Wednesday, March 4, 2020

DKT. NDUMBARO AKUTANA,KUFANYA MAZUNGUMZO NA MASENETA KUTOKA UFARANSA


Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Maseneta sita (6) kutoka Ufaransa walioko kwenye ziara nchini.

Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ofisi Ndogo za Wizara, jijini Dar es Salaam ambapo ujumbe wa Maseneta hao unaongozwa na Mhe. Hervé Maurey, Mwenyekiti wao ambae pia ni Rais wa Kamati ya Bunge ya Mipango Miji na Maendeleo Endelevu pamoja na Balozi wa Ufaransa nchini Mhe. Frederic Clavier.

Katika mazungumzo hayo ujumbe wa maseneta umeeleza kuridhishwa na jitihada mbalimbali za kuleta maendeleo zinazofanywa na Serikali ya Tanzania katika kukuza uchumi kupitia uwekezaji kwenye miundombinu na kutunza mazingira.

Kwa upande wake Naibu Waziri Dkt. Ndumbaro ametumia fursa hiyo kuueleza ujumbe huo sekta ambazo Tanzania inaweza kushirikiana na Ufaransa ili kukuza zaidi ushirikiano baina ya nchi hizi mbili uliodumu kwa muda mrefu.

Ametaja sekta hizo kuwa ni pamoja na sekta ya kilimo na mifugo, madini, utafiti katika vyuo vikuu pamoja na utalii na utunzaji wa mazingira.

"Katika kipindi hiki Serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Dkt. John Pombe Joseph Magufuli imeweka kipaumbele kuendeleza viwanda hususan viwanda vya kuongeza thamani, amesema Dkt. Ndumbaro.

Naibu Waziri aliongeza kuwa, "Tanzania ina mazingira bora ya uwekezaji na niwasihi tu mtufikishie taarifa hizi kwa wawekezaji wanaoweza kuja kuwekeza nchini katika viwanda vya dawa na vifaa tiba pamoja na kiwanda cha kuunganisha magari," Amesema Dkt. Ndumbaro. 


Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akiongea na Ujumbe wa Maseneta sita (6) kutoka Ufaransa leo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam



Mwenyekiti wa Ujumbe wa Maseneta kutoka Ufaransa, Bw. Herve Maurey (upande wa kulia mwa Naibu Waziri) akifafanua jambo wakati wa maongezi baina yao na Naibu Waziri, Dkt. Ndumbaro katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam



Mwenyekiti wa Maseneta kutoka Ufaransa, Bw. Herve Maurey akimkabidhi zawadi Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro



Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na Ujumbe wa Maseneta kutoka Ufaransa katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam



Tanzania Kuuza Makontena 200 ya Maharage nchini Ubelgiji

Ubalozi wa Tanzania nchini Ubelgiji umepata soko kubwa la maharage machanga ya kijani yanayojulikana kama haricots vertz(green thin beans) nchini Ubelgiji. Soko hilo limepatikana baada ya Balozi wa Tanzania nchini humo, Mhe. Jestas Abuok Nyamanga kufanya mazungumzo  na uongozi wa juu wa kampuni ya CBG-Charlier-Brabo Group inayonunua maharage hayo kutoka sehemu mbalimbali duniani na kuyauza katika supermarkets kubwa za Carrefour, Delhaize na Aldi za nchini Ubelgiji, Luxembourg na nchi nyingine za Ulaya.

Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika tarehe 3 Machi 2020, kampuni hiyo ipo tayari kununua containers kati ya 180-200 za maharage hayo kila mwaka kutoka Tanzania. 

Kupatikana kwa soko la maharage hayo nchini Ubelgiji ni habari njema kwa wakulima wa Tanzania na wafanyabiashara wa mazao ya kilimo hususan wa aina hiyo ya maharage ambayo tayari Tanzania inayauza nchini Uholanzi.

Kampuni hiyo pia imeonesha utayari wa kununua aina nyingine ya maharage ijulikanayo kama red kidney beans na chickpea kwa kiwango cha containers 8 kila mwaka katika hatua za mwanzo.

Ubalozi wa Tanzania unatoa wito kwa Watanzania kuchangamkia upatikanaji wa soko hilo jipya nchini Ubelgiji kwa kuwasiliana na kampuni hiyo kupitia tovuti yao ya www.cbg.be au kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa maelekezo zaidi.

Maharage aina ya haricots vertz(green thin beans) yaliyopata soko nchini Ubelgiji.
Balaozi Jestas Abuok Nyamanga akiwa amebeba maharage yaliyopata soko la kununuliwa na kampuni ya  CBG-Charlier-Brabo Group ya nchini Ubelgiji. Kulia kwake ni Wim Vandenbus scheambayeni Meneja Mauzo na Ununuzi wa kampuni, na kushoto kwa Balozi Nyamanga ni Bi Martine Danneel, ambaye ni Afisa Mauzo wa kampuni. Kushoto zaidi kwa Balazo ni Dr. Geoffrey B. Kabakaki, Afisa Mkuu wa Ubalozi kwa masuala ya uchumi na biashara.
Balozi akiangalia bidhaa aina ya nanasi zilizokatwa na kuifadhiwa katika kopo na kampuni hiyo ambazo pia zinaweza kuagizwa kutoka Tanzania

Tuesday, March 3, 2020

DKT. NDUMBARO AKUTANA, KUFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA CUBA NCHINI


Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) amekutana na kufanya mazugumzo na Balozi wa Cuba nchini Mhe. Prof. Lucas Domingo Hernandez Polledo katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

Katika mazungumo hayo viongozi hao wamekubaliana kuendelea kushirikiana katika sekta ya afya nchin na Cuba imeiomba Tanzania kuinga mkono katika mpango wake wa kugombea kiti katika Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa.

Pamoja na mambo mengine walizungumzia kuhusu jinsi ya kuboresha mahusiano yaliyopo katika kati ya Tanzania na Cuba, ambapo Cuba imekuwa mdau muhimu wa maendeleo ya sekta ya afya nchini.


Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akimsikiliza Balozi wa Cuba nchini Mhe. Prof. Lucas Domingo Hernandez Polledo wakati wa mazungumzo yao yaliyofanyika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam




PROF. KABUDI APOKEA HATI ZA UTAMBULISHO KUTOKA UN, UNHCR


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) amepokea hati za utambulisho kutoka kwa Mratibu Mkazi wa Shughuli za Umoja wa Mataifa (UN) Bw. Zlatan Milišić Pamoja na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) Bw. Antonio Canhandula Jijini Dar es Salaam.

Waziri Kabudi amewaeleza Bw. Milišić na Bw. Canhandula kuwa UN pamoja na UNHCR zimekuwa na mchango mkubwa kwa kuiunga mkono Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kukuza maendeleo pamoja na zile za kushughulikia masuala ya wakimbizi.

“Kwa ujumla UN imekuwa ikisaidia Tanzania kufanikisha agenda zake za maendeleo endelevu ya kijamii, na kiuchumi hivyo Serikali itaendelea kuhakikisha inaendeleza uhusiano huu," Amesema Prof. Kabudi.

Kwa upande wake Mratibu Mkazi wa Shughuli za Umoja wa Mataifa nchini (UN) Bw. Milisic amesema kuwa uhusiano wa UN na Serikali ya Tanzania ni wa muda mrefu na hivyo ni jukumu la UN kuhakikisha inaimarisha uhusiano huo na kuuboresha.

 “Ni matumaini yangu kuwa uhusiano huu tutauboresha vizuri na kuimarisha kwa maslahi mapana na maendeleo endelevu ya taifa la Tanzania," Amesema Bw. Milišić

Nae Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) Bw. Canhandula amesema wanatambua mchango mkubwa ambao Tanzania imekuwa ikiutoa kuhakikisha inaimarisha ulinzi wa maeneo ya wakimbizi ili wananchi wa maeneo hayo waendelee kuishi kwa amani na utulivu pamoja na kupatiwa mahitaji muhimu kama vile malazi na mavazi.

"Kwa kweli UNHCR tunafurahishwa na jinsi Serikali ya Tanzania ambavyo imekuwa ikipokea wakimbizi na kuwapatia baadhi ya mahitaji muhimu……tunaomba tuendeleze ushirikiano huu kwa maendeleo yetu," Amesema Bw. Canhandula.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akimfafanulia jambo Mratibu Mkazi wa Shughuli za Umoja wa Mataifa (UN) Bw. Zlatan Milišić katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiisoma hati ya utambulisho mara baada ya kuipokea kutoka kwa Mratibu Mkazi wa Shughuli za Umoja wa Mataifa (UN) Bw. Zlatan Milišić katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) Bw. Antonio Canhandula akiongea na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) kabla ya kukabidhi hati ya utambulisho katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akipokea hati ya utambulisho kutoka kwa Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) Bw. Antonio Canhandula katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam 



BALOZI MBELWA ATOA RAI KWA WAFANYABIASHARA WA TANZANIA

Mhe. Mbelwa Kairuki Balozi wa Tanzania nchini China, ametoa rai kwa wafanyabiashara wa Tanzania ambao shughuli zao zinahushisha China, kuwa na subira ya kuzuru China wakati huu ambao tatizo la Corona Virus (COVID-19) bado linaendelea kushughulikiwa nchini humo.


Monday, March 2, 2020

MKUTANO WA BARAZA LA MAWAZIRI WA SADC KUFANYIKA TAREHE 16 - 17 MACHI


Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) unatarajiwa kufanyika hapa nchini kuanzia tarehe 11 hadi 17 Machi, 2020 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiriikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) amesema kuwa mkutano huo utafanyika kuanzia tarehe 12 hadi 17 Machi 2020 ambapo utatanguliwa na mkutano wa wataalamu pamoja na Makatibu Wakuu na kufuatiwa na mkutano wa mawaziri tarehe 16 - 17 Machi, 2020.

"Pamoja na mambo mengine, mkutano huu utahusisha Mawaziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mawaziri wa Fedha, Uchumi na Mipango pamoja na Mawaziri wa Viwanda na Biashara," Amesema Prof. Kabudi

Waziri Kabudi amesema kuwa mkutano huo utahudhuriwa na Mawaziri 16 kutoka Nchi wanachama wa SADC za Angola, Namibia, Zambia, Zimbabwe, Comoro, Lesotho, Mauritius, Madagascar, Kongo DRC, Shelisheli, Msumbiji, Afrika Kusini, Tanzania, Malawi, Botswana pamoja na Eswatini)

Aidha, Kwa mujibu wa Mhe. Waziri Kabudi, Mkutano huo utakuwa mkutano wa kwanzawa SADC wa Baraza la Mawaziri kuendeshwa kwa lugha ya Kiswahili baada ya lugha hiyo kuwa miongoni mwa lugha rasmi za Jumuiya hiyo.

Prof. Kabudi aliongeza kuwa, mkutano huo utajadili masuala mbalimbali muhimu kwa mustakabali wa maendeleo na ustawi wa nchi wananchama wa SADC.

"Mktano huu utapokea taarifa na kutolea maelekezo taarifa za vikao mbalimbali vya kisekta vya kamati za mawaziri ambavyo vimefanyika nchini tangu Septemba 2019," Ameongeza Prof. Kabudi.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiriikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo ktk picha) kuhusu Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC utakaofanyika tarehe 11 – 17 Machi, 2020 Jijini Dar es Salaam. Kulia mwenye kilemba ni Bibi. Zamaradi Kawawa, akifuatiwa na Naibu Katibu MKuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhani Mwinyi, kulia kwake ni Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Bibi. Agnes Kayola

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiriikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC utakaofanyika tarehe 11 – 17 Machi, 2020 Jijini Dar es Salaam  




Friday, February 28, 2020

MASENETA WA UFARANSA KUFANYA ZIARA NCHINI


Ujumbe wa maseneta sita (6) kutoka Ufaransa unatarajiwa kufanya ziara nchini kuanzia tarehe 01 hadi 08 Machi, 2020.  

Ujumbe huo utawasili nchini tarehe 29 Februari, 2020 kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Aman Karume Zanzibar utaongozwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge la Ufaransa inayoshughulikia masuala ya Maendeleo Endelevu na Naibu Rais wa Kikundi cha Kirafiki na nchi za Bahari ya Hindi Seneta Harve Maurey.


PROF. KABUDI AHUTUBIA BARAZA LA HAKI ZA BINADAMU LA UMOJA WA MATAIFA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akihutubia katika Kikao cha 43 cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa linaloendelea Geneva,nchini Uswisi ambalo linatarajiwa kumalizika March 20,2020 ambapo masuala kadhaa kuhusu haki za binadamu yanajadiliwa.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akitoa hotuba ya Tanzania katika Kikao cha 43 cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa linaloendelea Geneva,nchini Uswisi ambalo linatarajiwa kumalizika March 20,2020 ambapo masuala kadhaa kuhusu haki za binadamu yanajadiliwa.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akipongezwa na Balozi wa kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Maimuna Tarishi pamoja na baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki mara baada ya kutoa hutuba katika Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa, Geneva, Uswisi

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akipongezwa na baadhi ya viongozi wa Mataifa ya Afrika wanaohudhuria Mkutano wa Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa linaloendelea Geneva,Uswisi




Wednesday, February 26, 2020

PROF. KABUDI AKUTANA NA KATIBU MKUU JUMUIYA YA MADOLA


Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) (katikati aliyeshika kalamu) akiwa katika mazungumzo na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola Bi Patricia Scotland. Kushoto kwa Prof. Kabudi ni Balozi wa kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa Geneva,Uswisi Balozi Maimuna Tarishi pamoja na Wakurugenzi na Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ofisi ndogo za Jumuiya hiyo zilizopo Geneva,Uswisi
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola Bi Patricia Scotland akiwa katika mazungumzo na Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) (hayupo pichani) Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ofisi ndogo za Jumuiya hiyo zilizopo Geneva,Uswisi. Kulia ni msaidizi wa Bi Patriacia Scotland.
Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb)akiwa katika mazungumzo na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola Bi Patricia Scotland.Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ofisi ndogo za Jumuiya hiyo zilizopo Geneva,Uswisi.

Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na  Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola Bi Patricia Scotland mara baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika katika Ofisi ndogo za Jumuiya hiyo zilizopo Geneva,Uswisi. Kushoto kwa Bi. Patricia Scotland ni Balozi wa kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa Geneva,Uswisi Balozi Maimuna Tarishi
Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiagana na  Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola Bi Patricia Scotland mara baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika katika Ofisi ndogo za Jumuiya hiyo zilizopo Geneva,Uswisi.




TANZANIA YAKABIDHIWA TAKWIMU ZA UFANYAJI BIASHARA KATI YAKE NA JUMUIYA YA MADOLA.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola Patricia Scotland mazungumzo yaliyolenga masuala kadhaa ikiwa ni pamoja na mradi ambao Jumuiya ya Madola umeufanya kuhusu Tanzania.

Mradi huo umelenga kuangalia takwimu mbalimbali zinazohusu biashara kwa kuangalia nchi ambazo Tanzania inaagiza ama kuuza bidhaa zake kwa wingi katika nchi za Jumuiya ya Madola mradi ambao umeelezwa kuwa na manufaa makubwa kwa Tanzania ambapo kwa sasa nchi za India na Afrika kusini ndizo kinara.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola Bi Patricia Scotland amesema Tanzania ni mdau muhimu katika jumuiya hiyo na kwamba amefurahi kumkabidhi Prof. Kabudi nakala ya utafiti huo kwa niaba ya Tanzania jambo litakaloifanya Tanzania kuendelea kuangalia maeneo ya kujiimarisha katika ufanyaji wa biashara na nchi za Jumuiya ya Madola.

Mbali na masuala hayo ya mradi huo wa takwimu wa biashara kuhusu Tanzania uliofanywa bure na Jumuiya hiyo ya Madola pia wawili hao wamezungumzia masuala mengine ikiwa ni pamoja na namna Jumuiya hiyo na Tanzania zitakavyofanya kuongeza usawa wa jinsia,masuala ya haki za binadamu pamoja na uimarishaji wa mfumo wa mahakama nchini Tanzania.