Tuesday, March 3, 2020

DKT. NDUMBARO AKUTANA, KUFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA CUBA NCHINI


Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) amekutana na kufanya mazugumzo na Balozi wa Cuba nchini Mhe. Prof. Lucas Domingo Hernandez Polledo katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

Katika mazungumo hayo viongozi hao wamekubaliana kuendelea kushirikiana katika sekta ya afya nchin na Cuba imeiomba Tanzania kuinga mkono katika mpango wake wa kugombea kiti katika Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa.

Pamoja na mambo mengine walizungumzia kuhusu jinsi ya kuboresha mahusiano yaliyopo katika kati ya Tanzania na Cuba, ambapo Cuba imekuwa mdau muhimu wa maendeleo ya sekta ya afya nchini.


Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akimsikiliza Balozi wa Cuba nchini Mhe. Prof. Lucas Domingo Hernandez Polledo wakati wa mazungumzo yao yaliyofanyika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam




No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.