Tuesday, April 28, 2015

Rais Kikwete amkaribisha Rais Clinton (Mstaafu) Ikulu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa ameambatana na Rais Mstaafu wa Marekani Mhe. Bill Clinton mara baada ya kuwasili Ikulu, na kufanya mazungumzo naye. Kushoto ni Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe (Mb.), ambaye pia alishiriki mazungumzo hayo. Rais Clinton yupo nchini kwa ziara binafsi ya siku tatu.  

Rais Kikwete akiwa katika Mazungumzo na Mhe. Clinton. Wa kwanza kulia ni waziri wa Mambo ya Nje na Ushikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard K. Membe ambaye alishiriki kwenye mazungumzo hayo pamoja na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Mhe. Dkt. Seif Suleiman Rashid (hayupo pichani)

Waziri wa Mambo ya Nje akiwa katika picha ya pamoja na Rais Mstaafu wa Marekani Mhe. Bill Clinton, Ikulu Dar es salaam, leo tarehe 28 Aprili 2015. 




Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.