Friday, February 22, 2013

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI




TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Mkutano wa kwanza wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Oman (Joint Permanent Cooperation), tarehe 24 hadi 25 Februari, 2013

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb), anatarajiwa kufungua Mkutano wa Kwanza wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Oman (Joint Permanent Cooperation), tarehe 24 Februari, 2013 katika Hoteli ya Hyatt Regency (Kilimanjaro) iliyopo Dar es Salaam.

Mkutano huo pia utahudhuriwa na Waziri anayeshughulikia Masuala ya Mambo ya Nje wa Oman, Mhe. Yousuf bin Alawi bin Abdullah anayetarajiwa kuwasili nchini Jumamosi tarehe 23 Februari, 2013 saa 11 kamili jioni kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere uliopo mjini Dar es Salaam. 

Mkutano huo unatokana na Makubaliano yaliyosainiwa tarehe 14 Oktoba 2009 kati ya nchi hizo mbili mjini Muscat, Oman.

Pamoja na mambo mengine, Mkutano huo utajadili masuala ya ushirikiano baina ya Tanzania na Oman katika Sekta za Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Nishati na Madini, Viwanda na Biashara, Elimu, Afya, Uwekezaji, Utamaduni na Habari.



Imetolewa na:

KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI,

WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA,

DAR ES SALAAM.

22 Februari, 2013.



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.