Friday, February 22, 2013

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI




TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Mkutano wa kwanza wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Oman (Joint Permanent Cooperation), tarehe 24 hadi 25 Februari, 2013

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb), anatarajiwa kufungua Mkutano wa Kwanza wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Oman (Joint Permanent Cooperation), tarehe 24 Februari, 2013 katika Hoteli ya Hyatt Regency (Kilimanjaro) iliyopo Dar es Salaam.

Mkutano huo pia utahudhuriwa na Waziri anayeshughulikia Masuala ya Mambo ya Nje wa Oman, Mhe. Yousuf bin Alawi bin Abdullah anayetarajiwa kuwasili nchini Jumamosi tarehe 23 Februari, 2013 saa 11 kamili jioni kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere uliopo mjini Dar es Salaam. 

Mkutano huo unatokana na Makubaliano yaliyosainiwa tarehe 14 Oktoba 2009 kati ya nchi hizo mbili mjini Muscat, Oman.

Pamoja na mambo mengine, Mkutano huo utajadili masuala ya ushirikiano baina ya Tanzania na Oman katika Sekta za Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Nishati na Madini, Viwanda na Biashara, Elimu, Afya, Uwekezaji, Utamaduni na Habari.



Imetolewa na:

KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI,

WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA,

DAR ES SALAAM.

22 Februari, 2013.



Wednesday, February 20, 2013

Rais Mwai Kibaki wa Kenya awasili nchini kwa ziara ya siku mbili


Ndege iliyombeba Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Mwai Kibaki ikiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere huku Viongozi na Wanachi waliofika kumpokea wakishangilia kuwasili kwa Rais huyo nchini. Mhe. Rais Kibaki yupo nchini kwa ziara ya kitaifa ya siku mbili.
Mhe. Rais Kibaki akiteremka kwenye ndege mara baada ya kuwasili ambapo alipokelewa na mwenyeji wake Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Gwaride la Heshima wakati wa mapokezi hayo.

Mhe. Rais Kibaki akielekea kukagua Gwaride la Heshima.


Mhe. Rais Kibaki akikagua Gwaride la Heshima.
 Mhe. Rais Kibaki akiwa na mwenyeji wake Mhe. Rais Kikwete mara baada ya kukagua Gwaride la Heshima.
Mhe. Rais Kibaki pamoja na mwenyeji wake Mhe. Rais Kikwete wakifurahia burudani ya kikundi cha utamaduni kilichokuwepo Uwanjani hapo wakati wa mapokezi
Mhe. Rais Kibaki akiwa na Mhe. Rais Kikwete wakiondoka Uwanjani hapo mara baada ya mapokezi.

Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) (kushoto), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwa na Mhe. Sam Ongeri, Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya wakielekea Hotelini kwa mazungumzo mara baada ya mapokezi ya Mhe. Rais Kibaki.

Rajoelina upbeat on AU Sanctions



Hon. Bernard K. Membe (MP), Minister for Foreign Affairs and International Co-operation (left), hand-delivers a special message to H.E. Andry Rajoelina, President of the Transition Government of Madagascar yesterday in the State House located in Antananarivo City. Minister Membe was in Madagascar as a Government Special Envoy to hand-deliver a special message on behalf of President Jakaya Mrisho Kikwete of the United Republic of Tanzania.

Hon. Membe (2nd left), in discussion with President Rajoelina. Also in the photo are Ambassador Liberata Mulamula (left), Senior Advisor (Diplomatic Affairs) to President Kikwete and interpreter (2nd right).

Hon. Membe holds a press conference after his meeting with President Rajoelina of the Transitional Government of Madagascar.

Hon. Membe in discussion with Mr. Andriatina Jacques Ulrich, Acting Minister of Foreign Affairs in Madagascar.

Hon. Membe in discussion with Acting Foreign Minister of Madagascar, Mr. Andriatina Jacques Ulrich (right) and Ambassador Mulamula.

Hon. Bernard K. Membe (MP) (2nd left), Minister for Foreign Affairs and International Co-operation in a group photo with Mr. Andriatina Jacques Ulrich (left), Acting Minister for Foreign Affairs in Madagascar. Others in the photo are Mr. Mkwizu of the President's Office (right), Mr. Stephen Wambura (2nd right), SADC Liaison Officer (Tanzania) in Madagascar, Mr. Nicodemus Mwangela (3rd right), SADC Liasion Officer (Tanzania) in Madagascar and Mr. Afonso Evaristo Eduardo (3rd left - behind), Liaison Officer (Angola) in Madagascar.



Rajoelina upbeat on AU Sanctions

By TAGIE DAISY MWAKAWAGO

Antananarivo, Madagascar

President of Transitional Government of Madagascar, Andry Rajoelina has appealed to the international community, essentially the AU and SADC to remove the sanctions imposed on his transitional government.

He made such a profound request yesterday when he met with Hon. Bernard K. Membe (MP), the Minister for Foreign Affairs and International Co-operation, in his State House located in Antananarivo City. Minister Membe was in Madagascar as a Government Special Envoy to hand-deliver a Special Message on behalf of President Jakaya Mrisho Kikwete of the United Republic of Tanzania.

Speaking to the reporters after the meeting, Hon. Membe said that the message he carried from President Kikwete was a follow up on the development of transitional government in Madagascar, as it prepares for the upcoming Presidential elections. He further noted that President Kikwete wanted to know the outcome of discussion between President Rajoelina and the United Nations’ Secretary General Ban Ki moon in their recent meeting this year.

President Kikwete currently serves a Chairperson of the Southern Africa Development Community (SADC –Troika), after inheriting the Chairmanship from South Africa last August 2012.

On his part, President Rajoelina appealed to President Kikwete to assist in lifting any and all sanctions imposed upon his transitional government and for perpetrating the status quo. Other sanctions targeted the 109 accomplices and confidants of President Rajoelina for their involvement in the 2009 coup d’etat. He explained that the conditions set in the roadmap by the international community have been fully implemented.

Further, President Rajoelina availed the commitment of his transitional government to see a democratic election takes place in July 2013.

In his response, Minister Membe said that the removal of sanctions is not conditional to the return of Marc Ravalomanana, former President of the Republic of Madagascar. “The roadmap is for SADC-Troika to see that the upcoming elections will be fair and profound for the people of Madagascar,” said Hon. Membe.

The sanctions in question were imposed by the African Union and supported by the Southern Africa Development Cooperation (SADC) and the International Community.

Minister Membe further explained that President Rajoelina informed him that his transitional government has fulfilled its obligation as mandated by AU, which included his withdrawal of presidential candidacy in the upcoming elections in July of this year. Others are storing peace and normalcy back in the country in preparation for the democratic election later this year.

Hon. Membe led the Tanzania delegation that included Ambassador Liberata Mulamula, Senior Advisor (Diplomatic Affairs) to President Kikwete, Mr. Mkwizu of the President’s Office, Mr. Assah Mwambene, Director of Information in the Ministry of Communication, Youth, Culture and Sports and other Governmental officials. For the Madagascar’s part, the delegation was led by President Rajoelina, Mr. Andriatina Jacques Ulrich, Acting Minister for Foreign Affairs and other transitional government officials.

Hon. Membe is expected to return back in Dar es Salaam later today.


Tuesday, February 19, 2013

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI




TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Mwai Kibaki anatarajia kuwasili nchini tarehe 20 Februari, 2013 kwa ziara ya kitaifa ya siku mbili. Ziara hiyo ya Mhe. Rais Kibaki inafuatia mwaliko wa Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Aidha, ziara ya Mhe. Rais Kibaki inafanyika kufuatia ziara ya Mhe. Rais Kikwete nchini Kenya mwezi Septemba, 2012.

Mhe. Rais Kibaki ambaye anatarajiwa kuwasili katika  Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere tarehe 20 Februari, 2013 saa 9.00 alasiri, atapokelewa na mwenyeji wake, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete.

Akiwa hapa nchini, Mhe. Rais Kibaki atafanya mazungumzo rasmi na Mhe. Rais Kikwete tarehe 20 Februari 2013 kabla ya kushiriki katika Dhifa ya Kitaifa itakayoandaliwa kwa heshima yake na Mhe. Rais Kikwete, Ikulu, Dar es Salaam.

Mhe. Rais Kibaki anatarajiwa pia kukutana na  Wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam tarehe 21 Februari, 2013, kuzindua Barabara ya Mwai Kibaki na kutembelea Gereza Kuu la Ukonga Jijini Dar es Salaam ili kujionea shughuli mbalimbali zinazolenga kuwarekebisha Wafungwa kuwa Raia wema na kuwapa mafunzo ya kiufundi kuwawezesha kujitegemea wanapomaliza vifungo vyao. Shughuli hizo ni pamoja na  ushonaji, useremala na kilimo cha kisasa.

Mhe. Rais Kibaki ataondoka nchini tarehe 21 Februari, 2013 kurejea nchini kwake.

IMETOLEWA NA: WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA, DAR ES SALAAM.
19 FEBRUARI, 2013




Mhe. Mahadhi akutana na Msajili wa Mahakama ya ICTR

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) akizungumza na Msajili Mpya wa Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR) ya Jijini Arusha, Mhe. Bongani Majola (hayupo pichani) wakati Msajili huyo alipofika Wizarani kwa mazungumzo na Mhe. Mahadhi  juu ya masuala mbalimbali kuhusu Mahakama hiyo.

Mhe. Mahadhi (kulia) akiendelea na mazungumzo na Mhe. Bongani Majola, Msajili Mpya wa Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR) alipofika Ofisini kwa Mhe. Mahadhi kwa mazungumzo.

Mhe. Mahadhi akifafanua jambo kwa Mhe. Majola wakati wa mazungumzo yao. Wengine katika picha ni wajumbe waliofuatana na Mhe. Majola. Kulia ni Bw. Roland Konassi Amoussouga ambaye ni Mshauri Mwandamizi wa Sheria na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mipango wa ICTR na kushoto ni Bw. Jerry Mburi, Afisa Sheria na Utawala wa ICTR.

Mhe. Majola akiendelea na mazungumzo na Mhe. Mahadhi.
Mhe. Mahadhi na Wajumbe wengine wa ICTR wakimsikiliza Mhe. Majola.

Mhe. Mahadhi akimsikiliza Bw. Amoussouga alipokuwa akifafanua jambo.

Mhe. Majola (kulia) na Bw. Mburi wakimsikiliza mwenzao Bw. Amoussouga (hayupo pichani) alipokuwa anafafanua jambo kwa Mhe. Mahadhi (naye hayupo pichani)

Bw. Benedict Msuya (kulia), Afisa kutoka Kitengo cha Sheria, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akinukuu mazungumzo kati ya Mhe. Mahadhi na ujumbe kutoka ICTR. Mwingine katika picha ni Bw. Amoussouga mmoja wa wajumbe kutoka ICTR.

Mhe. Mahadhi akiagana na Mhe. Majola mara baada ya mazungumzo yao.

Mhe. Mahadhi akifurahia jambo na Bw. Amoussouga wakati wa kuagana.

UTEUZI WA BODI YA CHUO CHA DIPLOMASIA




TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Balozi Mwanaidi Sinare Maajar kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Diplomasia (CFR) kilichopo Kurasini Jijini Dar es Salaam.

Aidha, kufuatia uteuzi huo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Kamillius Membe (Mb.) amewateua Wajumbe wa Bodi hiyo kuwa ni:-

1.           Bw. Dushhood M. K. Mndeme
2.           Mhe. Balozi Abdi Mshangama
3.           Mhe. Dkt. Leonidas Mushokolwa
4.           Mhe. Dkt. Harold Utouh
5.           Mhe. Saidi Mtanda (Mb.)
6.           Mhe. Betty Machangu (Mb.)
7.           Bw. Affan Othman Maalim
8.           Bw. Abdurahaman Abdallah

Uteuzi wa Mwenyekiti na Wajumbe hao ni kwa kipindi cha miaka mitatu (3) kuanzia tarehe 22 Januari, 2013 hadi tarehe 21 Januari, 2016.

   
IMETOLEWA NA: WIZARA YA MAMBO YA NJE NA

USHIRIKIANO WA KIMATAIFA, DAR ES SALAAM


15 FEBRUARI, 2013

Saturday, February 16, 2013

Nchi za EAC zasaini Itifaki ya Amani na Usalama





Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), akiweka saini Itifaki ya Amani na Usalama ya Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC). Uwekaji saini huo ulifanyika katika Hoteli ya New Africa, jijini Dar es Salaam.


Mhe. Membe (wa pili kushoto) akiwa na viongozi wenzake wa nchi za EAC wakiwa wameshikilia Itifaki hiyo mara baada ya kusainiwa

Mhe. Membe akipitia Itifaki hiyo kabla ya kusainiwa huku Bw. John M. Haule, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akishuhudia.
Mhe. Membe akijadiliana jambo na Katibu Mkuu wake Bw. Haule. Mwingine katika picha ni Mhe. Pereira Ame Silima (Mb.), Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi.

Picha nyingine ya Mhe. Membe na Katibu Mkuu wake Bw. Haule na wajumbe wengine waliohudhuria mkutano huo.

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dkt. Richard Sezibera (kulia) akijadiliana jambo na Waziri wa Ulinzi wa Uganda.

Mhe. Membe akifanya mahojiano na Waandishi wa Habari baada ya shughuli ya utiaji saini kukamilika.

Picha zaidi za mahojiano kati ya Mhe. Membe na Waandishi wa Habari.














Friday, February 15, 2013

Waziri Membe akutana na Uongozi wa APRM Tanzania

Mhe Waziri leo amekutana na uongozi wa APRM Tanzania. Ujumbe huo chini ya Mwenyekiti Prof. Hassa Mlawa, umetumia fursa hiyo kumshukuru Mhe. Waziri Membe kwa ushirikiano alioutoa yeye kama Focal Point wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wizara kwa ujumla, ikiwemo kulipwa kwa deni la muda mrefu la mchango wa Tanzania katika Sekretariati ya APRM na kuliondolea taifa aibu. Aidha, Ujumbe huo ulitumia fursa hiyo kumueleza Mhe. Waziri juu ya hatua zinazofuata katika utekelezaji wa yatokanayo na Ripoti ya Tathmini ya Tanzania.
Mhe. Membe alipongeza Uongozi wa APRM kwa kazi nzuri waliyoifanya kwa uadilifu mkubwa na kuiletea Tanzania heshima. Ametumia fursa hiyo kuwahakikishia ushirikiano wa Wizara yake katika kuratibu utekelezaji wa yatokanayo na Ripoti hiyo.
Amewataka APRM kusambaza taarifa hiyo kwa wananchi na wadau wote kwa kuwa taarifa hiyo ni ya umma.


Wednesday, February 13, 2013

Courtesy visit of Indonesian Ambassador to Tanzania


Ambassador Mbelwa Kairuki (right), Director of the Department of Asia and Australasia in a discussion with H.E. Zakaria Anshar, the new Ambassador of the Republic of Indonesia to the United Republic of Tanzania.  

H.E. Ambassador Anshar paid a courtesy visit earlier today, with the purpose to explain his Country's desire to increase technical cooperation in various sectors in the coming years.  For a long time now, Indonesia has been actively involved in developing agriculture sector and providing training programs for farmers in Tanzania. 

Ambassador Kairuki explains how Tanzania has benefited from Indonesia's support in its training programs especially in agricultural field and expressed the Government's commitment to continue economic cooperation with Indonesia.

Ambassador Kairuki (center) in a discussion with Ambassador Anshar of Indonesia earlier today in his office.  Also in the photo is Mr. Charles Faini, Foreign Service Officer in the Ministry of Foreign Affairs.

Ambassador Kairuki, Director of the Department of Asia and Australasia and H.E. Ambassador Anshar of the Republic of Indonesia to Tanzania shake hands at the end of their discussion, solidifying the lasting, friendly relation that exist between the two countries.


Photos by Tagie Daisy Mwakawago 




Kikao cha wadau cha maandalizi ya mkutano wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Oman chafanyika

Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya (katikati) akipitia kumbukumbu wakati akiongoza kikao cha Wadau cha maandalizi ya Mkutano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Oman unaotarajiwa kufanyika Jijini Dar es Salaam tarehe 24 na 25 Februari, 2013. Wengine katika picha ni Balozi Bertha Semu-Somi (kulia), Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Bw. Elibariki Maleko, Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Mashariki ya Kati.
Baadhi ya wadau waliohudhuria kikao hicho wakimsikiliza mwenyekiti (hayupo pichani)
Wadau wengine wakati wa kikao hicho.