Monday, April 13, 2015

Mapokezi ya Waziri Membe nchini Kuwait katika Picha

Mhe. Bernard Membe akiwasili hotelini nchini Kuwait kwa ziara ya siku moja ambapo atakutana na kufanya mzaungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Kuwait na Mkurugenzi Mkuu wa Kuwait Fund.  

Aliyeongozana na Waziri Membe ni Balozi wa Kuwait nchini Tanzania Mhe. Nassem Ibrahim Al Najib ambaye alimpokea uwanja wa ndege.

Waziri Membe kwenye picha ya pamoja na baadhi na Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao kwenye nchi ya Kuwait na Tanzania. (Wa kwanza kushoto) ni Mhe. Prof. Abdillah Omari, Balozi wa Tanzania nchini Kuwait mwenye makazi yake Saudia Arabia na (kulia) ni Mhe. Nassem Ibrahim Al Najib, Balozi wa Kuwait nchini Tanzania.

Mhe. Membe ujumbe wake wakimsikiliza Mhe. Najib na kuangalia picha za viongozi mbalimbali wa Kuwait.

Msafara wa Mhe. Membe ukitokea airport kuelekea hotelini ambapo atakaa kwa siku leo tarehe 13 usiku hadi 14 usiku, Aprili 2015 (usiku) moja kabla ya kuelekea Oman kuendelea na ziara yake.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.