Tuesday, June 24, 2014

Makamu wa Rais wa China afungua Kongamano la Taasisi ya Utamaduni Barani Afrika na kuweka Jiwe la Msingi la Ubalozi wa China nchini

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mohamed Gharib Bilal akimkaribisha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Li Yuanchao katika Ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kufungua rasmi Kongamano la Pamoja kwa Taasisi za Confucius Barani Afrika. Taasisi ya Confucius  inajishughulisha na ukuzaji utamaduni na lugha mbalimbali za Afrika  na China ambapo kwa hapa nchini ina matawi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kile cha Dodoma.
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof. Rwekaza Mukandala akimkaribisha Mhe. Dkt. Bilal kuhutubia wajumbe waliohudhuria ufunguzi wa kongamano hilo.
Mhe. Dkt. Bilal akizungumza.

Wajumbe wakimsikiliza Mhe. Dkt. Bilal (hayupo pichani
Mhe. Li naye akizungumza

Mhe. Dkt. Bilal akimsikiliza Mhe. Li (hayupo pichani)

Vikundi vya burudani vikitumbuiza wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Pamoja kwa Taasisi za Confucius Barani Afrika. Juu ni kikundi cha ngoma kutoka Mkoa wa Dodoma na chini ni Vijana kutoka Chuo Kikuu cha UDOM wakionesha utamaduni wa Kichina wa Kung-Fu.
Mhe. Dkt. Bilal na Mhe. Li wakifurahia burudani zilizokuwa zikitolewa na vikundi mbalimbali (havipo pichani)
Picha ya pamoja.

......Uwekaji Jiwe la Msingi la Jengo la Ubalozi wa China nchini......

Mhe. Li akisalimiana na raia wa China wanaoishi hapa nchini kabla ya kuweka Jiwe la Msingi la Jengo la Ubalozi wa China hapa nchini
Mhe. Bilal na Mhe. Li kwa pamoja na wajumbe wengine wakichota mchanga kuashiria uwekaji wa Jiwe la Msingi la Jengo la Ubalozi wa China hapa nchini litakalojengwa katika Makutano ya Mtaa wa Sokoine na Shaaban Robert Jijini Dar es Salaam
Picha ya pamoja baada ya kuweka Jiwe la Msingi

Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.