Tuesday, February 12, 2013

Mhe. Membe akutana kwa mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Atomiki Duniani

Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwa katika mazungumzo na Mhe. Yukiya Amano, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nguvu za Atomiki Duniani (IAEA) alipofika kumtembelea Wizarani leo.
Mhe. Yukiya Amano, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nguvu za Atomiki Duniani akifafanua masuala mbalimbali kuhusu Shirika hilo kwa  Mhe. Membe.
Mhe. Membe (kushoto) na Mhe. Prof. Makame M. Mbarawa (Mb.), Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nguvu za Atomiki Duniani, Mhe. Yukiya Amano (hayupo pichani) wakati akizungumza nao leo.
Mhe. Juma Duni Haji (kulia), Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,  Mhe. Dkt. Binilith Mahenge (katikati), Naibu Waziri wa Maji na Balozi Celestine Mushy (kushoto), Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nguvu za Atomiki Duniani, Mhe. Yukiya Amano (hayupo pichani).
Mhe. Yukiya Amano (kulia), Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nguvu za Atomiki Duniani akimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani) wakati wa mazungumzo yao leo. Wengine katika picha ni Prof. Manase Selema (katikati), Mkurugenzi wa Divisheni ya Ulaya ya Shirika hilo na Bw. Conleth Brady, Msaidizi wa Mkurugenzi Mkuu.
Mhe. Membe akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Yukiya Amano mara baada ya mazungumzo yao.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.