarah Gordon-Gibson (2nd left), Deputy Country Director and Mr. Richard Ragan, Representative and Country Director of the UN's WFP in the United Republic of Tanzania.

Ambassador Celestine Mushy (left), Director of the Department of Multilateral Cooperation was also in attendance during the meeting.  Others in the photo are Mr. Togolani Mavura (center), Private Assistant to Hon. Minister Membe and Mr. Songelaeli Shilla, Economist in the Ministry of Foreign Affairs.  

Hon. Membe and Ms. Cousin in a discussion during their meeting today.

Hon. Bernard K. Membe (MP), making a point during his discussion with Ms. Ertharin Cousin of the UN's World Food Programme.

Mr. Richard Ragan (left), Representative and Country Director of the UN's WFP in Tanzania explains impacts of outflow of refugees during the meeting with Hon. Membe.

Hon. Membe highlighting various areas that needs improvements and that can benefit from the UN's WPF during his meeting with Ms. Cousin. 


All photos by Tagie Daisy Mwakawago 


Mhe. Membe akutana na Ujumbe wa Wabunge kutoka Ujerumani

Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwa na Mhe. Klaus-Peter
Willsch, Kiongozi wa Ujumbe wa Wabunge wa Kamati ya Bajeti ya Bunge la Ujerumani alipokutana nae Wizarani kwa  mazungumzo kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Ujerumani.

Mhe. Membe akimsikiliza Mhe. Willsch wakati wa mazungumzo yao.
Mhe. Willsch (kulia kwa Waziri Membe) akimsikiliza Mhe. Membe wakati wa mazungumzo yao. Wengine katika picha ni baadhi ya Wabunge wa Kamati ya Bajeti ya Bunge la Ujerumani pamoja na Mhe. Klaus-Peter Brandes ( wa sita kutoka kushoto), Balozi wa Ujerumani hapa nchini.

Wajumbe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakimsilikiza Mhe. Membe (hayupo pichani) wakati wa mazungumzo yake na Wabunge kutoka Ujerumani. Kutoka kushoto ni Balozi Dora Msechu, Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika,Bibi Zainab Angovi, Afisa kutoka Idara ya Ulaya na Amerika na Bw. Grayson Ishengoma, Afisa kutoka Idara ya Ulaya na Amerika.

Mhe. Membe akifurahia Medali Maalum aliyokabidhiwa na Mhe. Willsch kama ishara ya kutambua ushirikiano mzuri uliopo kati ya Tanzania na Ujerumani.

Mhe. Membe akiwa katika picha ya pamoja na Ujumbe huo.



Tanzania emerges a winner in 3 of its tourist attractions




At last Tanzania won 3 of Africa's Seven Natural Wonders!


At last the three Tanzania tourist attractions candidates for seven Natural Wonders of Africa emerged among the seven winners? Kilimanjaro, Ngorongoro and the Serengeti. Congrats Tanzania!

Mt. Kilimanjaro

Ngorongoro crator



Tuesday, February 12, 2013

Mhe. Membe akutana kwa mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Atomiki Duniani

Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwa katika mazungumzo na Mhe. Yukiya Amano, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nguvu za Atomiki Duniani (IAEA) alipofika kumtembelea Wizarani leo.
Mhe. Yukiya Amano, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nguvu za Atomiki Duniani akifafanua masuala mbalimbali kuhusu Shirika hilo kwa  Mhe. Membe.
Mhe. Membe (kushoto) na Mhe. Prof. Makame M. Mbarawa (Mb.), Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nguvu za Atomiki Duniani, Mhe. Yukiya Amano (hayupo pichani) wakati akizungumza nao leo.
Mhe. Juma Duni Haji (kulia), Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,  Mhe. Dkt. Binilith Mahenge (katikati), Naibu Waziri wa Maji na Balozi Celestine Mushy (kushoto), Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nguvu za Atomiki Duniani, Mhe. Yukiya Amano (hayupo pichani).
Mhe. Yukiya Amano (kulia), Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nguvu za Atomiki Duniani akimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani) wakati wa mazungumzo yao leo. Wengine katika picha ni Prof. Manase Selema (katikati), Mkurugenzi wa Divisheni ya Ulaya ya Shirika hilo na Bw. Conleth Brady, Msaidizi wa Mkurugenzi Mkuu.
Mhe. Membe akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Yukiya Amano mara baada ya mazungumzo yao.

Friday, February 8, 2013

Ambassador Kairuki holds a meeting with Chinese Ambassador


Ambassador Mbelwa Kairuki (left), Director of the Department of Asia and Australasia in the Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation, today met with H.E. Ambassador Lu Youqing, Ambassador of the People's Republic of China in the United Republic of Tanzania to discuss various areas of strengthening cooperation between the two countries.  Among the pertinent issues discussed, the Ambassadors also discussed the energy sector and its potential to Chinese investors. 
 
Ambassador Kairuki and Ambassdor Youqing in discussion together with other officials from both Tanzania and Chinese Governments.  From left is Mr. Ouyang Zhibing, Senior Officer from Embassy of the Republic of China to Tanzania, Mr. Lin Zhiyon (2nd left), Officer in charge of Economic Affairs in the Chinese Embassy and Mr. Ren (3rd left), Interpreter.  Others are Ms. Haika (right) and Mr. Ngaiza (2nd right), Foreign Service Officers in the Ministry of Foreign Affairs.  

Ambassador Kairuki and Ambassador Youqing share a light moment during their discussion. 
 
Ambassador Kairuki and Ambassador Youqing in a photo after their discussion held today in the Ministry of Foreign Affairs in Dar es Salaam. 

 
Photos by Tagie Daisy Mwakawago

 

Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa akutana na Mwakilishi Mkazi wa UN nchini

Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy (kushoto) akizungumza masuala mbalimbali ya ushirikiano na Mwakilishi Mkazi wa Mashirika ya Kimataifa hapa nchini, Dkt. Alberic Kacou. Mazungumzo hayo yalifanyika Wizarani tarehe 8 Februari, 2013.
Balozi Mushy kulia akimsikiliza Dkt. Kacou wakati wa mazungumzo yao leo.
Dkt. Kacou akimsikiliza Balozi Mushy wakati wa mazungumzo yao leo. Mwingine katika picha ni Bi. Tunsume Mwangolombe, Afisa Mambo ya Nje akinukuu mazungumzo hayo.