Thursday, August 15, 2019

RAIS CYRIL RAMAPHOSA AWASILI NCHINI KWA ZIARA YA SIKU MBILI.

Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini Mhe. Cyril Ramaphosa akiwa na mkewe Dkt. Tshepo Motsepe wakiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.
Rais Ramaphosa amewasili Nchini kwa Zara ya kikazi ya siku mbili na bade atashiriki Mkutano wa 39 wa Jumuiya ya Maendeleo kwa Nchi za Kusini mua Afrika (SADC)

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akimlaki Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini Mhe. Cyril Ramaphosa katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar Es Salaam. 

Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini Mhe. Cyril Ramaphosa akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe. Kisare Makori.
Wengine judoka kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Daniel Chongolo,Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Sarah Msafiri,Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Sophia Mjema.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwa ameongozana na Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini Mhe. Cyril Ramaphosa.
 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.