Friday, April 17, 2015

Waziri Membe akabidhi Ujumbe Maalum wa Mhe. Rais kwenda kwa Sultani wa Oman

Mhe. Bernard K. Membe, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Tanzania akimkabidhi Mhe. Yousuf bin Alawi bin Abdulla, Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman Ujumbe Maalum kutoka kwa Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenda  kwa Mhe. Sultani Qaboos bin Said Al Said, Mtawala wa Oman. Mhe. Membe alifanya ziara ya kikazi ya siku mbili nchini humo
Makabidhiano yakiendelea huku Balozi wa Tanzania nchini Oman, Mhe. Ali Ahmed Saleh akishuhudia. 
Waziri Membe akiwa kwenye mazungumzo na Mhe. Alawi bin Abdulla, Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman.

===========================================
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Ujumbe Maalum wa Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete kwenda kwa Sultan Qaboos wa Oman

Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa amekabidhi ujumbe maalum kutoka kwa Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenda kwa Mhe. Sultani Qaboos bin Said Al Said, Mtawala wa Oman.

Ujumbe huo maalum ulikabidhiwa kwa Mhe. Yousuf bin Alawi bin Abdulla, Waziri wa Mambo ya Nje na mwenyeji wa ziara ya Waziri Membe nchini Oman, kwenye ofisi za Wizara hiyo jijini Muscat, Oman Alhamisi Aprili 16, 2015.

Makabidhiano hayo ya kihistoria nchini hapa, yalishuhudiwa na Mhe. Dkt. Mwinyihaji Makame, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utawala Bora, Zanzibar , Mhe. Ali Ahmed Saleh, Balozi wa Tanzania Oman, na viongozi wengine wa nchi zote mbili na waandishi wa habari.

Baada ya makabidhiano, viongozi hao wawili na ujumbe wao walitumia fursa hiyo kuzungumzia masuala mbalimbali ya ushirikiano baina ya Tanzania na Oman.

Viongozi hao waliahidi kukuza uhusiano na utamaduni wa nchi hizi mbili ambao unafanana kwa sababu za kihistoria. Mhe. Membe alimuelezea mwenyeji wake nia ya Serikali kujenga Ofisi za Ubalozi  kwenye kiwanja chake hapa Mascut kama sehemu ya utekelezaji wa mpango wa kuwa na majengo ya Tanzania kwenye nchi mbalimbali duniani.

Aidha mradi mkubwa wa bandari ya Bagamoyo pia ulizungumzwa na viongozi hao ambapo Serikali ya Oman ni mojawapo ya mdau wa mradi huo. Wahusika wengine wa mradi wa Bandari ya Bagamoyo ni Serikali ya China na Tanzania.

Mhe. Yousuf bin Alawi bin Abdulla, Waziri wa Mambo ya Nje wa Omani alimuhakikishia mgeni wake ushirikiano wa Serikali yake kwenye hatua zote hizi muhimu za kuendeleza na kukuza uhusiano wa muda mrefu wa nchi hizi mbili.

-Mwisho-

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,
Dar es Salaam
17 Aprili 2015


Thursday, April 16, 2015

Serikali kuwarudisha nchini Watanzania waliopo Yemen


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akiwasili katika Hoteli ya Hyatt ya mjini Muscat, Oman mara baada ya kuwasili nchini humo kwa ajili ya kuanza ziara ya kikazi ya siku mbili. Wengine katika picha ni Balozi wa Tanzania, Oman, Mhe. Ali Ahmed Saleh (kulia) na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Afrika Mashariki katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Oman, Bw. Abdullah bin Said al-Riyami. Wakati wa ziara hiyo Mhe. Membe alitangaza azma ya Serikali kuwarudisha nchini Wanzania waliopo Yemen kufuatia machafuko yanayoendelea nchini humo.
Mhe.  Membe akiwa na Mhe. Ali Ahmed Saleh, Balozi wa Tanzania nchini Oman (kulia) na Bw. Abdullah bin Said al-Riyami, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Afrika Mashariki wakimsikiliza Bw. Fahad al-Bulushi, Afisa Itifaki wa ujumbe wa Mhe. Membe mara baada ya kuwasili nchini Oman.
========================================= 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Serikali kuwarudisha Watanzania waliopo Yemen

Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ametangaza hatua ya Serikali kuwarudisha Watanzania waishio nchini Yemen, kufutia mapigano yanayoendelea nchini humu ya vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Akizunguza na Mhe. Ali Ahmed Saleh, Balozi wa Tanzania nchini Oman siku ya Alhamis tarehe 16 Aprili 2015, Waziri Membe amesema ni jukumu la Serikali kuhakikisha kuwa Watanzania hao ambao wengi wao ni wanafunzi, wanarejea nyumbani salama.

Zoezi la kurudisha Watanzania hao lilianza siku chache zilizopita ambapo familia ya watu watano ilisaidiwa na kurudi nyumbani kupitia Oman, wakati zoezi la kuwatambua na kuwaandikisha Watanzania likenddelea.

“Nimeruhusu matumizi ya fedha ya dharura ili kuhakikisha ndugu zetu walioko kwenye hatari na machafuko ya Yemen wanarejeshwa salama nyumbani mara moja” alisema Mhe. Membe.

Watanzania hao ambao wengi wao hadi sasa wameshafika kwenye miji midogo ya Sarfat na Al-Mazyouna kwenye mkoa wa Salala mpakani mwa Oman na Yemen, walituma maombi ya dharura (distress call) kwenye Ofisi za Ubalozi Oman, kuelezea mazingira ya hatari yanayowakabili, na kuomba kurudishwa nyumbani.

“Kulingana na maelekezo ya Waziri Membe, zoezi la kuwarejesha Watanzania limeanza. Nimewapeleka maafisa wa ubalozi kule Salala ni kilometa takriban elfu moja kutoka Muscut, ambapo watahakiki na kukabidhiwa Watanzania wote sitini na nne (64) na wataruhusiwa kuingia nchini Oman na kuelekea Tanzania” alimaliza Mhe. Ali Ahmed Saleh, Balozi wa Tanzania nchini Oman.

Mgogoro wa Yemen unaoendelea baina ya maafisa wa polisi waaminifu kwa aliyekuwa rais wa nchi hiyo, Ali Abdullah Saleh, na makundi ya usalama yanayomuunga mkono rais wa sasa, Abed Rabbo Mansour Hadi, umeua mamia ya watu na kujerui maelfu.

Mhe. Membe ametoa rai kwa Watanzania wote wenye ndugu au jamaa nchini Yemen kuchukua tahadhari na kuwataarifu watafute msaada kupitia Ubalozini Muscat ili kujihakikishia usalama wao. Aidha ametoa tahadhari kwa Watanzania wanaotegemea kusafiri kwenda Yemen, kusitisha safari zao hadi hali ya usalama itakaporejea.

-Mwisho-

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,
Dar es Salaam
16 Aprili, 2015


Wednesday, April 15, 2015

Ziara ya Mhe. Membe Kuwait katika Picha

Msafara wa Mhe. Membe ukiingingia Mjini Kuwait kwa ziara ya siku moja kwa mwaliko wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Kuwait.


Mhe. Bernard Membe, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwasili kwene hoteli ya Sheraton Jijini Kuwait kwa ziara ya siku moja nchini humo.


Mhe. Membe na ujumbe wake wakimsikiliza Mhe. Balozi Najib na kuangalia picha  mbalimbali za historia ya Mji wa Kuwait mara baada ya kuwasili nchini humo kwa ziara ya siku moja. 

Waziri Membe akifuatiwa na Balozi Najeb na ujumbe wake wakiingia kwenye Ofisi za Mfuko wa Maendeleo wa Kuwait  kwa mazungumzo ya pamoja na viongozi wa mfuko huo tarehe 14 Aprili 2015.

Mhe. Bernard K. Membe, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwa na Mhe. Abdulwahab A. Al-Bader, Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Maendeleo wa Kuwait mara baada ya kuwasili ofisini kwake kwa mkutano.
Bw. Peter Noni, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo Tanzania (TIB) akimuonyesha Mhe. Abdulwahab A. Al-Bader kazi zinazofanywa na benki yake kwa ajili ya miradi ya maendeleo nchini Tanzania. 
Mazungumzo yakiendelea


Mhe. Membe akiagana na Mhe. Abdulwahab A. Al-Bader, mara baada ya mazungumzo hayo kumalizika. 

Msafara wa Waziri Membe ukielekea kwenye ofisi za Makamu wa Kwanza wa Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Kuwait (jengo refu la kwanza kushoto)

Waziri Membe akiwasili na mapokezi yakiendelea





Waziri Membe akitambulisha ujumbe wake kwa Mhe. Sheikh Sabah Al-Khalid Al-Sabah,  Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Kuwait mara baada ya kuwasili ofisini kwake kwa mkutano.

Mazungumzo yakiendelea



Ujumbe wa Mhe. Membe ulihudhuria pia chakula cha mchana pamoja na mwenyeji wake Mhe. Sheikh Sabah Al-Khalid Al-Sabah,  Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Kuwait


Waziri Membe akiagana na mwenyeji wake Mhe. Sheikh Sabah Al-Khalid Al-Sabah,  Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Kuwait.
Mhe. Membe akiagana na Balozi Najeb kwenye Uwanja wa Ndege wa Kuwait baada ya kukamilisha ziara yake nchini humo. 

Tanzania kufungua Ubalozi nchini Kuwait

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akizungumza na Mhe. Skeikh Sabah Al-Khalid Al-Sabah,  Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Kuwait. Waziri Membe alifanya ziara ya siku moja nchini humo tarehe 14 Aprili, 2015 kwa lengo la kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizi mbili.
Waziri Membe akimtambulisha kwa Mhe. Skeikh Sabah Al-Khalid Al-Sabah,  Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Kuwait Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya.
Waziri Membe akimtambulisha kwa Mhe. Skeikh Sabah Al-Khalid Al-Sabah,  Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Kuwait Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Uwekezaji Tanzania (TIB), Bw. Peter Noni. 
Mazungumzo ya ushirikiano yakiendelea
=======================================
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Tanzania kufungua Ubalozi nchini Kuwait

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepanga kufungua Ubalozi nchini Kuwait  kabla  ya kumalizika kwa mwaka huu wa fedha wa 2014/2015.

Kauli hiyo imetolewa   na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) alipokutana na  Mtukufu Sheikh Sabah Al-Khalid Al-Sabah,  Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Kuwait nchini Kuwait siku ya Jumanne tarehe 14 Aprili, 2015.

Katika mazungumzo yao viongozi hao wawili walisifu ushirikiano uliopo baina ya nchi hizi mbili ambao ni wa kidugu na unalenga kuwanufaisha wananchi wa nchi hizi.

“Kwa kufungua ofisi za Ubalozi, Kuwait ushirikiano huu wa kidugu utaongezeka kwenye nyanja zote muhimu na utazaa matunda yatakayo wanufaisha watu wetu, kwa nchi hizi mbili” alisisitiza Waziri Membe katika mazungumzo yake na kiongozi huyo.

Kwa upande wa Kuwait, Serikali yao ilifungua ubalozi nchini Tanzania Februari 2015 na Mhe. Jassem Ibrahim Al Najem kuwa Balozi wake wa kwanza nchini Tanzania, mwenye makazi yake Jijini Dar es salaam.

Aidha, kwa sasa Tanzania inawakilishwa nchini Kuwait kupitia Ubalozi wake uliopo Riyadh, Saudi Arabia.

Katika mkutano huo, Mtukufu Sabah Al-Khalid Al Sabah alisifu jitihada za Tanzania kwenye kulinda na kuleta amani Barani Afrika hasusan kwenye maeneo yenye migogoro. Alisema kuwa Serikali yake itaendelea kushirikiana na Tanzania sio tu kwenye maeneo muhimu ya maendeleo lakini pia hata kwenye ulinzi wa amani kwani ndio changamoto kubwa inayoikabili dunia kwa sasa.

Kuhusu misaada  Barani Afrika, viongozi hao walijadili suala la uratibu wa misaada mbalimbali ya Serikali ya Kuwait Barani humo ambapo waliangalia uwezekano wa kuanzisha kituo maalum nchini Tanzania kwa ajili ya kusimamia shughuli za uratibu wa misaada hiyo.

Kwa sasa Serikali ya Kuwait kupitia Mfuko wake wa Maendeleo – Kuwait Fund- imetoa Dola za Kimarekani Bilioni moja kwenye Umoja wa Afrika kwa ajili ya usalama wa chakula Barani Afrika.

Awali Waziri Membe alikutana na Mhe. Abdulwahab A. Al-Bader, Mkurugenzi wa Mfuko wa Maendeleo wa Kuwait na kumshukuru kwa misaada mbalimbali ya kimaendeleo wanayoendelea kuitoa nchini Tanzania na barani Afrika kwa ujumla.

Aidha Waziri Membe alielezea kuwa maandalizi ya miradi mitano ya umwagiliaji nchini Tanzania ambayo inayofadhiliwa na mfuko huo yamekamilika, na kwamba sasa iko tayari kuanza. Aidha Waziri Membe na Mhe. Al-Bader walizungumzia uwezekano wa mfuko huo kuikopesha Benki ya Uwekezaji Tanzania (TIB) ili iweze kuendesha shughuli zake kikamilifu.

Waziri Membe yuko nchini Kuwait kwa ziara ya siku moja na anatarajiwa kuondoka kesho kuelekea nchini Oman. Ujumbe wa Mhe. Membe  nchini Kuwait unamjumuisha Bw. Peter Noni, Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Uwekezaji Tanzania, Balozi Simba Yahya, Mkuregenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Bi. Mindi Kasiga, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Wizara ya Mambo ya Nje.

-Mwisho-

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Dar es Salaam

15 Aprili 2015.






H.E Mkapa delivers Lecture to Foreign Affairs Staff on Economic Partnership Agreement


Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania awasilisha mada kwa Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje


Waziri Membe awasili Nchini Kuwait

Mhe. Bernard Membe akiwasili hotelini nchini Kuwait kwa ziara ya siku moja ambapo atakutana na kufanya mzaungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Kuwait na Mkurugenzi Mkuu wa Kuwait Fund.
Mhe. Membe na ujumbe wake wakimsikiliza Mhe. Najib na kuangalia picha za viongozi mbalimbali wa Kuwait. 
Waziri Membe kwenye picha ya pamoja na baadhi na Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao kwenye nchi ya Kuwait na Tanzania. (Wa kwanza kushoto) ni Mhe. Prof. Abdillah Omari, Balozi wa Tanzania nchini Kuwait mwenye makazi yake Saudia Arabia na (kulia) ni Mhe. Nassem Ibrahim Al Najib, Balozi wa Kuwait nchini Tanzania.

Kamati ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar yatembelea Wizara ya Mambo ya Nje

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Rajab Gamah akifungua kikao  kati ya Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Kamati ya Kudumu ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar inayosimamia Ofisi za Viongozi za Kitaifa  kushoto ni Mwenyekiti wa Jimbo la Kwamtipura Mhe. Hamza Hassan Juma kulia ni Mwenyekiti wa Jimbo la Wawi, Mhe. Saleh Nassor Juma.  
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Baraza la Wawakilishi inayosimamia Ofisi za Viongozi wa Kitaifa wakimsikiliza Kaimu Katibu Mkuu, Balozi Gamaha (hayupo pichani)
 Kaimu Mkurugenzi wa Idara za Diaspora katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bibi Rosemary Jairo (kushoto) akiwa pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bi. Bictoria Mwakasege (katikati)  na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Bw. Elibariki Maleko  wakati wa kikao kati ya  Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Kamati ya Kudumu ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar.
Kikao kikiendelea.

Picha na Reginald Philip 

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje akutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Comoro

 Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb),akimkaribisha Wizarani Waziri wa Mambo ya Nje wa Muungano wa Visiwa vya Comoro, Mhe El-Anrif Said Hassane kwa mazungumzo ya kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Comoro.
Balozi wa Comoro hapa Nchini Mhe.Dr.Ahamada El Badaoui Mohamed(kushoto)akisalimiana na Naibu Waziri Dkt.Mahadhi huku Waziri wa Mambo ya Nje wa Comoro Mhe.El-Anrif Said Hassane(katikati) akishuhudia.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe.Dkt.Mahadhi Juma Maalim (Mb),akifurahia jambo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Comoro wakati wakiendelea na mazungumzo yao.
Katibu wa Naibu Waziri, Bw.Adam Misara (kulia) pamoja na Afisa Mambo ya Nje, Bw.Mudrick Soragha wakinukuu mazungumzo kati ya mhe. Mahadhi na Mhe. Hassane (hawapo pichani).
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe.Dkt.Mahadhi Juma Maalim (Mb),akifafanua jambo katika kikao hicho.

Picha na Reuben Mchome

Tuesday, April 14, 2015

Mkutano wa Waziri Membe na viongozi wa Kuwait Fund nchini Kuwait katika picha

Mhe. Bernard Membe, Waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Kimataifa akisalimiana na Mhe.  Abdulwahab A. Al-Bader, Mkurugenzi wa Mfuko wa Maendeleo wa Kuwait mara baada kuwasili ofisini kwake kwa mkutano leo tarehe 14 Aprili 2015.

Waziri Membe akiwatambulisha wajumbe alioongozana nao kwenye kikao hicho kilichofanyika Kuwait City leo Jumanne tarehe 14 Aprili 2015.


Kikao kikiendelea

Mhe.  Abdulwahab A. Al-Bader, Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Maendeleo wa Kuwait akipokea maelezo kuhusu Benki ya Maendeleo ya Tanzania kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo Bw. Peter Noni ambaye aliongozana na Mhe. Membe kwenye mkutano huo.




Mhe. Bernard Membe akiwa kwenye picha na Abdulwahab A. Al-Bader, Mkurugenzi wa Mfuko wa Maendeleo wa Kuwait (kati) pamoja na Balozi Yahya Simba, Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Wizara ya Mambo ya Nje.


Picha ya pamoja
Ujumbe wa Waziri Membe ukiondoka baada ya kumaliza mkutano na viongozi wa Mfuko wa Maendeleo wa Kuwait - Kuwait Fund.