Tuesday, June 24, 2014

Mhe. Rais amwapisha Balozi Sokoine

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akimwapisha Balozi Joseph Edward Sokoine ambaye pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Hafla hiyo ilifanyika, Ikulu, Dar es Salaam tarehe 24 Juni, 2014 
Wakurugenzi Wasaidizi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa nao walikuwepo kushuhudia kuapishwa kwa Balozi Sokoine. Kutoka kulia ni Bibi Victoria Mwakasege, Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Ulaya na Amerika, Bw. Innocent Shiyo, Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Ulaya na Amerika

Balozi Sokoine akisaini hati ya kiapo mbele ya Mhe. Rais Kikwete
Wageni waalikwa wakishuhudia tukio hilo
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John Haule akisalimiana na Mama mzazi wa Balozi Sokoine ambaye alikuwepo kushuhudia tukio hilo.
Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Balozi Sokoine pamoja na ndugu, jamaa na marafiki wa balozi huyo.
Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Sokoine, Katibu Mkuu Haule pamoja na Wakurugenzi na wajumbe wengine kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Picha na Reginald Philip



Balozi Sokoine apokelewa kwa shangwe Wizara ya Mambo ya Nje

Balozi Joseph Sokoine ambaye pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika akisalimiana na Naibu Balozi wa Tanzania nchini Uswisi,  Robert Kahendaguza huku Wafanayakazi wengine wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakishangilia mara baada ya Balozi Sokoine kuwasili Wizarani baada ya kuapishwa.
Balozi Sokoine akisalimiana na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Bi. Glory Mboya mara baada ya kuwasili Wizarani baada ya kuapishwa.


Balozi Sokoine akisalimiana kwa furaha na Bw. Kelvin Kheri mmoja wa Wafanayakazi Wizarani.

Mapokezi yakiendelea.

Balozi Sokoine akisalimiana na Wafanyakazi wa Wizara walipompokea kwa furaha 
Balozi Sokoine akiwa ameongozana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John Haule (katikati) pamoja na Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria, Balozi Irene Kasyanju mara baada kuwasili.

Picha na Reginald Philip



Monday, June 23, 2014

Makamu wa Rais wa China afungua rasmi Kongamano la Uwekezaji

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe Li Yuanchao akifungua rasmi Kongamano la Pili la Uwekazaji kati ya Tanzania na China. Ufunguzi wa Kongamano hilo ulifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Benki Kuu ya Tanzania Jijini Dar es Salaam tarehe 23 Juni, 2014. Ufunguzi huo ulihudhuriwa pia na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Pinda, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji na Uwekezaji, Mhe. Mary Nagu, Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Abdallah Kigoda, Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Bi. Julieth Kairuki, Viongozi mbalimbali kutoka Serikalini na Taasisi Binafsi na wadau mbalimbali.
Wajumbe mbalimbali wakifurahia hotuba ya ufunguzi ya  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Li Yuanchao (hayupo pichani).
Mhe. Pinda, Mawaziri na wajumbe wengine wakimsikiliza Makamu wa Rais wa China, Mhe. Li Yuanchao (hayupo pichani) alipokuwa akifungua Kongamano la Uwekezaji kati ya Tanzania na China
Wajumbe wakifuatilia ufunguzi
Mhe. Li Yuanchao (wa tatu kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na  Mhe. Pinda (mwenye tai nyekundu), Mhe. Nagu (wa pili kushoto), Mhe. George Mkuchika (wa kwanza kushoto), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utawala Bora, Balozi wa China nchini, Mhe. Lu Youqing (wa kwanza kulia) na Bi. Kairuki. Mkurugenzi wa TIC.
Picha ya pamoja na Wajumbe wa Kongamano

Picha na Reginald Philip

Sunday, June 22, 2014

Makamu wa Rais wa China awasili nchini kwa ziara ya kikazi



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Mohammed Gharib Bilal akimlaki kwa furaha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Li Yuanchao mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 22 Juni, 2014 kwa ajili ya kuanza rasmi ziara yake ya kikazi  ya siku tano hapa nchini.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Li Yuanchao akisalimiana na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Irene Kasyanju aliyekuwepo Uwanjani hapo kwa ajili ya mapokezi ya Makamu huyo wa Rais.
Mhe. Li Yuanchao akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mbelwa Kairuki mara baada ya kuwasili Jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa China Mhe. Li Yuanchao akipita  katikati ya Gwaride la Heshima wakati wa mapokezi yakehuku  akisindikizwa na Mwenyeji wake Mhe. Dkt. Bilal.
Mhe. Li akifurahia kikundi cha burudani kilichokuwa uwanjani hapo (hawapo pichani) wakati wa mapokezi yake.
Moja ya vikundi vya burudani vikitumbuiza wakati wa mapokezi ya Makamu wa Rais wa China alipowasili hapa nchini.
Picha na Reginald Philip

Friday, June 20, 2014

Waziri Membe azungumza na Balozi wa Oman nchini


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard K. Membe (Mb), akimkaribisha ofisini kwake Balozi wa Oman nchini Tanzania, Mhe. Soud Al Mohammed Al-Ruqaish alipofika kwa ajili ya mazungumzo yaliyojikita katika kuimarisha mahusiano kati ya nchi hizi mbili mapema leo tarehe 20 Juni, 2014, Jijini Dar es Salaam.
Waziri Membe akifafanua jambo wakati wa mazungumzo na Balozi wa Oman nchini
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga na Afisa Mambo ya Nje, Batholomeo Jungu wakifuatilia mazungumzo kati ya Mhe. Membe na Balozi wa Oman  hapa nchini (hawapo pichani)
Waziri Membe pamoja na Balozi wa Omani wikifurahia jambo wakati wa mazungumzo yao wa kwanza kushoto ni Afisa aliyeambatana na na Balozi wa Oman.
Picha ya pamoja.


Picha na Reginald Philip



Thursday, June 19, 2014

Balozi mpya wa Marekani nchini ajitambulisha rasmi kwa Waziri Membe


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akimkaribisha kwa furaha na kwa mara ya kwanza ofisini kwake Balozi wa Marekani hapa nchini, Mhe. Mark Childress alipofika e kwa ajili ya kujitambulishana pia kuzungumzia masuala ya ushirikiano kati ya Tanzania na Marekani.
Mhe. Membe na Mhe. Childress katika picha ya pamoja.
Mhe. Childress akisaini Kitabu cha Wageni alipowasili Ofisini kwa Mhe. Membe
Mhe. Membe na Balozi Childress wakiwa katika mazungumzo
Mhe. Childress na ujumbe aliofuatana nao wakimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani)
Picha ya pamoja kati ya Mkhe. Membe na Mhe. Childress pamoja na Maafisa kutoka Ubalozi wa Marekani na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga (wa kwanza kulia).

Waziri Membe akutana kwa mazungumzo na Mabalozi wa China, Cuba, Japan, Msumbiji na Kaimu Balozi wa Ujerumani

......Mkutano wa Mhe. Membe na Balozi wa China


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akimkaribisha Ofisini kwake Balozi wa China hapa nchini,  Mhe. Lu Youqing alipofika kwa ajili ya mazungumzo ambayo yalihusu pia ziara ya Makamu wa Rais wa China atakayoifanya hapa nchini kuanzia tarehe 21 hadi 26 Juni, 2014.
Mhe. Balozi Lu akimweleza jambo Mhe. Membe wakati wa mazungumzo yao.
Mkurugenzi Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akifuatilia mazungumzo kati ya Mhe. Membe na Balozi LU (hawapo pichani)

 Mkutano wa Mhe. Membe na Balozi wa Cuba

Mhe. Waziri akimkaribisha Ofisini kwake Balozi wa Cuba hapa nchini, Mhe. Jorge Luis Lopez Tormo alipofika kwa ajili ya mazungumzo kuhusu kuimarisha ushrikiano kati ya Tanzania na Cuba. Tanzania na Cuba zinashirikiana katika sekta mbalimbali ikiwemo elimu, afya na siasa.
Mhe. Membe akimsikiliza kwa makini Balozi Tormo.

Mazungumzo yakiendelea huku Afisa Mambo ya Nje, Bw. Lucas Mayenga akinukuu.

Mkutano wa Mhe. Membe na Balozi wa Japan

Mhe. Membe akimkaribisha ofisini kwake Balozi wa Japan hapa nchini Mhe. Masaki Okada alipofika kwa ajili ya mazungumzo kuhusu kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Japan.

Mhe. Balozi Okada akifafanua jambo wakati wa mazungumzo yake na Mhe. Membe.

Mkurugenzi Msaidizi katika Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Nathaniel Kaaya akifuatili mazungumzo kati ya Mhe. Membe na Mhe. Okada (hawapo pichani)

Mkutano wa Mhe. Membe na Kaimu Balozi wa Ujerumani

Mhe. Membe akimkaribisha ofisini kwake Kaimu Balozi wa Ujerumani hapa nchini, Bw. Hans Koeppel alipofika kwa mazungumzo na Mhe. Waziri  kuhusu salamu za shukrani kwa Serikali ya Tanzania kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, Mhe. Frank-Walter Steinmeir kufuatia ziara yake ya mafanikio aliyoifanya hapa nchini mwezi Machi 2014

Mhe. Membe akipokea barua ya salamu hizo kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga akifuatilia mazungumzo kati ya Mhe. Membe na Kaimu Balozi wa Ujerumani hapa nchini (hawapo pichani)

Mkutano wa Mhe. Membe na Balozi wa Msumbiji

Mhe. Membe akizungumza na Balozi wa Msumbiji hapa nchini, Mhe. Vicente M. Veloso alipofika ofisini kwake kwa mazungumzo kuhusu kuimarisha ushirikiano kati ya nchi hizi mbili.
Balozi Veloso na ujumbe aliofuatana nao wakimsikiliza Mhe. Membe alipozungumza nao.

Press Release

Queen Elizabeth II


PRESS RELEASE
H.E Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to her Majesty Queen Elizabeth II on the occasion of her 88th birthday.

The message reads as follows:-
“Your Majesty Queen Elizabeth II,
Buckingham Palace,
London,
UNITED KINGDOM.

On behalf of the people and the Government of the United Republic of Tanzania, I extend sincere congratulations on the occasion of your 88th birthday.

As you celebrate your birthday allow me to take this opportunity to express my appreciation on the good relations that exist between our two countries and peoples.

The celebration of your birthday offers us yet another opportunity to reaffirm our commitment to continue working closely together in strengthening further the relations between our two countries.

Please accept, Your Majesty, my best wishes for your continued good health and peace and prosperity for the people of the United Kingdom.”

Issued by the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation, Dar es Salaam

18th June 2014


Wednesday, June 18, 2014

Makamu wa Rais atembelea mradi wa Dubai Sports City

Makamu wa Rais Dk. Mohamed Ghalib Bilali, leo ametembelea mradi mpya wa Dubai Sports City, kujionea ramani ya mradi huo mkubwa wa kijiji cha michezo cha Dubai. kulia kwa makamu wa Rais, ni Bw. MOhamed Sharif, Mtanzania ambaye ni mtendaji Mkuu wa Mradi wa Dubai Sports City, na kushoto ni Balozi Mdogo Dubai, Omar Mjenga 

Ujumbe ulio ambatana na Makamu wa Rais nao wakitazama ramani ya mradi huo.