Monday, June 23, 2014

Makamu wa Rais wa China afungua rasmi Kongamano la Uwekezaji

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe Li Yuanchao akifungua rasmi Kongamano la Pili la Uwekazaji kati ya Tanzania na China. Ufunguzi wa Kongamano hilo ulifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Benki Kuu ya Tanzania Jijini Dar es Salaam tarehe 23 Juni, 2014. Ufunguzi huo ulihudhuriwa pia na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Pinda, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji na Uwekezaji, Mhe. Mary Nagu, Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Abdallah Kigoda, Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Bi. Julieth Kairuki, Viongozi mbalimbali kutoka Serikalini na Taasisi Binafsi na wadau mbalimbali.
Wajumbe mbalimbali wakifurahia hotuba ya ufunguzi ya  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Li Yuanchao (hayupo pichani).
Mhe. Pinda, Mawaziri na wajumbe wengine wakimsikiliza Makamu wa Rais wa China, Mhe. Li Yuanchao (hayupo pichani) alipokuwa akifungua Kongamano la Uwekezaji kati ya Tanzania na China
Wajumbe wakifuatilia ufunguzi
Mhe. Li Yuanchao (wa tatu kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na  Mhe. Pinda (mwenye tai nyekundu), Mhe. Nagu (wa pili kushoto), Mhe. George Mkuchika (wa kwanza kushoto), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utawala Bora, Balozi wa China nchini, Mhe. Lu Youqing (wa kwanza kulia) na Bi. Kairuki. Mkurugenzi wa TIC.
Picha ya pamoja na Wajumbe wa Kongamano

Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.