Wednesday, April 15, 2015

Ziara ya Mhe. Membe Kuwait katika Picha

Msafara wa Mhe. Membe ukiingingia Mjini Kuwait kwa ziara ya siku moja kwa mwaliko wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Kuwait.


Mhe. Bernard Membe, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwasili kwene hoteli ya Sheraton Jijini Kuwait kwa ziara ya siku moja nchini humo.


Mhe. Membe na ujumbe wake wakimsikiliza Mhe. Balozi Najib na kuangalia picha  mbalimbali za historia ya Mji wa Kuwait mara baada ya kuwasili nchini humo kwa ziara ya siku moja. 

Waziri Membe akifuatiwa na Balozi Najeb na ujumbe wake wakiingia kwenye Ofisi za Mfuko wa Maendeleo wa Kuwait  kwa mazungumzo ya pamoja na viongozi wa mfuko huo tarehe 14 Aprili 2015.

Mhe. Bernard K. Membe, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwa na Mhe. Abdulwahab A. Al-Bader, Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Maendeleo wa Kuwait mara baada ya kuwasili ofisini kwake kwa mkutano.
Bw. Peter Noni, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo Tanzania (TIB) akimuonyesha Mhe. Abdulwahab A. Al-Bader kazi zinazofanywa na benki yake kwa ajili ya miradi ya maendeleo nchini Tanzania. 
Mazungumzo yakiendelea


Mhe. Membe akiagana na Mhe. Abdulwahab A. Al-Bader, mara baada ya mazungumzo hayo kumalizika. 

Msafara wa Waziri Membe ukielekea kwenye ofisi za Makamu wa Kwanza wa Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Kuwait (jengo refu la kwanza kushoto)

Waziri Membe akiwasili na mapokezi yakiendelea





Waziri Membe akitambulisha ujumbe wake kwa Mhe. Sheikh Sabah Al-Khalid Al-Sabah,  Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Kuwait mara baada ya kuwasili ofisini kwake kwa mkutano.

Mazungumzo yakiendelea



Ujumbe wa Mhe. Membe ulihudhuria pia chakula cha mchana pamoja na mwenyeji wake Mhe. Sheikh Sabah Al-Khalid Al-Sabah,  Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Kuwait


Waziri Membe akiagana na mwenyeji wake Mhe. Sheikh Sabah Al-Khalid Al-Sabah,  Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Kuwait.
Mhe. Membe akiagana na Balozi Najeb kwenye Uwanja wa Ndege wa Kuwait baada ya kukamilisha ziara yake nchini humo. 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.