Thursday, April 9, 2015

Rais Mstaafu Mkapa atoa elimu ya uchumi kwa Mabalozi, Maofisa na Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje

Rais wa Awamu ya Tatu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Benjamin William Mkapa akitoa mada katika semina ya masuala ya diplomasia ya uchumi kwa Mabalozi, Maofisa na Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa (hawapo pichani). Semina hiyo ilifanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere jijini Dar es Salaam tarehe 9 Aprili 2015.
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), akimpokea Rais wa Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin William Mkapa mara baada ya kuwasili Mwalimu Nyerere kwa ajili ya semina hiyo. 

 ...Waheshimiwa wakielekea ukumbini.
 Rais Mstaafu Mkapa akiteta jambo na Mhe. Membe wakati wa semina hiyo ambapo alizungumzia changamoto za ushirikiano wa kiuchumi na diplomasia nchini Tanzania, na nje ya nchi na kwenye Jumuiya za Kimataifa. Andiko la mada hii litapatikana baada ya muda mfupi kwenye tovuti ya Wizara www.foreign.go.tz
 Mabalozi, Maofisa na Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje pamoja na Walimu na Wanachuo cha Diplomasia wakimsikiliza kwa makini Mhe. Benjamin W. Mkapa. 

 Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati Balozi Simba Yahya (mbele kushoto) pamoja na Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria Balozi Irene Kasyanju wakifuatilia semina hiyo.
 Wajumbe wa semina wakimsikiliza kwa makini Balozi Mlay (Mstaafu) (mbele kushoto aliyesimama) akitoa maoni yake kuhusu mada iliyowasilishwa katika semina hiyo.
 Balozi (Mstaafu) Bertha Semi Somi akichangia katika semina hiyo.
 Mhadhiri wa Chuo cha Diplomasia Dkt. Kitojo akiuliza swali katika semina hiyo. 
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali kwa Umma wa Wizara ya Mambo ya Nje Bi. Mindi Kasiga akiuliza swali kufuatia mada iliyotolewa na Rais Mstaafu Mhe. Mkapa katika hiyo semina hiyo.
  Baadhi ya washiriki wakifuatilia mjadala wa semina hiyo.
Rais Mstaafu Benjamin W. Mkapa (katikati), Waziri wa Mambo ya Nje Mhe. Bernard Membe na Kaimu Katibu Mkuu wa  Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Rajab Gamaha,  kwenye picha ya pamoja na Maafisa Mambo ya Nje.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.