Wednesday, February 13, 2013

Kikao cha wadau cha maandalizi ya mkutano wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Oman chafanyika

Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya (katikati) akipitia kumbukumbu wakati akiongoza kikao cha Wadau cha maandalizi ya Mkutano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Oman unaotarajiwa kufanyika Jijini Dar es Salaam tarehe 24 na 25 Februari, 2013. Wengine katika picha ni Balozi Bertha Semu-Somi (kulia), Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Bw. Elibariki Maleko, Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Mashariki ya Kati.
Baadhi ya wadau waliohudhuria kikao hicho wakimsikiliza mwenyekiti (hayupo pichani)
Wadau wengine wakati wa kikao hicho.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.