Thursday, June 12, 2014

Mhe. Membe akutana na Mhe. Mark Simmonds Waziri wa Uingereza anayeshughulikia maswala ya Afrika

Mhe. Bernard K. Membe, Waziri wa Mambo ya Nje na

Ushirikiano wa Kimataifa akiwa kwenye mazungumzo na

Mhe. Mark Simmonds, Waziri wa Uimgereza

anayeshughulikia masuala ya Afrika kwenye Wizara ya

Mambo ya Nje ya Uingereza leo tarehe 11 Juni 2014.

Pamoja na mambo mengine, Mawaziri hao wamezungumzia

maazimio ya Mkutano wa Kimataifa kuhusu Ukomeshwaji

wa Udhalilishaji wa kijinsia kwenye maeneo yenye

Migogoro (''End Sexual Violence in Conflict") unaoendelea

mjini London, Uingereza. Tanzania inashiriki Mkutano huo

kufuatia mualiko wa Serikali ya Uingereza kutokana na

mchango mkubwa wa Tanzania katika kufanikisha kuwepo

kwa Tamko la Umoja wa Mataifa linalo husu suala hilo

(Declaration of Commitment to End Sexual Violence in

Conflict).  


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.