Friday, April 10, 2015

Rais amteua Mhe. Mgaza kuwa Balozi wa Saudi Arabia

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Mhe. Hemed Iddi Mgaza kuwa Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi (KMK), Balozi Ombeni Sefue imesema uteuzi huo ulianza Machi 27.

Kabla ya uteuzi huo, Mhe. Mgaza alikuwa Ofisa Mambo ya Nje Mkuu, Daraja la Pili na Mkuu wa Utawala katika Ubalozi wa Tanzania nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

Mhe. Mgaza anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Balozi Abdillah Omar ambaye mkataba wake wa utumishi umekwisha.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.