Tuesday, August 27, 2019

WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA JAPAN AWAANDALIA HAFLA MAALUM MAWAZIRI WANAOSHIRIKI MKUTANO WA SABA WA TICAD

Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan, Mhe.  Kono Taro akimkaribisha  Waziri wa Mambo ya Nje  na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi alipowasili kwenye Hoteli ya Royal Palace iliyopo jijini Yokohama kwa ajili ya kushiriki hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na Mhe. Taro kwa heshima ya Mawaziri wanaoshiriki Mkutano wa  Saba wa Kimataifa wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Afrika (TICAD 7) unaofanyika nchini humo kuanzia tarehe 28 hadi 30 Agosti 2019.
Mhe. Taro akizungumza wakati wa hafla hiyo ambapo ameendelea kuwahakikishia  ushirikiano Mawaziri kutoka Afrika 
Mhe. Taro akizungumza huku Mawaziri wakimsikiliza
Mhe. Prof. Kabudi akiwa katika meza moja na Mhe. Taro na Mawaziri wengine kutoka nchi za Afrika wanaoshiriki Mkutano wa Saba wa TICAD
Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiwa na Waziri mwenzake wakati wa hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa  na Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan kwa heshima ya Mawaziri kutoka nchi za Afrika wanaoshiriki Mkutano wa Saba wa TICAD
Picha ya pamoja ya Mhe. Taro na Mawaziri kutoka nchi za Afrika wanaoshiriki Mkutano wa Saba wa Kimataifa wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Afrika (TICAD 7) utakaofanyika Yokohama, Japan kuanzia tarehe 28 hadi 30 Agosti 2019
Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi, waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akisalimiana na Mawaziri wenzake akiwemo Waziri wa Mambo ya Nje wa Afrika Kusini, Mhe. Dkt. Naledi Pandor (kulia) mara baada ya kumalizika kwa hafla maalum iliyoandaliwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan, Mhe. Taro.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.