Friday, August 16, 2019

MABALOZI WA TANZANIA WATEMEBELEA MRADI WA RELI NA UPANUZI WA BANDARI YA DAR ES SALAAM



Mhe. Nahim Azizi Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia na Umoja wa Afrika  akisalimiana na mfanyakazi wa Bandari ya Dar es Salaam akiwa na ujumbe wa mabalozi wengine walipowasili bandarini hapo kwa ziara ya kikazi.


Wakiwa katika Bandari ya Dar es Salaam mabalozi walipata nafasi ya kutembelea mradi wa ujenzi wa upanuzi wa bandari sambamba na kuongeza kina cha bahari ili kuweza kuhudumia meli zinazobeba mzigo mkubwa. 

Mara baada ya kukamilika kwa mradi huo, Bandari ya Dar es Salaam itakuwa na uwezo wa kuhudumia mizigo ya kiasi cha tani milioni 28 kwa mwaka, ikiwa ni mara mbili ya kiwango cha sasa ambapo inauwezo wa kuhudumia mizigo kiasi cha tani milioni 13 pekee. 

Aidha, sambamba na kuongezeka kwa uwezo wa kuhudumia mizigo mingi, pia mradi huo utapunguza muda wa kuhudumia meli kutoka masaa 80 kwa meli moja kama ilivyo sasa hadi masaa 30 mara mradi huo utakapo kamilika.

Wakati huo huo  mabalozi walitembelea mradi wa ujenzi wa wa reli ya kiwango cha kimataifa (SGR) ambapo walipata fursa ya kuona maendeleo ya ujenzi wa mradi huo kuanzia Stesheni jijini Dar Salaam hadi Soga mkaoni Pwani.

Mabalozi wamefurahishwa na jitihada za Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi madhubuti wa Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli za kuendelea kutekeleza miradi ya  maendeleo kwa kasi  na ufanisi wa hali ya juu kwa manufaa ya Wananchi.  Mabalozi kwa nyakati tofauti wamesema licha ya miradi hii kuliongezea pato Taifa, mara baada ya kukamilika miradi hii itaiweka Tanzania katika nafasi nzuri zaidi ya ushindani wa kibiashara katika soko la Afrika Mashariki na katika ukanda wa Kusini mwa Afrika

Balozi Ramadhani Mwinyi Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akisaini kitabu cha wageni alipoambatana na mabalozi katika ziara ya kikazi Bandari ya Dar es Salaam.
Mhe. Dkt. Asha Rose Migiro Balozi wa Tanzania nchini Uingereza akizungumza wakati wa ziara ya kikazi Bandari ya Dar es Salaam
Mabalozi wakifuatilia wasilisho kuhusu mradi wa upanuzi wa Bandari ya Dar es Salaam

Mabalozi wakisiliza ufafanuzi kutoka kwa mtaalamu wa Shirika la Reli kuhusu mchoro wa mradi mpya wa SGR
Mabalozi wakipanda Treni tayari kwa safari ya kuelekea Soga mkoani pwani, ambapo pamoja na mambo mengine walijionea kiwanda cha kuunda baadhi ya vifaa vya kujengea mradi
Sehemu ya mabalozi wakiangalia mandhari yanayozunguka eneo la mradi wa SGR wakiwa njiani kuelekea kambi ya mradi ya Soga
Sehemu nyingine ya mabalozi wakifurahia jambo wakati wa ziara ya kikazi kutoka stesheni, Dar es Salaam kuelekea  Soga, Pwani. 
Sehemu ya Watendaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki walioambatana na ujumbe wa mabalozi wakati wa kutembelea mradi wa ujenzi wa SGR


Mabalozi wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watendaji wa Wizara, Shirika la Reli na wafanyakazi wa ujenzi wa mradi wa SGR
Baadhi ya Wafanyakazi wakiendelea na majuku ya kutengeneza zana za kujengea mradi wa SGR kwenye kiwanda kidogo kilichopo kambi ya Soga, Pwani.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.