Friday, September 14, 2018

Prof. Mkenda na Balozi wa Kenya wakutana kujadili utatuzi wa changamoto za biashara mipakani

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda akizungumza na Balozi wa Kenya nchini, Mhe. Dan Kazungu walipokutana jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuzungumzia masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Kenya. Pamoja na mambo mengine walijadili changamoto za biashara hususan tukio la hivi karibuni la kukwamishwa kwa bidhaa za Tanzania kuingia Kenya kwa sababu mbalimbali ikiwemo vinywaji, mchele na unga wa ngano. Katika kikao hicho ilikubalika Tanzania kuitisha kikao cha Makatibu Wakuu wenye dhamana ya Mambo ya Nje na Afrika Mashariki na Biashara na Wakuu wa Mamlaka za Mapato za Tanzania na Kenya. Pia walikubaliana kuendelea kuratibu ziara za viongozi wa juu kati ya nchi hizi mbili kwa lengo la kukuza mahusiano.

Prof. Mkenda na Balozi Kazungu wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mazungumzo yao.

Thursday, September 13, 2018

Waziri Mahiga afungua rasmi Ofisi za Uwakilishi wa Ubalozi wa Ujerumani jijini Dodoma

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga kwa pamoja na Balozi wa Ujerumani nchini, Mhe. Detlef Waechter wakikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa Ofisi Ndogo ya Uwakilishi wa Ubalozi wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani jijini Dodoma. Ofisi hiyo ni ya kwanza kwa Balozi za nje zilizopo Tanzania kufunguliwa Dodoma. Ufunguzi huo ni katika kuitikia wito wa Mhe. Rais baada ya Serikali kuhamia  rasmi Dodoma. Ofisi hizo ambazo zipo ghorofa ya nne katika Jengo la PSPF Barabara ya Benjamin Mkapa zitatoa huduma mbalimbali kwa Serikali, Bunge na Wananchi kwa ujumla huku zikisimamiwa na Bw. Richard Shaba ambaye ni Mtanzania. Pia Ofisi hizo zimejumuisha Mashirika ya Misaada ya Ujerumani ambayo ni GIZ na KFW.
Mhe. Waziri Mahiga kwa pamoja na Balozi Waechter wakifungua kitambaa kuashiria kuwa Ofisi Ndogo za Uwakilishi wa Ubalozi wa Ujerumani zimefunguliwa rasmi jijini Dodoma
Mhe. Waziri Mahiga akizungumza wakati wa hafla hiyo ambapo aliipongeza Serikali ya Ujerumani kwa uamuzi huo ambao ni ishara njema kwamba nchi hiyo inaunga mkono kwa dhati uamuzi wa Serikali wa kuhamia Dodoma. Pia alisema Tanzania ina mengi ya kujifunza kutoka Ujerumani kwani nchi hiyo ina uzoefu wa kuhamisha makao makuu kutoka Bonn kwenda Berlin ambapo ilifanya hivyo miaka 30 iliyopita
Mhe. Waziri Mahiga akiendelea na hotuba yake. Wengine katika picha ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Dkt. Binilith Mahenge (wa nne kushoto), Balozi Waechter (wa pili kulia), Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Jestas Nyamanga (kushoto), Msimamizi wa Ofisi Ndogo za Uwakilishi wa Ubalozi wa Ujerumani jijini Dodoma, Bw. Richard Shaba (wa tatu kushoto), Katibu wa Waziri, Bw. Gerald Mbwafu (wa pili kushoto na Wawakilishi kutoka GIZ na KFW. 
Mhe. Balozi Waechter nae akizungumza ambapo alisema wamefungua Ofisi hizo ili kuendelea kuimarisha ushirikiano uliopo katika nyanja mbalimbali kati ya Tanzania na Ujerumani
Mhe. Waziri Mahiga akiwa katika picha na Mhe. Balozi Waechter pamoja na viongozi wengine walioshiriki hafla hiyo
Mhe. Waziri Mahiga akimpongeza Balozi Waechter ufunguzi wa Ofisi Ndogo za Uwakilishi wa Ubalozi wa Ujerumani jijini Dodoma
Wageni waalikwa walioshiriki ufunguzi wa Ofisi hizo wakifuatilia matukio mbalimbali 
Mhe. Waziri Mahiga akizungumza na vyombo vya habari
Awali Mhe. Waziri Mahiga alisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili kwenye Ofisi Ndogo za Uwakilishi wa Ubalozi wa Ujerumani zilizopo jijini Dodoma. Kushoto ni Balozi wa Ujerumani nchini, Mhe. Detlef Waechter. Wa pili kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Dkt. Binilith Mahenge na kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Jestas Nyamanga
Mhe. Waziri Mahiga, Mhe. Balozi Waechter na Mkuu wa Dodoma Dkt. Mahenge wakiwa katika picha ya pamoja na wageni waalikwa walioshiriki hafla hiyo wakiwemo Watumishi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Picha ya pamoja na wafanyakazi wa Ubalozi wa Ujerumani nchini



Wednesday, September 12, 2018

Tanzania ilivyoshiriki Maonesho ya Kimataifa ya Biashara nchini Msumbiji

Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji, Mheshimiwa Rajabu Luhwavi, (katikati), akikaribishwa katika Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya 54 ya FACIM yaliyofanyika tarehe 27 Agosti hadi 2 Septemba 2018 Maputo nchini Msumbiji. Wengine ni Bw. Albert Philipo, Afisa wa Wizara, Idara ya Diaspora (kushoto) na ndugu Nelson Nkini, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania (Diaspora) wanaoishi nchini Msumbiji  Ushiriki wa wafanyabiashara kutoka Tanzania uliratibiwa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kupitia Ubalozi wa Tanzania nchini Msumbiji kwa kushirikiana na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade).
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Msumbiji, Mheshimiwa Carlos Agostinho do Rosário wakati wa ufunguzi wa Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya 54 ya FACIM alipotembelea banda la Tanzania na kukaribishwa na Bi. Getrude Ngweshemi, Kaimu Meneja - Masoko ya Ndani wa TanTrade na Bw. Albert Philipo, Afisa Idara ya Diaspora, Wizara ya Mambo ya Nje ambapo alipatiwa maelezo kuhusu bidhaa za viwandani pamoja na vivutio vya utalii wa Tanzania.
                                                                                                         

Balozi Rajabu Luhwavi akifafanua jambo kwa wafanyabiashara na washiriki kutoka mataifa mengine (hawapo pichani) waliofika katika banda la Tanzania wakati maonesho ya biashara ya 54 ya FACIM yakiendelea.  Wafanyabiashara wa Tanzania walikutana na wafanyabiashara wenzao kutoka mataifa zaidi ya 20 ambapo walibadilishana mawazo na kuzitangaza bidhaa na huduma za Tanzania katika maonesho hayo.
Balozi Rajabu Luhwavi akipokea maelezo kutoka kwa Afisa wa Wizara, Bw. Albert Philipo kuhusu bidhaa za Tanzania zilizoletwa na wafanyabiashara mbambali kutoka Tanzania wakati wa maonesho ya biashara ya kimataifa ya 54 ya FACIM Maputo, Msumbiji. Wengine katika picha hiyo ni wafanyabiashara kutoka Kampuni mbalimbali nchini Tanzania.

Mheshimiwa Balozi Luhwavi akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyabiashara kutoka Tanzania walioshiriki katika Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya 54 ya FACIM mjini Maputo.
Gavana wa Nampula, Mheshimiwa Victor Borges akiwa na Mheshimiwa Balozi Rajabu Luhwavi kushoto kwake wakikata utepe wakati wa kufungua Maonyesho ya Biashara Nampula tarehe 20 Agosti 2018. Maonesho hayo yalihusisha wafanyabiashara kutoka Tanzania na wenyeji wa Msumbiji. 
Mheshimiwa Balozi Rajabu Luhwavi akitoa maelezo mafupi wakati wa ufunguzi wa Maonyesho ya Biashara Nampula yaliyohusisha wafanyabiashara kutoka Tanzania. Kwa upande wake Balozi Luhwavi, alieleza kuwa maonesho haya ni ya kimkakati kwa ajili ya kukuza na kuimarisha umoja, mshikamano na mahusiano ya kiuchumi yaliyojengwa na waasisi wetu hayati Mwalimu Julius Nyerere, aliyekuwa Rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; hayati Sheikh Abeid Amani Karume, aliyekuwa rais wa kwanza wa Zanzibar na hayati Samora Moises Machel, aliyekuwa rais wa kwanza wa Jamhuri ya Msumbiji. Maonesho haya yalifungua fursa za masoko kwa bidhaa za viwanda vya Tanzania pamoja na kuendeleza juhudi za utekelezaji wa diplomasia ya uchumi kwa vitendo na kukuza uchumi, hususan uchumi wa viwanda.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Ndugu Juma Ali Juma aliyekuwa mgeni rasmi wakati wa kilele cha maonesho ya bidhaa za viwanda vya Tanzania mjini Nampula akiwa pamoja na Balozi Rajabu Luhwavi na Katibu Mkuu wa Jimbo la Nampula, Bi. Veronica Langa wakipata maelezo kuhusu teknolojia ya ufugaji samaki kutoka kampuni ya Dokaman ya nchini Tanzania.
Kutoka kulia ni Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji, Mheshimiwa Rajabu Luhwavi, Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Ndugu Juma Ali Juma, Mkurugenzi wa Ukuzaji Biashara TanTrade, Bi. Anna Bulondo wakipata maelezo kutoka kwa wawakilishi wa kampuni ya A - Z Textile Mills. 

Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji, Mheshimiwa Rajabu Luhwavi akiwa pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Ndugu Juma Ali Juma wakipokea maelezo kuhusu bidhaa zinazotengenezwa na Kampuni ya Tanzania M/s Darsh Industries wakati wa maonesho ya bidhaa za viwanda mjini Nampula, Msumbiji. 





Monday, September 3, 2018

Tanzania na China zasaini Mkataba wa Makubaliano ya ushirikiano kwenye sekta ya kilimo na uvuvi

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akiwa kwenye mazungumzo rasmi na Waziri wa Kilimo, Uvuvi na Mifugo wa China, Mhe. Han Changfu alipotembelea Makao Makuu ya Wizara hiyo jijini Beijing tarehe 03 Septemba, 2018. Katika mazungumzo yao Mhe. Majaliwa alimweleza Waziri Han nia ya Tanzania ya kushirikiana na China katika kuendeleza sekta za kilimo, uvuvi na mifugo. Naye Waziri Han alimhakikishia Waziri Mkuu ushirikiano wa hali ya juu kati ya Tanzania na China ambapo nchi hiyo ipo tayari kutoa mafunzo ya muda mfupi na mrefu kwa wataalam wa kilimo kutoaka Tanzania. Mhe. Waziri Mkuu yupo nchini China kwa niaba ya Mhe. Rais kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la shirikiano kati Afrika na China.
Mazungumzo ya pande mbili yakiendelea na kuhudhuriwa na viongozi wengine mbalimbali akiwemo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga, Katibu Mkuu, Prof. Adolf Mkenda na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Bw. Khatibu Kazungu. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia Bibi Justa Nyange akifuatilia mazungumzo
Waziri wa Kilimo, Maliasili na Uvuvi kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Rashid Ali Juma kwa pamoja na mwakilishi kutoka Wizara ya Kilimo ya China wakisaini kwa niaba ya Serikali zao Mkataba wa Makubaliano ya Ushirikiano kwenye sekta za kilimo na uvuvi. Wanaoshuhudia ni Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa na Waziri wa Kilimo wa China, Mhe. Han Changfu
Wakibadilishana mkataba mara baada ya kuusaini




Waziri Mkuu ahamasisha uwekezaji kutoka Jimbo la Jiangsu la China


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akisalimiana na Naibu Meya wa Jimbo la Jiangsu la nchini China, Bw.Guo Yuan Qiung mara alpowasili kwenye Ubalozi wa Tanzania nchini China kwa ajili ya mazungumzo rasmi. Mhe. Waziri Mkuu yupo nchini humo kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya Afrika Nna China (FOCAC) utakaofanyika tarehe 03 na 04 Septemba, 2018.
 
Mhe. Waziri Mkuu akizungumza na Bw. Qiung mara baada ya kumkaribisha Ubalozini
Mhe. Waziri Mkuu akimtambulisha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Augustine Mahiga kwa Naibu Meya Qiung wakati wa mazungumzo rasmi kati ya Waziri Mkuu na Naibu Meya

Mhe. Waziri Mkuu na ujumbe wa Tanzania wakizungumza na Naibu Meya wa Jiangsu na ujumbe wake walipofika Ubalozini. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda.
Naibu Meya Qiung (wa tatu kulia) akiwa na ujumbe aliofuatana nao wakimsikiliza Waziri Mkuu hayupo pichani

Mazungumzo yakiendelea

Mazungumzo yakiendelea. Wa pili kulia ni Balozi wa Tanzania nchini China Mhe. Mbelwa Kairuki

============================================================

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa amesema Tanzania inahitaji wawekezaji wa uhakika kwenye sekta ya kilimo hususan watakaowekeza kwenye viwanda vya kuchakata mazao ya kilimo, kuongeza thamani na kutafuta masoko.

Mhe. Majaliwa aliyasema hayo wakati wa mazugumzo yake na Naibu Meya wa Jimbo la Jiangsu nchini China, Bw. Guo Yuan Qiung aliyoyafanya tarehe 03 Septemba, 2018 katika Ubalozi wa Tanzania nchini humo ikiwa ni mwendelezo wa program yake ya kukutana na wadau muhimu wa maendeleo kabla ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya Afrika na China (FOCAC) utafanyika jijini Beijing kuanzia tarehe 01 hadi 04 Septemba, 2018.

Katika mazungumzo yao, Mhe. Waziri Mkuu alimweleza Naibu Meya huyo kuwa, Tanzania inaendelea kuboresha sekta ya kilimo kwa kushirikiana na wadau mbalimbali na kwamba jimbo la Jiangsu ni moja ya mdau muhimu ambaye anaweza kuchangia maendeleo ya Tanzania kwa kutumia teknolojia ya viwanda vya uchakataji mazao ili kuongeza thamani na kupata masoko ya uhakika kwa mazao hayo. Alisema kuwa kwa kuwa jimbo la Jiangsu ni miongoni mwa majimbo yaliyopiga hatua kubwa ya maendeleo ya teknolojia na viwanda duniani. Hivyo kushirikiana na Tanzania katika sekta za kilimo na viwanda kutaiwezesha nchi kufikia malengo yake ya kuwa nchi ya nchi ya viwanda ifikapo mwaka 2020 na nchi ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

Pia alisema kuwa, anathamini mchango wa Jimbo hilo katika uchumi wa Tanzania ambapo sasa kuna Kampuni mbili kubwa za uwekezaji kutoka jimboni humo ikiwemo kampuni ya kuchambua pamba na kutengeneza nyuzi ya mjini Shinyangana na Kiwanda cha Urafiki cha jijini Dar es Salaam. Hata hivyo alisema bado mchango wa jimbo hilo unahitajika katika uendelezaji viwanda hususan katika masuala ya teknolojia ya viwanda; kuimarisha utafiti kwenye sekta ya kilimo na kuisaidia Tanzania kupata masoko ya mazao kama mbaazi, mhogo na soya.

“Tanzania inapongeza kazi nzuri unayoifanya na tunathamini sana mchango wako katika maendeleo ya nchi yetu. Hadi sasa tunavyo viwanda viwili kutoka Juangshu. Tunaomba uendelee kuhamasisha kampuni nyingi zaidi kutoka jimboni kwako kuja kuwekeza nchini kwenye maeneo mbalimbali pamoja na kutusaidia kupata masoko ya mazao kama mbaazi, mhogo na soya” alisisitiza Mhe. Majaliwa.

Katika hatua nyingine walikubaliana na Naibu Meya huyo kuangalia uwezekano wa kufanya mapitio kuhusu changamoto  za uendeshaji wa Kiwanda cha Urafiki ili kutafuta suluhu ya haraka kwa kiwanda hicho ikiwa ni pamoja na kuwaagiza wataalam wa pande mbili kukutana kuainisha changamoto hizo.

Kwa upande wake, Bw. Qiung alimhakikishia ushirikiano wa hali ya juu Mhe. Waziri Mkuu hususan katika uwekezaji wa viwanda na kwamba ni Imani yake kuwa mkutano wa FOCAC utatoa dira kwa maendeleo si kwa  Tanzania pekee bali kwa Bara zima la Afrika.

Aidha aliongeza kuwa, mbali na ushirikiano katika masuala ya kilimo na uendelezaji viwanda, jimbo lake lipo tayari kushirikiana na Tanzania katika masuala ya elimu ambapo jimbo hilo lina vyuo vikuu zaidi ya 60,000 vinvyotoa kozi mbalimbali na kuwakaribisha wanafunzi kutoka Tanzania kwenda jimboni humo.

Sunday, September 2, 2018

Tanzania yapata Mwakilishi wa Heshima Hong Kong na Macao

Balozi wa Tanzania nchini China, Mhe. Mbelwa Kairuki kwa pamoja na Bibi Annie Suk-Ching Wu wakisaini Mkataba kumwezesha Bibi Wu kuwa Mwakilishi wa Heshima wa Tanzania huko Hong Kong na Macao. Tukio hilo lilifanyika kwenye Ubalozi wa Tanzania jijini Beijing, China na kushuhudiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda pamoja viongozi wengine ambao wapo nchini China kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya Afrika na China (FOCAC).
Balozi Mbelwa na Bibi Wu wakibadilishana mkataba mara baada ya kuusaini
Mhe. Waziri Mahiga akitoa hotuba kumpongeza Bibi Wu kwa kukubali kuiwakilisha Tanzania kwenye maeneo hayo na kumtaka kuiwakilisha vema nchi
Mhe. Waziri na viongozi wengine wakisubiri kuanza kwa ratiba
Mhe. Waziri Mahiga akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Balozi Mbelwa na Bibi Wu mara baada ya kushuhudia uwekwaji saini wa mkataba wa kumwezesha Bibi Wu kuiwakilisha Tanzania Hong Kong na Macao
Picha ya pamoja na viongozi na wageni mbalimbali waliohudhuria hafla hiyo
Katibu Mkuu, Prof. Mkenda akiteta jambo na Mhe. Balozi Mbelwa
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Bibi Justa Nyange akiwa na Maafisa ambao walikuwepo kushuhudia uwekwaji saini wa mkataba wa kumwezesha Bibi Wu kuwa Mwakilishi wa Heshima kwenye majimbo ya Hong Kong na Macao ya nchini China

Waziri Mkuu afungua Kongamano la Biashara kati ya Tanzania na China

Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa akitoa hotuba wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Biashara kati ya Tanzania na China ambapo zaidi ya Kampuni 80 kutoka nchi hizi mbili zilishiriki. Wakati wa Kongamano hilo Mhe. Waziri Mkuu alizialika kampuni za biashara na uwekezaji kutoka China kuja kuwekeza Tanzania na kusisitiza kuwa mazingira ya uwekezaji ni mazuri. Mhe. Waziri Mkuu yupo nchini China kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika utakaofanyika tarehe 3 na 4 Septemba, 2018 jijini Beijing.


Sehemu ya wageni waalikwa wakfuatilia hotuba ya Mhe. Waziri Mkuu

Sehemu ya wageni kutoka Tanzania akiwemo Mzee John Cheyo wakifuatilia mkutano

Balozi wa Tanzania nchini China Mhe. Mbelwa Kairuki akitoa neno wakati wa Kongamano hilo
Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Bw. Geofrey Mwambe akiwa pamoja na wageni wengine walioshiriki kongamano hilo

Mkurugenzi Mkuu wa Eneo Maalum la Uwekezaji (EPZA), Kanali Mstaafu Joseph Simbakalia naye akifuatilia Kongamano la Biashara kati ya Tanzania na China

Balozi wa China nchini Tanzania, Mhe. Wwang Ke naye alishiriki kongamano hilo

Sehemu nyingine ya wageni waalikwa

Mshereheshaji kwenye kongaano hilo Bw. Laizer Mollel akitoa ratiba kabla ya kuanza kwa kongamano

Mhe. Balozi Kairuki akihojiwa na Mwandishi kutoka TBC, Bi. Anna Mwasyoke kuhusu umuhimu wa kongamano hilo kwa Tanzania
====================================================
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa amewakaribisha wafanyabiasha na wawekezaji kutoka China kuja Tanzania kuwekeza kutokana na  mazingira rafiki ya uwekezaji na hali ya amani na utulivu iliyopo nchini.

Waziri Mkuu alitoa rai hiyo wakati akifungua  Kongamano la Biashara kati ya Tanzania na China lililowashirikisha wafanyabiashara zaidi ya 80 kutoka nchi hizi mbili. Mhe. Majaliwa ambaye yupo nchini China kwa ajili ya kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya Afrika na China (FOCAC) alitumia fursa hiyo kukutana na wafanyabiashara hao ili kuwaeleza hali ya uwekezaji nchini katika

Mhe. Majaliwa alisema kuwa, Tanzania imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali za kuvutia wawekezaji ambazo kwa kiasi kikubwa  zimezaa matunda ambapo katika Ripoti ya uwekezaji duniani kwa mwaka 2018 imeitaja Tanzania kuwa kitovu cha uwekezaji kwa ukanda wa Afrika Mashariki ambapo imewekeza takribani dola za marekani bilioni 1.2.

Mhe. Majaliwa aliongeza kuwa, Tanzania inamazingira mazuri sana ya uwekezaji ikiwemo ardhi nzuri kwa kilimo cha mazao mbalimbali kama miwa, mpunga, ngano, mahindi, Mhogo na katani. Alisema kuwa, jumla ya hekta milioni 44 za ardhi zinafaa kwa kilimo na zaidi ya hekta milioni 29 zinafaa kwa kilimo cha umwagiliaji.

Akizungumzia sekta ya madini, Mhe. Majaliwa alisema kuwa ni moja ya sekta muhimu inayochangia pato la taifa na kuwahamashisha wawekezaji kuchangamkia sekta hiyo hususan kwenye uchimbaji na uchakataji wa madini ya chuma na uchimbaji wa madini ya urani.

Kuhusu utalii, Mhe. Waziri Mkuu alisema kuwa Tanzania imekuwa ikifaidika kwa kiasi kikubwa kutokana na kujaliwa vivutio vingi vya utalii ikiwemo fukwe zilizopo Zanzibar, Mlima Kilimanjaro na Hifadhi ya Ngororngoro. Hata hivyo alisema bado sekta hii inahitaji wawekezaji hususan kwenye ujenzi wa miundombinu ya utalii kama vile hoteli na sekta ya huduma kwa watalii kwa ujumla.

Masuala mengine aliyowaeleza wawekezaji hao ambayo ni fursa kwao ni pamoja na eneo la teknolojia ya habari na mawasiliano ambapo kwa sasa soko ni kubwa  kutokana na ongezeko la watumiaji wa simu na mitandao hususan watu wanaoishi vijijini. Aliwakaribisha wawekezaji kuwekeza katika sekta hii katika maeneo ya ukarabati na utengenezaji wa vifaa vya mawasiliano na kujenga viwanda vya kuunganisha simu.

Mhe. Waziri Mkuu alihitimisha kwa kuhimiza wawekezaji kuja nchini na kusisitiza kuwa, “ukitaka kuwekeza Afrika karibu Tanzania”