Tuesday, June 24, 2014

Balozi Sokoine apokelewa kwa shangwe Wizara ya Mambo ya Nje

Balozi Joseph Sokoine ambaye pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika akisalimiana na Naibu Balozi wa Tanzania nchini Uswisi,  Robert Kahendaguza huku Wafanayakazi wengine wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakishangilia mara baada ya Balozi Sokoine kuwasili Wizarani baada ya kuapishwa.
Balozi Sokoine akisalimiana na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Bi. Glory Mboya mara baada ya kuwasili Wizarani baada ya kuapishwa.


Balozi Sokoine akisalimiana kwa furaha na Bw. Kelvin Kheri mmoja wa Wafanayakazi Wizarani.

Mapokezi yakiendelea.

Balozi Sokoine akisalimiana na Wafanyakazi wa Wizara walipompokea kwa furaha 
Balozi Sokoine akiwa ameongozana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John Haule (katikati) pamoja na Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria, Balozi Irene Kasyanju mara baada kuwasili.

Picha na Reginald Philip



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.