Friday, April 10, 2015

Rais Mstaafu Mkapa atoa elimu ya uchumi kwa Mabalozi, Maofisa na Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje

Rais wa Awamu ya Tatu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Benjamin William Mkapa akitoa mada katika semina ya masuala ya diplomasia ya uchumi kwa Mabalozi, Maofisa na Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa (hawapo pichani). Semina hiyo ilifanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere jijini Dar es Salaam tarehe 9 Aprili 2015.
Mkaguzi Mkuu wa ndani Bw. Mathias Abisai (wakwanza kushoto), Mkurugenzi Idara ya Ununuzi Bw.Elias Suka (Katikati), wakiwa pamoja na Mhasibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje Bw. Paul Kabale wakati wa Semina hiyo 
Sehemu ya Watumishi wakisikiliza kwa makini elimu iliyokuwa ikitolewa na Rais Mstaafu Benjamini Mkapa.
Waziri Membe akitoa Ufafanuzi katika moja ya mambo yaliyo jadiliwa
Mkurugenzi Idara ya Asia na Australasia Balozi Mbelwa Kairuki (Kushoto), Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Bi. Mindi Kasiga
Sehemu nyingine ya walioudhuria Semina Hiyo.
Balozi Mstaafu Mhe. Simon Mlay akiuliza swali meza kuu
Mkurugenzi wa Masomo wa Chuo cha Diplomasia Dkt. Watengere Kitojo akiuliza swali. 


Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati Balozi Simba Yahya (mbele kushoto) pamoja na Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria Balozi Irene Kasyanju wakifuatilia semina hiyo.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Mambo ya Nje Bi. Mindi Kasiga 
Muhadhiri kutoka Chuo cha Diplomasia Dr. Lucy Shule akiuliza swali
Rais Mstaafu Mkapa akiteta jambo na Mhe. Membe wakati wa semina hiyo ambapo alizungumzia changamoto za ushirikiano wa kiuchumi na diplomasia nchini Tanzania, na nje ya nchi na kwenye Jumuiya za Kimataifa. Andiko la mada hii litapatikana baada ya muda mfupi kwenye tovuti ya Wizara www.foreign.go.tz
Baadhi ya washiriki wakifuatilia mjadala wa semina hiyo.
Rais Mstaafu Benjamini W. Mkapa, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe (Mb.), na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Rajab Gamaha, kwenye Picha ya Pamoja na Watumishi Wizara ya Mambo ya Nje na Chuo cha Diplomasia 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), akimpokea Rais wa Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin William Mkapa mara baada ya kuwasili Mwalimu Nyerere kwa ajili ya semina hiyo. 

Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.