Saturday, February 16, 2013

Nchi za EAC zasaini Itifaki ya Amani na Usalama





Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), akiweka saini Itifaki ya Amani na Usalama ya Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC). Uwekaji saini huo ulifanyika katika Hoteli ya New Africa, jijini Dar es Salaam.


Mhe. Membe (wa pili kushoto) akiwa na viongozi wenzake wa nchi za EAC wakiwa wameshikilia Itifaki hiyo mara baada ya kusainiwa

Mhe. Membe akipitia Itifaki hiyo kabla ya kusainiwa huku Bw. John M. Haule, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akishuhudia.
Mhe. Membe akijadiliana jambo na Katibu Mkuu wake Bw. Haule. Mwingine katika picha ni Mhe. Pereira Ame Silima (Mb.), Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi.

Picha nyingine ya Mhe. Membe na Katibu Mkuu wake Bw. Haule na wajumbe wengine waliohudhuria mkutano huo.

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dkt. Richard Sezibera (kulia) akijadiliana jambo na Waziri wa Ulinzi wa Uganda.

Mhe. Membe akifanya mahojiano na Waandishi wa Habari baada ya shughuli ya utiaji saini kukamilika.

Picha zaidi za mahojiano kati ya Mhe. Membe na Waandishi wa Habari.














No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.