Friday, June 6, 2014

Waziri Mwandamizi wa Mambo ya Nje na Ndani wa Singapore ziarani nchini

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) akifafanua jambo wakati wa mazungumzo yake na Waziri Mwandamizi anayeshughulikia Mambo ya Nje na Ndani wa Jamhuri ya Singapore, Mhe. Masagos Zulkifli ambaye yupo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tano. Katika mazungumzo yao walisisitiza kuimarisha ushirikiano katika masuala mbalimbali ikiwemo utalii, uchukuzi  na uwekezaji.
Mhe. Zulkifli naye akizungumza wakati wa mkutano wake na Mhe. Dkt. Maalim.

Balozi wa Tanzania nchini India anayewakilisha pia nchini Singapore, Mhe. John Kijazi (kushoto) pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Nathaniel Kaaya wakifuatilia mazungumzo kati ya Mhe. Maalim na Mhe. Zulkifli (hawapo pichani)
Bw. Adam Isara (kushoto), Katibu wa Naibu Waziri na Bw. Khatib Makenga, Afisa Mambo ya Nje wakifuatilia mazungumzo
Mhe. Dkt. Maalim akimsindikiza Mhe. Zulkifli na ujumbe wake mara baada ya mazungumzo yao
Mhe. Dkt. Maalim akiagana na Mhe. Zulkifli.



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.