Saturday, August 17, 2019

Mkutano wa 39 wa Wakuu wa nchi na Serikali wa nchi za SADC wafunguliwa rasmi

Wakuu wa nchi na Serikali wa nchi wanachama wa  Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) pamoja wa wajumbe mbalimbali waliohudhuria ufunguzi wa Mkutano wa 39 wa Kilele wa Wakuu hao wakiwa wamesimama wakati wimbo wa Taifa na Jumuiya ukipigwa. Mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.

Pamoja na mambo mengine yaliyojiri katika mkutano huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amekabidhiwa nafasi ya uenyekiti wa Jumuiya hiyo ambapo atahudumu kwa kipindi cha mwaka mmoja 2019/ 2020

Mkutano huu unaofanyika kwa siku mbili utafikia tamati kesho tarehe 17 Agosti, 2019
Wakuu wa nchi na Serikali wa nchi wanachama wa SADC wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya Mkutano wa ufunguzi uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaa 
Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akikabidhiwa uenyekiti na mwenyekiti anayemaliza muda wake Mhe. Hage Geingob Rais wa Namibia, wakati ufunguzi wa Mkutano wa kilele wakawaida wa Wakuu wa nchi na Serikali wa nchi za SADC uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akifuatilia tukio hilo.
Dkt. Stregomena Tax Katibu Mtendaji wa SADC, akihutubia wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa nchi za SADC 
Wakuu wa nchi na Serikali wa nchi wanachama wa SADC wakiwa wamesimama wakati wimbo wa Taifa na SADC ukiwa unapigwa kabla ya kuanza kwa Mkutano
Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akifuatilia Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa nchi wanachama za SADC uliokuwa ukiendelea
Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akifuatilia Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa nchi wanachama za SADC uliokuwa ukiendelea
Baadhi ya Mambalozi wa Tanzania wanaoiwakilisha nchi sehemu mbalimbali  wakifurahia jambo wakati wa Mkutano uliokuwa ukiendelea wa Wakuu wa nchi na Serikali wa nchi wanachama za SADC
Sehemu nyingine ya Mabalozi wa Tanzania wakifuatilia Mkutano

Mabalozi wa Tanzania wahitimisha ziara ya miradi maendeleo


Mabalozi wa Tanzania wanaoiwakilisha nchi sehemu mbalimbali duniani wakiwa Makao Makuu  ya Kampuni ya Taifa Gas iliyopo Kigamboni, Dar es Salaam  walipoitembelea kampuni hiyo kwa lengo la kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na Kampuni hiyo.

Maeneo mengine ambayo Mabalozi  wametembelea ni pamoja na Uwanja mpya ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (Teminal 3) mradi wa ujenzi wa barabara za juu za Ubungo (Ubungo interchange), Mamlaka ya Usimamizi wa Mawasiliano Tanzania (TCRA)  na Ujenzi wa mradi wa dajara jipya la surrender.
Mabalozi wakisikiliza ufanunuzi wa masuala mbalimbali kutoka kwa watendaji wa Kampuni ya Taifa Gas walipoitembela Makao Makuu ya Kampuni hiyo. 
Mhe. Baraka Luvanda Balozi wa Tanzania nchini India (Wakwanza kulia) na Mhe. Matilda Masuka Balozi wa Tanzania Jamhuri ya Korea wakifuatilia hotuba fupi ya ukaribisho.
Tokea kulia: Mhe. Asharose Migiro Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mhe. Dkt. Wilbroad Slaa Balozi Tanzania nchini Sweden, Mhe. Dkt. Pindi Chana Balozi wa Tanzania nchini Kenya, na Mhe. Wilson Masilingi Balozi wa Tanzania Washngton DC wakifuatila hotuba ya ukaribisho ya Taifa Gas, Dar es Salaam 
Mabalozi wakiwa Uwanja Mpya wa Ndege wa Julius Nyerere (Terminal 3) walipotembelea kuona ufanisi wa uwanja huo.  
Mabalozi wakisikiliza ufafanuzi kutoka kwa mtaalam walipotembelea eneo la ujenzi wa barabara za juu eneo la Ubungo, Dar es Salaam
Balozi Ramadhani Mwinyi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki  akisalimiana na Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano alipowasili Makao Makuu ya TCRA akiwa ameambatana na ujumbe wa Mabalozi
Mabalozi wakiwa katika picha ya pamoja na watendaji wa TCRA walipotembelea Makao makuu ya Ofisi hiyo

Friday, August 16, 2019

Rais Ramaphosa aitembelea kambi ya Wapigania uhuru wa Afrika Kusini iliyopo Mazimbu, Morogoro

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa ameongozana na Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini, Mhe. Cyril Ramaphosa pamoja na mkewe mara baada ya kuwapokea walipotembelea iliyokuwa Kambi ya Wapigania uhuru dhidi ya ubaguzi wa rangi kutoka Afrika Kusini iliyopo Mazimbu mkoani Morogoro. Kambi hiyo ni maarufu kwa jina la Solomon Mahlangu mmoja wa wapigaia uhuru aliyewahi kuishi kwenye kambi hiyo. Ziara ya Mhe. Rais Ramaphosa imefanyika tarehe 16 Agosti 2019
Mhe. Rais Ramaphosa akizungumza wakati alipotembelea kambi za wapigaia uhuru kutoka Afrika Kusini zilizopo Mazimbu mkoani Morogoro. Katika hotuba yake alitoa shukrani kwa Watanzania hususan wakazi wa eneo hilo kwa mchango mkubwa walioutoa ikiwemo kutoa eneo na kuwahifadhi wapigania uhuru wa nchi hiyo ambapo alisema amefarijika kukanyaga ardhi hiyo yenye historia kubwa ya ushirikiano wa kindugu kati ya Tanzania na Afrika Kusini. Pia aliahidi kuhakikisha nchi yake inaimarisha soko la mazao mbalimbali kutoka Morogoro na pia kuifanya kambi hiyo kuwa kituo kikubwa cha utalii.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza wakati wa ziara ya Mhe. Rais Ramaphosa iliyofanyika kwenye kambi ya wapigania uhuru wa Afrika Kusini iliyopo Mazimbu mkoani Morogoro. Mhe. Waziri Mkuu alisistiza nchi hizo kuimarisha ushirikiano  wa kihistoria uliopo kati ya Tanzania na Afrika Kusini
Mhe. Prof. Kabudi naye akizungumza wakati wa ziara ya Rais wa Afrika Kusini mkoani Morogoro
Sehemu ya wadau mbalimbali wakifuatilia hotuba za viongozi

Sehemu nyingine ya wananchi waliojitokeza kwenye ziara ya Mhe. Rais Ramaphosa mkoani Morogoro

Msemaji wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi akiwa na Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiabo wa Afrika Mashariki, Bw. Emmanuel Buhohela wakati wa ziara ya Rais wa Afrika Kusini kwenye kambi za wapigania uhuru kutoka Afrika Kusini zilizopo Mazimbu mkoani Morogoro

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika  Mashariki, Bw. Wilbroad Kayombo (katikati) akishiriki na wadau wengine ziara ya Rais wa Afrika Kusini alipotembelea mkoani Morogoro
Wageni waalikwa

Mhe. Waziri Mkuu akimkabidhi zawadi Mhe. Rais Ramaphosa
Mhe. Rais Ramaphosa akiwa ameongozana na Mhe. Waziri Mkuu wakipita kwenye makaburi ya wapigania uhuru kutoka Afrika Kusini yaliyopo Mazimbu, Morogoro
Mhe. Rais Ramaphosa akimsikiliza mmoja wa watoto wa wapigania uhuru aliyezikwa kwenye eneo hilo

Mhe. Rais Ramaphosa akipanda mti wa kumbukumbu mara baada ya kumaliza ziara yake kwenye kambi ya wapigania uhuru kutoka nchini kwake iliyopo Mazimbu, Morogoro

Mhe. Rais Ramaphosa aliumwagia maji mti huo mara baada ya kuupanda

Mhe. Rais Ramaphosa akiweka shada la maua kuwakumbuka wapigania uhuru wa Afrika Kusini waliokufa wakiwa kwenye harakati za kuiokomboa nchi hiyo dhidi ya ubaguzi wa rangi 

Mhe. Rais Ramaphosa akiwaaga wananchi waliojitokeza kwenye ziara yake alipotembelea kambi ya wapigania uhuru wa Afrika Kusini iliyopo Mazimbu, Morogoro

MABALOZI WA TANZANIA WATEMEBELEA MRADI WA RELI NA UPANUZI WA BANDARI YA DAR ES SALAAM



Mhe. Nahim Azizi Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia na Umoja wa Afrika  akisalimiana na mfanyakazi wa Bandari ya Dar es Salaam akiwa na ujumbe wa mabalozi wengine walipowasili bandarini hapo kwa ziara ya kikazi.


Wakiwa katika Bandari ya Dar es Salaam mabalozi walipata nafasi ya kutembelea mradi wa ujenzi wa upanuzi wa bandari sambamba na kuongeza kina cha bahari ili kuweza kuhudumia meli zinazobeba mzigo mkubwa. 

Mara baada ya kukamilika kwa mradi huo, Bandari ya Dar es Salaam itakuwa na uwezo wa kuhudumia mizigo ya kiasi cha tani milioni 28 kwa mwaka, ikiwa ni mara mbili ya kiwango cha sasa ambapo inauwezo wa kuhudumia mizigo kiasi cha tani milioni 13 pekee. 

Aidha, sambamba na kuongezeka kwa uwezo wa kuhudumia mizigo mingi, pia mradi huo utapunguza muda wa kuhudumia meli kutoka masaa 80 kwa meli moja kama ilivyo sasa hadi masaa 30 mara mradi huo utakapo kamilika.

Wakati huo huo  mabalozi walitembelea mradi wa ujenzi wa wa reli ya kiwango cha kimataifa (SGR) ambapo walipata fursa ya kuona maendeleo ya ujenzi wa mradi huo kuanzia Stesheni jijini Dar Salaam hadi Soga mkaoni Pwani.

Mabalozi wamefurahishwa na jitihada za Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi madhubuti wa Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli za kuendelea kutekeleza miradi ya  maendeleo kwa kasi  na ufanisi wa hali ya juu kwa manufaa ya Wananchi.  Mabalozi kwa nyakati tofauti wamesema licha ya miradi hii kuliongezea pato Taifa, mara baada ya kukamilika miradi hii itaiweka Tanzania katika nafasi nzuri zaidi ya ushindani wa kibiashara katika soko la Afrika Mashariki na katika ukanda wa Kusini mwa Afrika

Balozi Ramadhani Mwinyi Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akisaini kitabu cha wageni alipoambatana na mabalozi katika ziara ya kikazi Bandari ya Dar es Salaam.
Mhe. Dkt. Asha Rose Migiro Balozi wa Tanzania nchini Uingereza akizungumza wakati wa ziara ya kikazi Bandari ya Dar es Salaam
Mabalozi wakifuatilia wasilisho kuhusu mradi wa upanuzi wa Bandari ya Dar es Salaam

Mabalozi wakisiliza ufafanuzi kutoka kwa mtaalamu wa Shirika la Reli kuhusu mchoro wa mradi mpya wa SGR
Mabalozi wakipanda Treni tayari kwa safari ya kuelekea Soga mkoani pwani, ambapo pamoja na mambo mengine walijionea kiwanda cha kuunda baadhi ya vifaa vya kujengea mradi
Sehemu ya mabalozi wakiangalia mandhari yanayozunguka eneo la mradi wa SGR wakiwa njiani kuelekea kambi ya mradi ya Soga
Sehemu nyingine ya mabalozi wakifurahia jambo wakati wa ziara ya kikazi kutoka stesheni, Dar es Salaam kuelekea  Soga, Pwani. 
Sehemu ya Watendaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki walioambatana na ujumbe wa mabalozi wakati wa kutembelea mradi wa ujenzi wa SGR


Mabalozi wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watendaji wa Wizara, Shirika la Reli na wafanyakazi wa ujenzi wa mradi wa SGR
Baadhi ya Wafanyakazi wakiendelea na majuku ya kutengeneza zana za kujengea mradi wa SGR kwenye kiwanda kidogo kilichopo kambi ya Soga, Pwani.


Thursday, August 15, 2019

Mabalozi wa Tanzania watembelea mradi wa bwawa la kuzalisha umeme la Julius Nyerere







TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

MABALOZI WA TANZANIA WATEMBELEA MRADI MKUBWA UMEME WA JULIUS

NYERERE

Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania nje ya nchi wameipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa kubuni, kutekeleza na kukamilisha miradi mikubwa ya maendeleo yenye manufaa kwa wananchi na Taifa kwa ujumla.

Mabalozi hao kutoka nchi 42 za uwakilishi duniani kote wametoa pongezi hizo tarehe 14 Agosti 2019 walipoutembelea mradi mkubwa wa kufua umeme wa Julius Nyerere uliopo Wilayani Rufiji, mkoani Pwani.

Akizungumza na Vyombo vya Habari kwa niaba ya Mabalozi wengine, Kiongozi wa Mabalozi hao, Mhe. Naimi Aziz, Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia na Umoja wa Afrika amesema kuwa Serikali ya Awamu ya tano chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni ya kupigiwa mfano kwa hatua kubwa iliyofikiawa katika maendeleo ndani ya kipindi kifupi cha uongozi wake.

"Kwa dhati na kwa heshima kubwa tunaipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa hatua hizi kubwa za maendeleo ikiwemo kubuni na kutekeleza miradi mikubwa ya maendeleo yenye manufaa mengi kwa nchi yetu. Sisi mabalozi tunaoiwakilisha Tanzania nje tunaona fahari na tunajivunia kuwa na Rais mchapakazi na tunatembea kifua mbele tunapoiona miradi mikubwa kama hii ikitekelezwa ndani ya nchi yetu”, amesema Balozi Aziz.

Naye Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani, Mhe. Abdallah Possi alieleza kuwa Mabalozi wanaunga mkono jitihada hizi za Serikali na wapo tayari kuendelea kusaidia jitihada hizo ikiwa ni pamoja na kuwaleta nchini wawekezaji na wataalam wenye tija kwa taifa.

Akiwasilisha mada kuhusu mradi huo wa Julius Nyerere utakaozalisha umeme wa Megawatt 2115 kwa kutumia maporomoko ya maji ya Mto Rufiji, Meneja wa Mradi huo, Mhandisi Stephen Manda amesema kuwa mradi huo ambao ni wa nne kwa ukubwa barani Afrika na wa kwanza Afrika Mashariki utakamilika ifikapo mwaka 2022.

Aliongeza kusema kwamba, mradi huo unasimamiwa na watanzania kwa asilimia mia moja na kugharamiwa na Serikali ambapo kiasi cha shilingi trilioni 6.5 zimetengwa kukamilisha mradi huo. Kati ya fedha hizo tayari Serikali imewalipa wakandarasi wa mradi huo ambao ni Kampuni za Arab Contractors na Elsewedy Electric za nchini Misri kiasi cha shilingi trilioni 1.7 ambayo ni asilimia 15 ya fedha zote za mradi huo.

Akielezea faida za mradi huo Mhandisi Manda alisema zipo za kiuchumi, kijamii na  kimazingira.
Kiuchumi mradi huo utaongeza uzaishaji viwandqni kutokana na kuwepo kwa umeme wa uhakika na hivyo kuzalisha ajira kwa vijana. Pia mradi huo utakuza utalii kutokana na maeneo pembezoni mwa bwawa hilo kuwa na nafasi ya kujengwa hoteli na fukwe za kupumzikia. Kijamii Mhandisi Manda amesema kuwa, mradi huo hadi sasa umewawezesha wananchi wa Rufiji kupata huduma mbalimbali za kijamii kwa uhakika kama vile maji, umeme kutokana na mradi huo kupita kwenye eneo lao.

Kuhusu utunzaji mazingira, Mhandisi Manda alieleza kuwa, tahmini ya kina kuhusu mazingira yanayozunguka mradi huo imefanywa na kuwaomba Mabalozi kusaidia kutoa elimu zaidi ili kufuta dhana inayoenezwa kuwa mradi huo utaharibu mazingira. Alifafanua kuwa, Mradi huu pamoja na mambo mengine utachangia utunzaji mazingira kwa kiasi kikubwa kwenye eneo lotelinalouzunguka kwani kutokana na umeme utakaozalishwa wananchi hawataendelea kukata miti kwa ajili ya nishati ya kuni. Pia mradi huo utasaidia kutunza mazingira ya eneo hilo kwa kudhibiti mafuriko yaliyokuwa yanatokea kwenye ukanda wa eneo hilo.

Mradi huo mkubwa wa umeme ulibadilishwa jina na kuitwa Bwawa la Kuzalisha Umeme la Julius Nyerere wakati wa uwekwaji wa jiwe la msingi uliofanywa na Mhe. Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli mwezi Julai 2019 ili kuenzi maono ya Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere ambaye alikuwa na ndoto ya kujenga bwawa hilo wakati wa utawala wake.

Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania nje ya nchi wapo nchini kuanzia tarehe 14 hadi 22 Agosti 2019 kwa ajili ya kushiriki Kikao Kazi chao Maalum pamoja na Mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serial,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dar es Salaam.
15 Agosti 2019

Balozi Ramadhani Mwinyi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, (wakwanza kushoto) akifuatilia uwasilishwaji wa taarifa ya hatua za maendeleo ya ujenzi wa mradi wa kuzalisha umeme wa bwawa la Julius Nyerere (2115MW) unaotekelezwa na Serikali wilayani Rufiji.


Mabalozi wa Tanzania wanaoiwakilisha nchi katika mataifa mbalimbali wakiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Watumishi wa Wizara na Wafanyakazi wa Mradi ,katika moja ya njia ya chini (tunnel) katika mradi wa ujenzi wa bwawa la kuzalisha umeme la Julius Nyerere lililopo katika hifadhi ya Selous wilayani Rufiji. Mabalozi walitembelea maradi huo kujionea hatua mbalimbali za maendeleo ya utekelezaji. Mradi huu unaotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Tano unatarajia kuzalisha Megawati 2115 baada ya kukamilika kwake mwaka 2022.
Mhe. Nahim Azizi Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia akizungumza mara baada ya kuwasili eneo la ujenzi wa mradi
Mabalozi wakisikliza maelezo kuhusu ujenzi wa mradi kutoka kwa Mhandisi Stevene Manda


Mabalozi wakisikiliza hotuba fupi ya ukaribisho kutoka Mhe. Juma Abdallah Njwayo Mkuu wa Wilaya ya Rufiji mara baada ya kuwasili katika eneo la mradi


RAIS CYRIL RAMAPHOSA AWASILI NCHINI KWA ZIARA YA SIKU MBILI.

Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini Mhe. Cyril Ramaphosa akiwa na mkewe Dkt. Tshepo Motsepe wakiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.
Rais Ramaphosa amewasili Nchini kwa Zara ya kikazi ya siku mbili na bade atashiriki Mkutano wa 39 wa Jumuiya ya Maendeleo kwa Nchi za Kusini mua Afrika (SADC)

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akimlaki Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini Mhe. Cyril Ramaphosa katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar Es Salaam. 

Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini Mhe. Cyril Ramaphosa akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe. Kisare Makori.
Wengine judoka kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Daniel Chongolo,Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Sarah Msafiri,Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Sophia Mjema.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwa ameongozana na Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini Mhe. Cyril Ramaphosa.