Tuesday, June 24, 2014

Mhe. Rais amwapisha Balozi Sokoine

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akimwapisha Balozi Joseph Edward Sokoine ambaye pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Hafla hiyo ilifanyika, Ikulu, Dar es Salaam tarehe 24 Juni, 2014 
Wakurugenzi Wasaidizi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa nao walikuwepo kushuhudia kuapishwa kwa Balozi Sokoine. Kutoka kulia ni Bibi Victoria Mwakasege, Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Ulaya na Amerika, Bw. Innocent Shiyo, Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Ulaya na Amerika

Balozi Sokoine akisaini hati ya kiapo mbele ya Mhe. Rais Kikwete
Wageni waalikwa wakishuhudia tukio hilo
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John Haule akisalimiana na Mama mzazi wa Balozi Sokoine ambaye alikuwepo kushuhudia tukio hilo.
Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Balozi Sokoine pamoja na ndugu, jamaa na marafiki wa balozi huyo.
Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Sokoine, Katibu Mkuu Haule pamoja na Wakurugenzi na wajumbe wengine kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Picha na Reginald Philip



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.