Friday, August 2, 2019

RAIS,DKT MAGUFULI ATIMIZA AHADI YAKE KWA RAIS WA KENYA,MHE.UHURU KENYATTA

Balozi wa Tanzania Nchini Kenya Dkt. Pindi Chana akimkabidhi Rais wa Kenya, Mhe. Uhuru Kenyatta nyaraka ya zawadi maalum ya ndege aina ya Tausi kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli. August 02,2019

Rais wa Kenya, Mhe. Uhuru Kenyatta akizungumza mara baada ya kupokea ndege aina ya Tausi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.Aliyesimama pembeni mwa Rais Kenyatta ni Balozi wa Tanzania Nchini Kenya, Dkt Pindi Chana. August 02,2019

Rais wa Kenya,Mhe. Uhuru Kenyatta akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Tanzania Nchini Kenya,Balozi Pindi Chana mbele ya Zawadi ya ndege aina ya Tausi mara baada ya kukabidhiwa zawadi hiyo. August 02,2019

Ndege aina ya Tausi ambao wamekabidhiwa kwa Rais wa Kenya, Mhe. Uhuru Kenyatta ikiwa ni zawadi kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli. Tausi hao wamekabidhiwa kwa Rais Kenyatta na Balozi wa Tanzania Nchini Kenya Dkt. Pindi Chana. August 02,2019

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.